-
Iran yaangusha ndege ya tatu ya kivita aina ya F-35, marubani wawili Waisraeli wakamatwa
Jun 14, 2025 09:44Jeshi la Iran (Artesh) limeripoti kuangusha ndege ya tatu ya kivita aina ya F-35 inayomilikiwa na utawala wa Kizayuni wa Israel, kwa kutumia mifumo ya ulinzi wa anga iliyotengenezwa ndani ya Iran.
-
Operesheni ya Iran dhidi ya Israel itaendelea kadiri itakavyolazimu
Jun 14, 2025 04:13Operesheni ya kulipiza kisasi ya Ahadi ya Kweli III inayotekelezwa na Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel itaendelea kadiri inavyohitajika. Haya yamesemwa na Mshauri Mkuu wa Kijeshi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Iran yapiga shabaha 150 za Israel katika Operesheni ya Ahadi ya Kweli 3
Jun 14, 2025 03:43Afisa wa ngazi ya juu wa Jeshi la Iran amesema kwa akali shabaha 150 zimepigwa wakati wa operesheni ya kulipiza kisasi ya Jamhuri ya Kiislamu dhidi ya utawala haramu wa Israel, ikiwa ni pamoja na kambi kadhaa za kimkakati za kijeshi za utawala huo pandikizi.
-
Iran yatungua ndege 2 za kivita za Israel za F-35, yamkamata rubani
Jun 14, 2025 03:35Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kimefanikiwa kutungua na kuteketeza ndege mbili za kivita za Israel aina ya F-35, na idadi kubwa ya ndege zisizo na rubani. Iran imekuwa nchi ya kwanza duniani kuweza kutungua ndege ya kijeshi ya F-35.
-
Jenerali Hatami ateuliwa kuwa Kamanda mpya wa Majeshi ya Iran
Jun 14, 2025 03:34Brigedia Jenerali Amir Hatami ameteuliwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, kuwa Kamanda Mkuu mpya wa Majeshi ya Iran.
-
Tehran: Mazungumzo ya nyuklia na US 'hayana maana' baada ya uvamizi wa Israel
Jun 14, 2025 03:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, mazungumzo na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran "hayana maana" kufuatia mashambulizi ya kinyama ya Israel, huku akiishutumu Washington kwa kuunga mkono uchokozi huo.
-
Operesheni ya Ahadi ya Kweli 3; Israel yakumbwa na wimbi la makombora ya Iran
Jun 13, 2025 23:21Vikosi vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimeanza kufanya wimbi la mashambulizi ya makombora dhidi ya Israel, ili kulipiza kisasi kufuatia hujuma za utawala huo wa Kizayuni dhidi ya ardhi ya Iran.
-
Araqchi: Tunachotegemea kwa Ulaya ni kulaani mashambulizi ya Israel
Jun 13, 2025 22:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa: Serikali na wananchi wa Iran wanataraji kuiona jamii ya kimataifa hususan Umoja wa Ulaya unalaani shambulio hilo la kijinai la Israel dhidi ya nchi yao.
-
Rais Pezeshkian: Jibu halali na kali la Iran litamfanya adui kujuta
Jun 13, 2025 10:38Katika ujumbe wake kwa taifa kufuatia jinai ya kinyama iliyofanywa na utawala wa Kizayuni usiku wa kumkia leo, Rais Masoud Pezeshkian amesisitiza juu ya ulazima wa watu kujiepusha na uvumi katika vita vya kisaikolojia vya adui na kuwaunga mkono na kuwaamini viongozi na kusema: Taifa la Iran na maafisa wa nchi hawatonyamaza mbele ya jinai hiyo.
-
Iran yataka kikao cha Baraza la Usalama, UN yakubali
Jun 13, 2025 10:01Katika barua ya dharura kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Mwakilishi wa Kudumu wa Iran kwenye Umoja wa Mataifa huko New York Marekani ametoa mwito wa kufanyika kikao cha dharura cha kulaani mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya vituo vya nyuklia na mauaji ya maafisa wa kijeshi wa Iran. Kwa upande wake, Umoja wa Mataifa umekubali kuitisha kikao hicho cha dharura.