-
Umoja wa Mataifa wataka hatua za haraka zichukuliwe kuzuia ukatili El-Fasher Sudan
Oct 03, 2025 23:09Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka ili kuzuia mauaji makubwa ya kikabila yanayoendelea kutekelezwa kwenye mji wa El-Fasher, magharibi mwa Sudan.
-
Makabiliano makali yazuka kati ya waandamanaji na polisi katika maandamano ya Gen Z nchini Morocco
Oct 03, 2025 23:08Maandamano yanaendelea nchini Morocco, kushinikiza mageuzi kuhusu namna huduma zinavyotolewa kwa wananchi, lakini pia kumaliza visa vya ufisadi.
-
Kenya yawahakikishia raia wake wanaofanya biashara Tanzania: Hamtaguswa na agizo jipya la leseni
Oct 03, 2025 07:05Serikali ya Kenya imewahakikishia raia wake wanaofanya biashara nchini Tanzania kwamba hawataguswa na agizo jipya la leseni lililotolewa hivi karibuni na serikali ya Tanzania.
-
Watu 14 wauawa katika shambulizi dhidi ya kambi ya wakimbizi mashariki mwa DRC
Oct 03, 2025 04:06Takriban watu 14 wameuawa siku ya Alhamisi katika shambulizi lililofanywa na makundi ya wanamgambo dhidi ya kambi ya wakimbizi wa ndani katika jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani.
-
Nguzo za kanisa zaporomoka Ethiopia na kuua watu 36
Oct 02, 2025 10:20Takriban watu 36 waliuawa na zaidi ya 200 kujeruhiwa katika tamasha la kidini katikati mwa Ethiopia, wakati viunzi vya mbao vilipowaangukia ndani ya kanisa lililokuwa likiendelea kujengwa.
-
Tanzania yakanusha ripoti ya HRW kuhusu ukandamizaji wa haki za binadamu
Oct 02, 2025 08:38Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekana madai kwamba ukandamizaji wa kisiasa umeongezeka nchini humo wakati taifa hilo linapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
-
Maandamano yashtadi Madagascar huku Rais akishinikizwa kujiuzulu
Oct 02, 2025 04:25Mitaa mbali ya Madagascar jana Jumatano ilishuhudia maandamano ya wananchi wanaoshinikiza kujiuzulu raia wa nchi hiyo. Polisi ya nchi hiyo kwa upande wake walichukua hatua za kuzuia kuibuka ghasia katika maandamano hayo.
-
Somalia yaridhia katiba ya Afrika kuhusu haki na ustawi wa watoto
Oct 02, 2025 04:24Bunge la Shirikisho la Somalia jana lilipasisha Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto baada ya wabunge kukutana mjini Mogadishu.
-
WHO: Mlipuko wa Ebola Kongo waonyesha dalili za kupungua maambukizi
Oct 02, 2025 04:24Shirika la Afya Duniani( WHO) limetangaza kuwa mlipuko wa wa ugonjwa wa Ebola kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unaonyesha "dalili za kupungua kwa maambukizi".
-
Rais wa Nigeria atangaza ‘hali mbaya zaidi imepita’
Oct 01, 2025 23:15Rais wa Nigeria, Bola Ahmed Tinubu, ameadhimisha miaka 65 ya uhuru wa taifa lake kwa hotuba iliyojumuisha heshima kwa waasisi wa taifa na tathmini ya mageuzi aliyosema yameinusuru nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika kutoka kwenye janga la kiuchumi.