-
Wabunge wa UK: Vikosi vya kijeshi vitakavyoongozwa na UN vipelekwe Ghaza kuzuia mauaji ya kimbari
Sep 18, 2025 03:46Wabunge watano wa Uingereza wamemwandikia barua waziri wao wa mambo ya nje Yvette Cooper wakiitaka serikali ya London "ifuatilie kwa dharura uingiliaji kati wa kijeshi utakaoongozwa na Umoja wa Mataifa" ili kukomesha mauaji ya kimbari ya yanayofanywa na Israel huko Ghaza.
-
Baada ya machafuko ya umwagaji damu, Nepal yateua Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke; UN yakaribisha
Sep 13, 2025 10:52Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayohudumu nchini Nepal yamekaribisha kuteuliwa Sushila Karki kuwa Waziri Mkuu wa mpito, wakati nchi hiyo ikikumbwa na mshtuko kufuatia ukandamizaji wa umwagaji damu dhidi ya maandamano yaliyoongozwa na vijana, ambayo yalisababisha vifo vya zaidi ya watu 50, uharibifu mkubwa wa mali na kujiuzulu kwa mtangulizi wake.
-
Araghchi aikosoa Ulaya kwa kufumbia macho uchokozi wa US, Israel dhidi ya Iran
Sep 12, 2025 07:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi ameyajia juu mataifa matatu ya Ulaya kwa mtazamo wao wa "kutowajibika" mkabala wa uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani na Israel dhidi ya Iran, pamoja na vitisho vyao vya kuhuisha maazimio yaliyobatilishwa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jambo ambalo anaamini litazidisha tu mivutano iliyopo.
-
Kwa nini UN imetoa wito wa kuondolewa vikwazo vya Marekani dhidi ya makundi ya kutetea haki za binadamu ya Palestina?
Sep 08, 2025 08:58Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, amekosoa vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya makundi ya kutetea haki za binadamu ya Palestina, na kutoa wito wa kuondolewa mara moja.
-
Msimamo wa karibuni wa Malaysia kuhusiana na utawala wa kizayuni na jinai unazofanya Ghaza
Sep 01, 2025 07:24Malaysia imeitaka Jamii ya Kimataifa isimamishe uwanachama wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Umoja wa Mataifa na kuuwekea vikwazo vikali utawala huo ghasibu.
-
Wasia wa ripota Mpalestina aliyeuliwa kigaidi na Israel kwa walimwengu: 'Msiisahau Ghaza'
Aug 11, 2025 10:49Anas al-Sharif, ripota mashuhuri wa chaneli ya Al Jazeera aliyeuliwa shahidi pamoja na wenzake wanne katika shambulio la makusudi lililofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel kwenye hema la waandishi wa habari katika Mji wa Ghaza, amewaomba walimwengu katika wasia wake wasiisahau Ghaza iliyowekewa mzingiro pamoja na watu wa Palestina.
-
UNICEF: Watoto wanafariki Ghaza kwa kasi ambayo 'haijawahi kushuhudiwa'
Aug 02, 2025 13:16Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limeitaka jamii ya kimataifa ichukue hatua za haraka ili kuzuia vifo vingi vya watoto katika Ukanda wa Ghaza, ambako hali inaendelea kuwa mbaya wakati huu wa vita vinavyoendelezwa na utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya eneo hilo uliloliwekea mzingiro.
-
Maafisa wa Uingereza na Umoja wa Mataifa waitaka London kulitambua rasmi taifa la Palestina
Jul 24, 2025 12:09Zaidi ya maafisa 50 wa zamani wa Uingereza na Umoja wa Mataifa wamemwandikia barua Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer wakimtaka alitambue rasmi taifa la Palestina.
-
UN yasema SDG hatarini kuweza kufikiwa katika anga ya kisiasa iliyopo
Jul 22, 2025 18:06Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia kuongeza kasi na dhamira ya kweli katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) yanayofikia ukomo wake 2030, akisisitiza kuwa malengo hayo yako hatarini kuweza kufikiwa katika anga ya kisiasa iliyopo hivi sasa duniani.
-
WFP: Theluthi moja ya watu wa Ghaza hawajala kwa siku kadhaa kutokana na mzingiro wa Israel
Jul 22, 2025 10:05Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetangaza kuwa, theluthi moja ya wakazi wa Ukanda wa Ghaza hawajala kwa siku kadhaa kutokana na mzingiro unaoendelea kuwekwa na utawala wa kizayuni wa Israel kwenye eneo hilo la Palestina.