-
Ali Larijani ateuliwa Mkuu Mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran
Aug 06, 2025 04:30Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemteua mwanasiasa mkongwe Ali Larijani kuwa Mkuu Mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC).
-
Iran yasambaza vifurushi vya chakula na maji kwa wakaazi wa Gaza
Aug 06, 2025 00:26Shirika la Hilali Nyekundu la Iran limesambaza vifurushi vya chakula na maji katika Ukanda wa Gaza ili kusaidia mahitaji ya dharura ya wakaazi wa Ukanda huo ambao wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa mahitaji ya dharura kama chakula na maji.
-
Balozi wa Iran nchini Denmark: Ulimwengu wa Kiislamu una wajibu maalumu wa kukomesha mauaji ya kimbari huko Gaza
Aug 06, 2025 00:26Katika barua aliyowaandikia mabalozi wa nchi za Kiislamu wanaoishi Denmark, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini humo ametahadharisha kuhusu athari mbaya za jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza na kusisitiza kuwa, Ulimwengu wa Kiislamu unabeba dhima maalumu katika kusimamisha mauaji ya kimbari na kuwatetea wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
-
Baqaei: Iran haiwezi kuiamini Marekani baada ya kushambulia vituo vyake vya nyuklia
Aug 05, 2025 11:16Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa nchi hii haiiamini Marekani khasa baada ya mashambulizi yake yasiyo na msingi katika vituo vya nyuklia vya Iran vinavyoendesha shughuli zake kwa malengo ya amani.
-
Iran: Nchi jirani zizuie ardhi zao zisitumiwe vibaya na utawala wa kizayuni wa Israel
Aug 04, 2025 23:35Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza matumaini aliyonayo ya kukamilika mkataba wa amani kati ya Jamhuri ya Azerbaijan na Armenia lakini amezitaka pia nchi majirani wa Iran zizuie ardhi zao zisitumiwe vibaya na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Kwa nini safari ya Rais Pezeshkian nchini Pakistan ni mabadiliko katika diplomasia ya kikanda?
Aug 04, 2025 09:50Sambamba na matukio ya kijiopolitiki ya kikanda, ziara ya Rais Masoud Pezeshkian wa Iran nchini Pakistan si tu ya kidiplomasia, bali pia ni hatua ya kimkakati ya kufafanua upya nafasi ya Iran katika milingano na mahesabu ya kieneo.
-
Araqchi: Waandishi wa habari walisimama kidete wakati wa vita vya siku 12
Aug 04, 2025 07:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepongeza kuwadia Siku ya "Waandishi wa habari" na amewakumbuka na kuwaenzi waandishi wa habari waliouliwa shahidi khususan katika vita vya kulazimishwa vya hivi karibuni.
-
Pezeshkian: Ukurasa mpya umefunguliwa katika uhusiano wa kidiplomasia kati ya Iran na Pakistan
Aug 04, 2025 04:10Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria ziara yake nchini Pakistan na mazungumzo aliyofanya na viongozi wa nchi hiyo na kusisitiza kuwa: Ukurasa mpya umefunguliwa katika uhusiano wa kidiplomasia kati ya Iran na Pakistan.
-
Iran yaalani hatua mpya za Wazayuni wenye misimamo ya mikali za kuuvunjia heshima Msikiti wa al Aqsa
Aug 04, 2025 04:09Esmaeil Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali kitendo cha Wazayuni wenye misimamo mikali cha kuuvunjia heshima kwa mara nyingine tena Msikiti wa Al-Aqsa wakiongozwa na waziri mtenda jinai wa utawala huo ghasibu Itamar Ben-Gvir ambaye ni Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel.
-
Iran yasisitiza kuwekewa vikwazo vya silaha na kuadhibiwa utawala mtenda jinai
Aug 03, 2025 23:28Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza kuwa, jamii ya kimataifa inapaswa kuacha kutoa kauli tupu na badala yake kuchukua hatua za kivitendo ili kuwapa nafuu watu wa Gaza na kukomesha mauaji ya kimbari.