-
Safavi: Marubani zaidi ya 16 wa Israel waliuawa katika vita vya siku 12
Sep 28, 2025 07:32Mshauri mkuu wa masuala ya kijeshi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuwa, zaidi ya marubani 16 wa Israel waliangamizwa katika vita vya siku 12 vilivyotwishwa Iran na utawala wa Kizayuni.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Israel ni utawala unaodharaulika na uliotengwa pakubwa duniani
Sep 28, 2025 03:52Ayatullah Sayyid Ali Khamenei Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ameitaja Israel kama utawala unaochukiwa zaidi duniani.
-
UN yaiwekea tena Iran vikwazo vilivyokuwa vimeondolewa kwa mujibu wa makubaliano ya nyuklia
Sep 28, 2025 03:51Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeiwekea tena Iran vikwazo vilivyokuwa vimendolewa huko nyuma kwa mujibu wa makubaliano ya nyuklia ya 2015 katika hatua iliyochochewa na mataifa ya Ulaya bila sababu ya msingi ili kutia dosari miradi ya nyuklia ya Iran, huku baraza hilo likipuuza hatua ya nchi za Magharibi ya kuhujumu makubaliano hayo.
-
Rais wa Iran akataa matakwa ya nyuklia ya Marekani na kuyataja kuwa 'hayakubaliki'
Sep 27, 2025 23:15Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, taifa hili linafadhilisha kurejeshwa kwa vikwazo kuliko kutii matakwa "yasiyokubalika" ya Marekani ya kukabidhi akiba yake yote ya urani iliyorutubishwa.
-
SEPAH: Tutaendelea kuunga mkono Muqawama hadi ukombozi wa Quds Tukufu
Sep 27, 2025 06:55Katika taarifa yake kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuuawa shahidi Jenerali Nilforoshan na Sayyed Hassan Nasrallah, Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi SEPAH limesisitiza kuwa litaendelea kuwa pamoja na imara na kambi ya Muqawama hadi Palestina na Quds Tukufu zitakapokombolewa.
-
Shehena muhimu zaidi ya satelaiti ya Iran ya Nahid-2 yafanyiwa majaribio
Sep 27, 2025 06:54Shehena kuu wa setilaiti ya Nahid-2 ya Iran, ambayo ilizinduliwa mwezi Agosti, kwa sasa inafanyiwa majaribio katika obiti. Shehena hiyo ina jukumu muhimu katika kuanzisha mawasiliano ya satelaiti.
-
Larijani: Utawala wa Kizayuni hauna huruma na nchi yoyote
Sep 27, 2025 06:53Katibu wa Baraza Kuu la Usalama la Taifa la Iran ambaye amewasili Beirut kuhudhuria kikao cha Baraza la Kumbukumbu za Mashahidi wa Muqawama wa Hizbullah amesema kwamba, utawala wa Kizayuni hauna huruma na nchi yoyote ile.
-
Rais wa Iran: Sera za Trump zitateketeza eneo zima na Iran itatoa jibu kali kwa wavamizi
Sep 27, 2025 03:14Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema sera za rais wa Marekani ziko kwenye mkondo wa kuibua mabadiliko makubwa na vurugu katika eneo lote la Asia ya Magharibi, akionya kuwa Iran itakabiliana na wavamizi wowote kwa nguvu ya juu kabisa iwapo kutatokea uvamizi mpya wa kijeshi.
-
Iran na Russia zasaini mkataba wa dola bilioni 25 kuhusu ujenzi wa mitambo ya nyuklia
Sep 27, 2025 03:11Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Russia zimesaini mkataba wa dola bilioni 25 kwa ajili ya kujenga mitambo minne ya nishati ya nyuklia, kama sehemu ya makubaliano ya muda mrefu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tehran na Moscow katika nyanja mbalimbali.
-
Iran: Kura ya 'snapback' ni batili, haina mashiko ya kisheria
Sep 26, 2025 23:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesisitiza kuwa, juhudi za mataifa matatu ya Ulaya ya Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani za kuhuisha vikwazo vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu kwa kutumia utaratibu unaojulikana kama snapback' ni "batili na hazina mashiko yoyote ya kisheria."