-
Qalibaf amwambia Spika wa Knesset: Nyinyi ni aibu kwa ubinadamu
Aug 01, 2025 10:08Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameandika katika ujumbe wake kwa Spika wa Knesset (Bunge la Israel) kwamba: "Ulimwengu unashuhudia mauaji makubwa zaidi ya kimbari yanayofanywa na Israel. Nyinyi ni aibu kwa ubinadamu."
-
Iran yakadhibisha madai hewa ya US na nchi zingine chache za Magharibi dhidi yake
Aug 01, 2025 04:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani hatua ya Marekani, Ufaransa na nchi nyingine kadhaa za Magharibi ya kukariri tuhuma zisizo na msingi na za kuchekesha dhidi ya Iran na kuzielezea kuwa ni jaribio la waziwazi la kutaka kubebesha lawama wasiohusika na hila ya kuzibabaisha fikra za umma duniani ziachane na suala muhimu zaidi la wakati huu, yaani mauaji ya kimbari katika Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Spika wa Iran: Walimwengu wote wajifunze kutokana na hadaa na utovu wa uaminifu wa Marekani
Jul 31, 2025 23:47Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema, walimwengu wote inawapasa wajifunze kutokana na hadaa ya Wamarekani na akasisitiza kuwa, viongozi na wasomi wenye vipawa wa nchi za Kiislamu wasighafilike na hadaa na utovu wa uaminifu wa Marekani.
-
Maspika wa Mabunge ya Iran na Tanzania wataka kuimarisha ushirikiano wa Kibunge
Jul 31, 2025 09:43Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge ya Dunia (IPU).
-
Rais Pezeshkian: Hakuna nchi inayoweza kuipigisha magoti Iran yenye umoja
Jul 31, 2025 09:06Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa hakuna nchi inayoweza kuwapigisha magoti wananchi wa Iran na hakuna kizuizi chochote kinachoweza kukwamisha ustawi wao madhali wanadumisha umoja na mshikamano wao.
-
Araqchi: Marekani imependekeza kuanza tena mazungumzo na Iran
Jul 31, 2025 09:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi ametaka kufidiwa hasara za vita vya mwezi uliopita na kusisitiza kuwa Marekani inapasa kufidia hasara zilizosababishwa kwa Iran katika vita vya karibuni vya siku 12.
-
Russia yalaani tishio jipya la Trump dhidi ya taasisi za nyuklia za Iran
Jul 31, 2025 04:05Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, Maria Zakharova amelaani matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani na kusema: "Vitisho vya mara kwa mara dhidi ya Iran vya kufanya mashambulizi mapya ya makombora na kushambulia vituo vya nyuklia vya nchi hiyo vimeibua wasiwasi mkubwa."
-
Pezeshkian apongeza msimamo wa kishujaa wa Venezuela wakati wa vita vya Israel dhidi ya Iran
Jul 31, 2025 00:46Rais Masoud Pezeshkian amesifu msimamo wa wazi na wa kishujaa wa Venezuela katika kulaani uchokozi wa hivi karibuni wa Israel dhidi ya Iran, pamoja na kuonyesha mshikamano na taifa la Iran.
-
Bunge la Iran latoa wito wa kuvunjwa mzingiro wa chakula Gaza na kuzuia maafa ya binadamu
Jul 30, 2025 09:18Katika taarifa yao iliyotolewa mapema leo Jumatano, wajumbe wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran wametaka kuvunjwa mzingiro wa chakula huko Gaza na kukomeshwa maafa makubwa ya binadamu katika eneo hilo.
-
Malengo halisi ya Magharibi kuhusu Iran ni yapi?
Jul 30, 2025 08:29Vyombo vya habari vya kigeni, sambamba na kuripoti kauli ya hivi karibuni ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, vimezingatia kwa namna ya kipekee sehemu ya hotuba yake ambapo amesisitiza kuwa: “Mpango wa nyuklia, urutubishaji na haki za binadamu ni visingizio – wanachotaka wao ni dini na elimu yenu.”