Apr 18, 2024 07:08
Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa imehusika na shambulio lililolenga kituo cha kijeshi kaskazini mwa 'Israel' na kuwajeruhi wanajeshi wasiopungua 14, na kusema, shambulio hilo limefanywa kulipiza kisasi cha mashambulizi ya utawala wa Kizayuni yaliyoua wanachama wa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu.