-
Pezeshkian: Iran iko ‘tayari kabisa’ kwa hali yoyote iwapo mpango wa snapback utatekelezwa
Sep 26, 2025 07:28Rais Masoud Pezeshkian amesema kuwa Iran iko tayari kikamilifu kwa hali yoyote endapo nchi za Ulaya zitaendelea na hatua ya kurejesha vikwazo vya Umoja wa Mataifa kupitia kile kinachoitwa utaratibu wa snapback, na ameonya kwamba mazungumzo ya kidiplomasia yatakuwa hayana maana chini ya vikwazo vilivyorejeshwa.
-
Iran yaandaa moja ya maonyesho makubwa ya teknolojia za elektroniki, kompyuta na biashara ya mtandaoni
Sep 26, 2025 07:23Jiji la Tehran wiki hii ni mwenyeji wa ELECOMP 2025, maonyesho makubwa na yenye ushawishi mkubwa zaidi nchini Iran yanayohusu teknolojia za elektroniki, kompyuta, na biashara kwa njia ya mtandao (e-commerce).
-
Marekani na washirika wake zaendelea kuiga kutengeneza droni maarufu ya Iran
Sep 26, 2025 03:00Nchi kadhaa duniani zikiongozwa na Marekani zinapigana vikumbo katika kuiga na kutengeneza nakala za ndege isiyo na rubani ya Shahed ya Iran, ambayo si ghali lakini yenye ufanisi na usahihi wa hali ya juu.
-
Rais Pezeshkian: Mazungumzo hayana maana ikiwa vikwazo vitarejeshwa
Sep 25, 2025 23:01Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa mazungumzo ya kidiplomasia hayatakuwa na maana iwapo kundi la nchi tatu za Ulaya E3 linaloundwa na Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zitarejesha tena vikwazo dhidi ya Tehran.
-
Baghaei: Madai ya Marekani ya kuheshimu diplomasia ni chapwa na udanganyifu
Sep 25, 2025 08:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema katika kujibu madai ya Marekani ya kwamba eti iko tayari kufanya mazungumzo na Iran na kuheshimu diplomasia na kusema: Huwezi kupiga nchi kwa mabomu na baadaye kudai eti unaheshimu mazungumzo ya kidiplomasia.
-
Kwa nini mazungumzo na Marekani hayana maana?
Sep 25, 2025 07:12Viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wametoa sababu mbalimbali kwa nini mazungumzo na Marekani hayana natija.
-
Iran yaonyesha taswira za ndani ya kinu cha nyuklia cha Israel, taarifa nyeti za wanasayansi na wataalamu 189 wa kijeshi
Sep 25, 2025 03:33Kwa mara ya kwanza, Wizara ya Usalama ya Iran imeonyesha hadharani picha na taswira nyeti za ndani ya kinu cha nyuklia cha Dimona cha utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Akihutubia UNGA, Rais wa Iran akemea mashambulizi ya Marekani na Israel
Sep 25, 2025 00:57Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani mashambulizi ya anga ya “kikatili” yaliyofanywa na Marekani na Israel mwezi Juni katika ardhi ya Iran.
-
Kamanda wa Iran: Israel haina ubavu wa kuanzisha vita bila ya msaada wa Marekani na NATO
Sep 25, 2025 00:10Kamanda mwandamizi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, utawala wa kizayuni wa Israel hauna uwezo wa kupigana bila ya kusaidiwa na shirika la kijeshi la NATO na Marekani, jambo linalodhihirisha kuwa makabiliano yanayoweza kutokea ni ya mpambano dhidi ya "ubeberu wa kimataifa."
-
Iran yakataa masharti ya kupunguza uwezo wa makombora yake
Sep 24, 2025 08:34Mkuu wa Usalama wa Taifa wa Iran amesema kuwa nchi hii itatetea kwa ari kubwa usalama wake wa kitaifa na haitakubali “masharti ya kudhalilisha” kama vile kuwekewa mipaka ya uwezo wa makombora yake, akijibu kwa ukali madai ya kupindukia kutoka mataifa ya Magharibi.