-
Waziri wa kizayuni aeleza 'anavyofurahishwa' na mateso wanayopata wafungwa Wapalestina
Aug 30, 2026 13:28Waziri wa usalama wa ndani wa utawala wa kizayuni wa Israel, Itamar Ben-Gvir, amesema "anafurahishwa" na unyanyasaji wa wafungwa Wapalestina walioko kwenye jela za utawala huo na kuongeza kwamba yeye anahusika moja kwa moja na hali zinazoshuhudiwa katika jela hizo.
-
Israel inanyakua maelfu ya ekari za ardhi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi
Aug 27, 2026 11:52Mamlaka za utawala wa Kizayuni wa Israel zimetwaa maelfu ya ekari za ardhi ya Wapalestina katikati mwa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu ili kujenga kile kinachoitwa "njia ya usalama" kuzunguka vitongoji haramu vya Wazayuni kinyume cha sheria za kimataifa na maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran: Iran kupanua kwa mafanikio mifumo ya ulinzi
Aug 27, 2026 04:24Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran amesema kuwa Iran inapiga hatua mbele kwa kutegemea kikamilifu uwezo wake wa ndani, ikipanua mifumo yake ya ulinzi wa anga na kuzalisha nakala za mifumo ile iliyofanya vyema wakati wa vita vya siku 40.
-
Kamanda Qaani: Palestina ni fikra iliyo hai na isiyobadilika
Aug 24, 2026 06:08Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran amesema: "Suala la kukomboa Palestina, kuanzia baharini hadi mtoni, (ardhi ya Palestina kuanzia Bahari ya Mediterania hadi Mto Jordan) liko hai zaidi na linawezekana kutimizwa sasa kuliko hapo awali."
-
Baada ya kukana kwa zaidi ya miaka 2, Israel yakiri kumuua mtoto wa Kipalestina Hind Rajab
Aug 20, 2026 11:40Kwa mara ya kwanza, jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limekiri kuwa lilimuua Hind Rajab mtoto wa Kipalestina mwenye umri wa miaka mitano huko Ghaza, na hivyo kubatilisha makanusho yake ya hapo awali, na kutangaza kwamba limeshaagiza kufanyika uchunguzi wa kijinai kuhusiana na mauaji yake.
-
Israel imepora hekta 25,000 za ardhi ya Ukingo wa Magharibi katika miaka mitatu iliyopita
Aug 20, 2026 03:18Utawala dhalimu wa Israel umepora hekta 25,000 za ardhi ya Ukingo wa Magharibi katika miaka mitatu iliyopita.
-
Iran yalaani kauli ya waziri wa Israel, Ben-Gvir ya kuhamasisha mauaji dhidi ya Wapalestina, Gaza
Aug 18, 2026 03:27Mwanadiplomasia mwandamizi wa Iran ameeleza ghadhabu yake baada ya waziri mmoja wa itikadi kali wa utawala wa Kizayuni wa Israel kushauri kwamba utawala huo unapaswa kuwaua Wapalestina wa Ukanda wa Gaza kwa misingi ya “kiwango cha mauaji ya kila usiku.”
-
Israel imebomoa kikamilifu misikiti 1,076 Ghaza, imeharibu 165 na kubakisha 34 tu
Aug 15, 2026 03:40Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kidini ya Ghaza imetangaza kuwa, kati ya jumla ya misikiti 1,275 ya eneo hilo la Palestina inayokaliwa kwa mabavu, 1,076 imebomolewa kikamilifu, 165 imebomolewa baadhi ya sehemu, na misikiti 34 pekee ndiyo iliyosalimika na jinai za jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Mwanzilishi mwenza aonya: Wikipedia imekuwa chombo cha propaganda cha CIA, taasisi zingine zenye nguvu
Aug 09, 2026 11:02Mwanzilishi mwenza wa Wikipedia, Lawrence Mark Sanger, ameonya kwamba ensaiklopidia hiyo ya mtandaoni imekuwa chombo cha propaganda, akisema Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na marekebisho yanayofanywa na makampuni mbalimbali kwenye Wikipedia yamedhoofisha sera yake ya kutopendelea upande wowote.
-
Mkuu wa Mossad awatimua maafisa wawili wakuu kwa kufeli mpango wa kuipindua serikali ya Iran
Aug 07, 2026 12:29Mkuu wa shirika la ujasusi na ugaidi la utawala wa kizayuni wa Israel Mossad, Roman Gofman, amewafukuza kazi maafisa wawili wakuu wa intelijensia baada ya kushindwa au kutotekelezwa mpango wa kuipindua serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.