-
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Kufuatia Mashambulizi ya Leo ya Utawala wa Kizayuni
Jun 13, 2025 01:04Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa rasmi kulaani vikali uvamizi wa kijeshi uliofanywa na utawala dhalimu wa Kizayuni dhidi ya ardhi ya Iran.
-
Taarifa Namba 1 kutoka Makao Makuu ya Majeshi ya Iran
Jun 13, 2025 00:45Kitengo cha Mawasiliano cha Makao Makuu ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kimetoa taarifa rasmi kikilaani vikali uvamizi wa wazi uliofanywa na adui muovu wa Kizayuni.
-
Kiongozi Muadhamu: Utawala wa Kizayuni umejiandalia hatima chungu na yenye maumivu
Jun 13, 2025 00:11Katika taarifa ya kulaani shambulio lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ardhi tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mapema leo alfajiri, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ametoa ujumbe mzito kwa taifa la Iran, akisisitiza kuwa adhabu kali inamsubiri mhalifu huyo wa kimataifa.
-
Makamanda wa ngazi za juu wa Iran wauawa shahidi katika hujuma ya Israel
Jun 12, 2025 23:37Meja Jenerali Hossein Salami, kamanda mkuu wa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), pamoja na Meja Jenerali Mohammad Bagheri, Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Iran wameuawa shahidi katika hujuma ya anga lililotekelezwa na utawala katili wa Israel mapema Ijumaa alfajiri mjini Tehran.
-
Milipuko mikubwa yasikika Tehran na maeneo mengine ya Iran
Jun 12, 2025 23:01Milipuko mikubwa ilisikika mapema asubuhi ya Ijumaa katika maeneo kadhaa ya mji mkuu wa Iran, Tehran, na pia katika mikoa mingine nchini.
-
Iran kuzindua taasisi mpya za kurutubisha urani. Ni jibu kwa hatua ya IAEA
Jun 12, 2025 07:10Wizara ya Mambo ya Nje na Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran zimetoa taarifa ya pamoja kujibu hatua ya kisiasa ya nchi za Magharibi katika Bodi ya Magavana ya IAEA dhidi ya mradi wa amani wa nyuklia wa Iran na kusema kuwa itazindua taasisi mpya za kurutubisha urani.
-
Rais wa Iran: Mazungumzo na mataifa ya magharibi sio ishara ya kusalimu amri
Jun 12, 2025 04:30Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesisitiza kuwa mazungumzo yanayoendelea kati ya Tehran na mataifa ya Magharibi hayaashirii kusalimu amri kwa mashinikizo ya nje.
-
Iran: Nchi za Ulaya hazina haki ya kisheria wala kimaadili kuiwekea Iran vikwazo
Jun 12, 2025 04:08Iran imesema kuwa mataifa ya Ulaya yaliyosaini mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015, yaani Uingereza, Ufaransa na Ujerumani (E3), hayana nafasi yoyote ya kisheria wala kimaadili ya kufufua vikwazo dhidi ya Iran, kwa kuzingatia kushindwa kwao kutekeleza majukumu yao chini ya makubaliano hayo.
-
Iran: EU ikishinikiza turejeshewa vikwazo vya UN, tutajitoa NPT
Jun 11, 2025 23:23Iran imeonya kwamba, huenda ikatumia haki yake ya kisheria ya kujiondoa kwenye Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji na Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT) ikiwa mataifa ya Ulaya yataendelea na jaribio lisilo na msingi wa kisheria la kuamilisha mchakato wa kurejeshwa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Je, mashirikiano ya Iran na Afrika yataimarika vipi?
Jun 11, 2025 22:39Katika kikao chao na Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, mabalozi wa Senegal na Sierra Leone wamesisitiza utayari wa nchi za Kiafrika kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara na Iran.