-
Iran yaapa kujibu kwa "njia muafaka" maamuzi haribifu ya Bodi ya IAEA
Jun 11, 2025 09:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa vikali hatua ya kichokozi ya Marekani na washirika wake wa Ulaya ya kuwasilisha azimio dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), akionya kuwa uamuzi wowote wa "kutozingatia busara" kutoka kwa wajumbe wa bodi hiyo ya wanachama 35 utajibiwa kwa hatua muafaka kutoka Tehran.
-
Kiongozi Muadhamu: Bunge la Iran ni tofauti na Mabunge yanayounga mkono wahalifu kama wauaji wa Gaza
Jun 11, 2025 09:26Kiongozi wa Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei amesisitiza kuwa, hadhi ya Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu (Bunge la Iran) ni ya kipekee miongoni mwa nchi za dunia na inatofautiana na Mabunge yanayounga mkono dhulma, ubaguzi, tofauti za kitabaka na wahalifu kama wauaji wa Gaza.
-
Iran: Operesheni yetu ya kiintelijensia imeyumbisha vikali usalama wa Israel
Jun 11, 2025 09:12Wizara ya Usalama wa Taifa (Intelijensia) ya Iran imetoa taarifa kuhusu mafanikio yake makubwa ya kukusanya na kuhamisha nyaraka nyingi za siri kutoka Israel, na kuieleza operesheni hiyo kama ushindi wa kipekee na wa kihistoria wa kijasusi ambao haujawahi kushuhudiwa.
-
Ni yapi mafanikio ya operesheni ngumu ya kiintelijensia ya Iran dhidi ya utawala wa Kizayuni?
Jun 11, 2025 02:31Taarifa muhimu ya Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetolewa kufuatia operesheni ngumu na nyeti ya kiintelijensia katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel). Taarifa hiyo imesisitiza kuwa: “Tukishambuliwa, vituo vya siri vya nyuklia vya utawala wa Kizayuni vitalengwa."
-
Iran yakosoa kauli ya mkuu wa IAEA, yasema ni sehemu ya vita vya kisaikolojia vya Israel
Jun 10, 2025 23:33Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran, Mohammad Eslami, amezishambulia vikali kauli za Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), akisema kuwa hazina msingi wa kitaalamu wala kisheria.
-
Kwa mara ya kwanza, Iran yapata Tuzo ya huduma bora za Hija Saudi Arabia
Jun 10, 2025 23:32Shirika la Hija la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetunukiwa Tuzo ya Labaytum kwa ubora katika Huduma kwa Mahujaji.
-
Nyaraka ilizopata Iran: Kuna ushirikiano wa siri baina ya Israel na wakala wa IAEA
Jun 10, 2025 08:35Nyaraka za siri ambazo Iran imefanikiwa kuzipata kutoka Israel zinaonyesha kuweko ushirikiano wa siri baina ya utawala haramu wa Israel na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Duru ya sita ya mazungumzo ya Iran na Marekani kufanyika Jumapili ijayo
Jun 10, 2025 08:34Duru ya sita ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya Iran na Marekani yanatajiwa kufanyika Jumapili ijayo huko Muscat Oman.
-
SEPAH: Sasa makombora ya Iran yatapiga shabaha za Israel kwa usahihi zaidi
Jun 10, 2025 04:11Meja Jenerali Hossein Salami, Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema kuwa sasa Jamhuri ya Kiislamu itaweza kupiga maeneo nyeti mmno ya Israel kwa usahihi zaidi baada ya vikosi vya kiintelijensia vya Iran kufanikiwa kukomba hazina kubwa ya taarifa za siri mno za utawala wa Kizayuni na kuzihamishia nchini Iran.
-
Iran: Tutapiga vituo vya siri vya nyuklia vya Israel iwapo tutashambuliwa
Jun 09, 2025 23:33Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) limeonya kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itavishambulia vituo vya siri vya nyuklia vya Israel iwapo utawala huo wa Kizayuni utafanya kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya taifa hili.