-
Kamanda Qaani: Palestina ni fikra iliyo hai na isiyobadilika
Aug 24, 2026 06:08Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran amesema: "Suala la kukomboa Palestina, kuanzia baharini hadi mtoni, (ardhi ya Palestina kuanzia Bahari ya Mediterania hadi Mto Jordan) liko hai zaidi na linawezekana kutimizwa sasa kuliko hapo awali."
-
Baada ya kukana kwa zaidi ya miaka 2, Israel yakiri kumuua mtoto wa Kipalestina Hind Rajab
Aug 20, 2026 11:40Kwa mara ya kwanza, jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limekiri kuwa lilimuua Hind Rajab mtoto wa Kipalestina mwenye umri wa miaka mitano huko Ghaza, na hivyo kubatilisha makanusho yake ya hapo awali, na kutangaza kwamba limeshaagiza kufanyika uchunguzi wa kijinai kuhusiana na mauaji yake.
-
Israel imepora hekta 25,000 za ardhi ya Ukingo wa Magharibi katika miaka mitatu iliyopita
Aug 20, 2026 03:18Utawala dhalimu wa Israel umepora hekta 25,000 za ardhi ya Ukingo wa Magharibi katika miaka mitatu iliyopita.
-
Iran yalaani kauli ya waziri wa Israel, Ben-Gvir ya kuhamasisha mauaji dhidi ya Wapalestina, Gaza
Aug 18, 2026 03:27Mwanadiplomasia mwandamizi wa Iran ameeleza ghadhabu yake baada ya waziri mmoja wa itikadi kali wa utawala wa Kizayuni wa Israel kushauri kwamba utawala huo unapaswa kuwaua Wapalestina wa Ukanda wa Gaza kwa misingi ya “kiwango cha mauaji ya kila usiku.”
-
Israel imebomoa kikamilifu misikiti 1,076 Ghaza, imeharibu 165 na kubakisha 34 tu
Aug 15, 2026 03:40Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kidini ya Ghaza imetangaza kuwa, kati ya jumla ya misikiti 1,275 ya eneo hilo la Palestina inayokaliwa kwa mabavu, 1,076 imebomolewa kikamilifu, 165 imebomolewa baadhi ya sehemu, na misikiti 34 pekee ndiyo iliyosalimika na jinai za jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Mwanzilishi mwenza aonya: Wikipedia imekuwa chombo cha propaganda cha CIA, taasisi zingine zenye nguvu
Aug 09, 2026 11:02Mwanzilishi mwenza wa Wikipedia, Lawrence Mark Sanger, ameonya kwamba ensaiklopidia hiyo ya mtandaoni imekuwa chombo cha propaganda, akisema Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na marekebisho yanayofanywa na makampuni mbalimbali kwenye Wikipedia yamedhoofisha sera yake ya kutopendelea upande wowote.
-
Mkuu wa Mossad awatimua maafisa wawili wakuu kwa kufeli mpango wa kuipindua serikali ya Iran
Aug 07, 2026 12:29Mkuu wa shirika la ujasusi na ugaidi la utawala wa kizayuni wa Israel Mossad, Roman Gofman, amewafukuza kazi maafisa wawili wakuu wa intelijensia baada ya kushindwa au kutotekelezwa mpango wa kuipindua serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais wa Somalia: Tutazuia Israel kuimarisha ushawishi wake Somaliland
Aug 03, 2026 11:10Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud, amesema kwamba Serikali ya Shirikisho itachanganya "nguvu na hekima" ili kuzuia "Israel" kupata nafasi au kuanzisha ushawishi wa kudumu katika eneo la "Somaliland," akisisitiza kwamba Mogadishu ingali inashikamana na umoja wa ardhi na mamlaka ya Somalia, na inapinga kwa nguvu zote kuhamisha migogoro ya "Mashariki ya Kati" hadi eneo la Pembe ya Afrika.
-
Muqawama wa Palestina watoa onyo baada ya mashambulizi mabaya zaidi ya Israel tangu kusitisha mapigano
Aug 03, 2026 10:10Makundi ya Muqawama ya Palestina yametoa onyo kali baada ya mashambulizi mabaya zaidi ya anga ya Israel tangu kusitisha mapigano Oktoba 2025, yakisema mashambulizi hayo yasiyokoma ni hujuma ya makusudi dhidi ya makubaliano ya kusitisha mapigano na ujumbe kwamba Israel haina nia ya kutimiza majukumu yake.
-
Vibaraka wawili wa Mossad wanyongwa nchini Iran kwa kutoa taarifa za usalama kwa Israel
Aug 03, 2026 09:48Wanaume wawili waliopatikana na hatia ya kufanya ujasusi kwa maslahi ya shirika la ujasusi la Israel, Mossad, wamenyongwa kwa kosa la kutoa taarifa nyeti kuhusu jeshi na maeneo ya usalama ya Iran katika vita vya hivi karibuni vya Marekani na Israel.