-
Minawi aonya dhidi ya kugawanyika tena Sudan
Nov 09, 2025 22:51Gavana wa Darfur, Minni Arko Minnawi, ameonya kwamba makubaliano yoyote ya kusitisha mapigano nchini Sudan ambayo hayajumuishi ulinzi wa raia na kuwajibishwa wahusika wa uhalifu "yatakuwa na maana ya mgawanyiko wa Sudan," na ametoa wito wa kuondoka wale aliowaita "Janjaweed na mamluki" - akikusudia Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF)- katika maeneo ya makazi ya raia, hospitali na mijini.
-
Magaidi watatu vinara wa al-Shabaab wauawa katika operesheni ya jeshi la Somalia
Nov 09, 2025 22:50Jeshi la Somalia jana Jumapili lilifanya oparesheni kadhaa katika majimbo ya Bakool na Bay na kuuwa wanachama wa ngazi ya juu wa kundi la kigaidi la al Shabaab.
-
Mtandao wa Madaktari Sudan: RSF imeteketeza mamia ya miili ya watu huko El Fasher
Nov 09, 2025 06:34Mtandao wa Madaktari wa Sudan umesema kwamba Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilikusanya mamia ya miili kutoka mitaani na vitongoji vya makazi ya raia vya El Fasher (mji mkuu wa Darfur Kaskazini) na kuzika baadhi ya miili hiyo katika makaburi ya umati, huku mingine ikichomwa moto kabisa.
-
Maandamano yazuka Nigeria kufuatia tishio la Trump la kuivamia nchi hiyo kijeshi
Nov 09, 2025 03:48Wananchi walimiminika mitaani siku ya Jumamosi katika jiji la Kano, kaskazini mwa Nigeria, kupinga vitisho vya Rais Donald Trump wa Marekani, vya kuivamia nchi hiyo kijeshi.
-
UNHCR yahimiza jamii ya kimataifa kuwasaidia wakimbizi wa Sudan nchini Chad
Nov 08, 2025 23:09Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetoa mwito wa dharura wa kusaidiwa sana kimataifa maelfu ya watu waliokimbilia Chad kukwepa mauaji ya kimbari nchini Sudan. Wasudan wanaendelea kumiminika katika nchi jirani ya Chad kutoka eneo la Darfur la magharibi mwa Sidan.
-
Wamorocco waandamana kuunga mkono Palestina na kulaani mzingiro Gaza
Nov 08, 2025 07:02Maelfu ya wananchi wa Morocco wameingia mitaani na kushiriki maandamano ya kutangaza mshikamano wao na wananchi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza, sanjari na kulaani mzingiro dhidi ya Gaza na njama za Israel za kukwamisha upelekaji misaada ya kibinadamu katika ukanda huo.
-
AU yatoa wito wa kuheshimiwa mamlaka ya kujitawala Nigeria, yapinga vitisho vya Trump
Nov 08, 2025 04:28Tume ya Umoja wa Afrika imeelezea wasiwasi wake kuhusu kauli za hivi karibuni za Marekani, ambazo zimeituhumu serikali ya Nigeria kuwa inashiriki katika mauaji iliyodai kuwa yanayowalenga Wakristo, na kudokeza uwezekano wa kuingilia kijeshi kwa kisingizio cha "kutetea uhuru wa kidini."
-
Ghannouchi na wanaharakati wa kisiasa wagoma kula kuonyesha mshikamano na Ben Mbarek
Nov 08, 2025 04:27Timu ya utetezi ya Rached Ghannouchi, spika wa zamani wa Bunge la Tunisia na mkuu wa harakati ya Ennahda, ilitangaza jana Ijumaa kwamba mwanasiasa huyo mkongwe ameanza mgomo wa kula usio na kikomo kuonyesha mshikamano na Jaouhar Ben Mbarek, ambaye ni miongoni mwa viongozi wa kundi la National Salvation Front and Citizens Against the Coup linalompinga Rais wa Tunisia, Kais Saied.
-
Balozi wa Russia nchini Sudan: Mamluki wa Ukraine wanaendeshaji droni huko Darfur
Nov 08, 2025 03:45Balozi wa Russia nchini Sudan, Andrey Chernovol, ameripoti kwamba kuna uvumi unaosambaa nchini Sudan kuhusu uwepo wa Waukreini wanasimamia operesheni za ndege zisizo na rubani katika safu ya waasi wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF).
-
Mahakama ya ICC yathibitisha mashtaka dhidi ya Joseph Kony
Nov 08, 2025 00:40Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC yenye makao yake mjini Hague, Uholanzi wamethibitisha kuwa kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony anakabiliwa na mashtaka ya jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu na hivyo kufungua njia kwa ajili kuanza kesi yake iwapo tu atatiwa nguvuni.