-
Kuanguka kizoro katika uso wa Israel - Mwaka wa Pili wa Kimbunga cha al Aqsa
Oct 07, 2025 10:35Historia muda wote imethibitisha kwamba, msimamo imara na kutotetereka mataifa ya dunia katika kupigania ukombozi, siku zote hushinda utumiaji mabavu, vita, njama na mauaji ya umati. Hiyo ni ahadi ya Qur'ani Tukufu ambapo katika Surat Muhammad, aya ya 7 tunasoma: "Mkimnusuru Mwenyezi Mungu basi na Yeye atakunusuruni."
-
Araghchi: Israel inatumia mamilioni ya dola kulipa watu waongope mitandaoni
Oct 07, 2025 07:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi ameshutumu kampeni ya propaganda iliyofichuliwa hivi karibuni ya Israel, yenye lengo la kuhamasisha uungwaji mkono kwa utawala huo kwenye mitandao ya kijamii.
-
Iran yataka OIC kuchukua hatua ya kuipiga marufuku Israel katika michezo ya dunia
Oct 05, 2025 10:42Waziri wa Michezo na Vijana wa Iran, Ahmad Donyamali amewataka mawaziri wenzake katika Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kuunda muungano wa pamoja dhidi ya utawala wa Israel ambao utasaidia kuupiga marufuku utawala huo wa Kizayuni kwenye michezo ya kimataifa.
-
Yemen yafanya mashambulizi mapya ya makombora dhidi ya Israel; sauti za ving'ora zasikika
Oct 05, 2025 07:37Ving'ora vya mashambulizi ya anga vimesikika katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu (Israel) kufuatia kombora la balestiki lililovurumishwa na Jeshi la Yemen ili kulipiza kisasi vita vya mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala ghasibu wa Israel huko Gaza.
-
Israel yampuuza Trump, yaendelea kuwaua Wapalestina Gaza; Hamas yalaani
Oct 05, 2025 02:47Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imemjia juu Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwa madai ya uwongo kuwa ameliamuru jeshi la utawala huo kupunguza mashambulizi yake katika Ukanda wa Gaza.
-
Mbinu ya ulaghai ya Trump; Je, shambulio dhidi ya Qatar litachukuliwa kuwa tishio la usalama dhidi ya Marekani?
Oct 04, 2025 02:26Trump ametoa amri ya kiutendaji akidai kuwa shambulio lolote katika ardhi ya Qatar litahesabiwa kuwa tishio la usalama kwa Marekani.
-
Mkuu wa UNRWA atoa indhari: Israel inaelekea kufanya "mauaji ya halaiki ya idadi kubwa" katika Mji wa Ghaza
Oct 03, 2025 10:40Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), Philippe Lazzarini, ametahadharisha kwamba utawala wa kizayuni wa Israel inaonekana unapanga kufanya "mauaji ya halaiki ya idadi kubwa" katika Mji wa Ghaza huku ukiwa unashadidisha mzingiro wake na mashambulizi makubwa ya kijeshi dhidi ya mji huo.
-
FIFA iliyoipiga marufuku Russia kwa sababu ya vita vya Ukraine yasema haiwezi kuchukua hatua dhidi ya Israel
Oct 03, 2025 10:34Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino amesema, taasisi hiyo haiwezi kutatua ‘masuala ya kijiopolitiki’, licha ya kuendelea kuandamwa na mashinikizo kimataifa ya kuitaka isimamishe uanachama wa Israel kutokana na vita vya kinyama na mauaji ya kimbari unayoendelea kufanya utawala huo wa kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ghaza, ambayo hadi sasa yameshateketeza roho za watu zaidi ya 65,000, wengi wao wakiwa wanawake na watoto.
-
Afrika Kusini yaitaka Israel iwaachie wanaharakati wa msafara wa Sumud
Oct 03, 2025 03:30Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa jana Alkhamisi alitaka kuachiliwa mara moja kwa Waafrika Kusini na raia wengine wa kigeni wanaozuiliwa na jeshi la Israel, baada ya wanajeshi wa majini wa utawala huo haramu kushambulia msafara wa kibinadamu uliokuwa unaelekea Gaza.
-
Colombia yawatimua wanadiplomasia wa Israel kwa kuvamiwa msafara wa Sumud, yasema Trump ni wa kufungwa jela
Oct 02, 2025 03:25Colombia imewafukuza wanadiplomasia wa utawala wa kizayuni wa Israel kwa uchokozi uliofanywa na utawala huo ghasibu wa kuuvamia kijeshi msafara wa kimaataifa wa meli unaojulikana kama Sumud uliokuwa ukielekea Ukanda wa Ghaza kwa ajili ya kufikisha misaada ya kibinadamu; sambamba na hilo, serikali ya Bogota imehimiza rais wa Marekani Donald Trump afungwe jela kwa ushiriki wa Washington katika mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na jeshi la kizayuni katika eneo hilo la ardhi ya Palestina.