-
Misri yaitisha kikao cha dharura cha Umoja wa Afrika kupinga hatua ya Israel kutambua "Somaliland"
Dec 30, 2025 03:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty, Jumatatu alitoa wito wa kufanyika kikao cha dharura cha Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika ili kupinga hatua ya utawala wa Israel kutambua jimbo lililojitenga na Somalia la Somaliland kama nchi huru.
-
Makumbusho ya taifa ya Libya yafunguliwa tena baada ya miaka 14
Dec 29, 2025 23:14Kufunguliwa tena kwa Jumba la Makumbusho Taifa la Libya baada ya kufungwa kwa miaka 14 kunatoa matumaini ya kurejea utulivu nchini humo na kujumuishwa utambulisho wa kitaifa.
-
EAC yaunga mkono mamlaka ya kujitawala Somalia baada ya Israel kuitambua rasmi Somaliland
Dec 29, 2025 06:26Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imevunja ukimya wake kuhusu hali ya mvutano unaoendelea nchini Somalia na Somaliland, na kuthibitisha uungaji mkono wake kwa Somalia.
-
Wasomali waandamana kuilaani Israel kwa kuitambua Somaliland
Dec 29, 2025 06:20Mamia ya wanachi wa Somalia jana Jumapili walifanya maandamano katika mji mkuu wa nchi hyo, Mogadishu kupinga na kulaani uamuzi wa utawala haramu wa Israel wa kuitambua kana nchi huru Somaliland, eneo la kaskazini mwa Somalia ambalo lilijitangazia uhuru wake mwaka 1991.
-
UN: Zaidi ya watu 10,000 wamelazimika kuhama makwao ndani ya siku tatu nchini Sudan
Dec 29, 2025 03:02Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa zaidi ya watu 10,000 wamelazimika kuhama makazi yao katika siku tatu katika majimbo ya Darfur Kaskazini na Kordofan Kusini mwa Sudan, huku vita vikiendelea nchini humo kati ya jeshi la taifa na wanamgambo wa RSF.
-
Uchaguzi wa urais Kenya ukifanyika leo Ruto atashinda, lakini utaingia katika duru ya pili
Dec 28, 2025 23:50Utafiti uliofanywa na kampuni ya Infotrak unaonyesha kuwa, endapo uchaguzi wa urais wa Kenya ungefanyika hivi leo, Rais William Ruto angeibuka mshindi; hata hivyo uchaguzi huo ungelazimu kuingia katika duru ya pili kwa sababu ushindi wake usingevuka kiwango cha asilimia 50+1 ya kura kinachohitajika.
-
Vikwazo vya UK vyazilazimisha Angola na Namibia zikubali kupokea wahamiaji wanaorejeshwa
Dec 28, 2025 23:50Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uingereza imetangaza kuwa, Angola na Namibia zimekubali kuruhusu kurejeshwa katika nchi hizo wahamiaji wasio rasmi na wahalifu baada ya serikali ya Uingereza kutishia kutoa adhabu ya vikwazo vya viza kwa nchi zinazokataa kutoa ushirikiano.
-
Baraza la Usalama na Arab League kukutana kujadili hatua ya Israel ya kuitambua rasmi Somaliland
Dec 28, 2025 08:07Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) zimepanga kufanya mikutano tofauti wiki hii kujadili matokeo ya hatua ya Israel ya kulitambua rasmi eneo la 'Somaliland, ambalo limejitenga na Somalia, kama taifa huru na lenye mamlaka kamili.
-
Wanawake na watoto ni kati watu zaidi ya 200 waliouawa katika mauaji mapya ya kikabila huko Darfur
Dec 28, 2025 07:09Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa watu zaidi ya 200, wakiwemo wanawake na watoto wameuawa katika mashambulizi ya kikabila yaliyofanywa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) huko Darfur nchini Sudan.
-
Jamhuri ya Afrika ya Kati yaendesha uchaguzi mkuu,Touadéra anawania muhula wa tatu wa urais
Dec 28, 2025 06:52Raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati waliotimiza masharti ya kupiga kura leo wameelekea kwenye masanduku ya kura katika zoezi la uchaguzi mkuu huku Rais Archange Touadéra akiwania kiti cha urais kwa muhula wa tatu.