-
Wabunge wa Iran waandaa muswada wa kuimarisha vikosi vya ulinzi kwa vita kamili na Israel
Jul 13, 2025 10:46Wabunge wa Iran wamo mbioni kuandaa mswada wa kuongeza bajeti ya matumizi ya kijeshi kwa lengo la kuviimarisha Vikosi vya Ulinzi kwa ajili ya makabiliano ya kijeshi ya pande zote na utawala haramu wa kizayuni wa Israel.
-
UNESCO yaongeza Bonde la Khorramabad la Iran kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia
Jul 13, 2025 10:46Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeongeza rasmi maeneo ya kale ya enzi ya mawe katika Bonde la Khorramabad, lililoko katika jimbo la Lorestan, magharibi mwa Iran, kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia.
-
Nini madhumuni ya barua mpya ya Iran kwa Baraza la Usalama kuhusiana na uvamizi wa kijeshi wa Israel dhidi ya Iran?
Jul 12, 2025 23:05Amir Saeid Iravani Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amemuandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama la umoja huo, na kuwasilisha ripoti iliyosasishwa kuhusu uharibifu uliosababishwa na uvamizi mkubwa wa kijeshi na wa bila ya sababu wa utawala wa Israel dhidi ya Iran.
-
Iran: Imani yetu kwa Marekani imeporomoka mno
Jul 12, 2025 12:30Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema Marekani imedhoofisha diplomasia na kukiuka sheria za kimataifa kwa mashambulizi yake ya kichokozi dhidi ya taifa hili, wakati mazungumzo ya nyuklia yalipokuwa yakiendelea, na hivyo kupunguza imani ya Iran kwa Marekani chini ya sifuri.
-
Araghchi: Iran haijasitisha ushirikiano wake na IAEA
Jul 12, 2025 10:59Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, ushirikiano wa Iran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki haujasimamishwa na kusisitiza kuwa, sisitizo la Ulaya kuhusu kuhuisha mchakato wa kurejeshwa vikwazo vya nyuklia dhidi ya Tehran litahitimisha jukumu lao katika faili la atomiki la Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kamanda Mkuu: Jeshi la Iran liko katika hali ya juu ya utayarifu wa kivita
Jul 12, 2025 03:55Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Iran amethibitisha kwamba Jeshi la Nchi hii linaendelea kudumisha kiwango cha uwezo wake “kamili.” Ametoa kauli hii chini ya mwezi mmoja tangu Majeshi ya Iran yalipojibu haraka na kwa ufanisi mashambulizi ya Israel, yaliyomlazimu adui Muisraeli kuomba kusitisha mapigano.
-
Iran inachunguza ombi la Marekani kuhusu kuanza tena mazungumzo ya nyuklia
Jul 12, 2025 03:38Mshauri mwandamizi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei, amethibitisha kuwa Iran imepokea ombi kutoka Marekani kuhusu kuanza tena mazungumzo ya nyuklia, na amesema kwa sasa Tehran inachunguza pendekezo hilo kwa kina.
-
Iran yaijia juu Marekani kwa kumwekea vikwazo Ripota wa UN
Jul 11, 2025 12:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei ameikosoa vikali Marekani kwa kumwekea vikwazo Francesca Albanese, Ripota Maalum wa Umoja wa Mataifa katika ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Tuhuma dhidi ya Iran zaendelea licha ya Grossi kukiri tena kwamba Iran haitengenezi silaha za nyuklia
Jul 11, 2025 23:04Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesisitiza kuwa, hakuna ushahidi wa kuaminika kwamba Iran imepata silaha za nyuklia na kusisitiza ulazima wa kutatuliwa kidiplomasia suala la nyuklia la Iran.
-
Kamanda: Hatutaruhusu hata shibri moja ya ardhi ya Iran itwaliwe
Jul 11, 2025 11:52Mkuu wa Jeshi la Iran, Meja Jenerali Amir Hatami, amesisitiza kuwa wanajeshi wa nchi hii hawataruhusu hata shubri moja ya ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu kuporwa.