-
Iran na Russia kusaini mikataba ya kujenga mitambo mipya ya nyuklia
Sep 22, 2025 09:32Mkuu wa Shirika la Nishati ya Nyuklia la Iran, Mohammad Eslami, ametangaza kuwa Iran na Russia zitasaini mikataba ya ujenzi wa mitambo mipya ya nyuklia nchini Iran wakati wa ziara yake rasmi nchini Russia.
-
Rais wa Iran atoa wito kwa China kutekeleza kwa vitendo mpango wa utawala wa kimataifa
Sep 22, 2025 03:59Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa Iran inatarajia China kuchukua hatua madhubuti kutekeleza mpango ilioupendekesza kuhusu utawala wa kimataifa, ili kuimarisha ushirikiano wa pande nyingi na kukabiliana na siasa za upande mmoja.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu awapongeza wanamieleka wa Iran kwa kutwaa ubingwa wa dunia
Sep 22, 2025 03:53Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ameipongeza kwa dhati timu ya mieleka ya mtindo wa Greco-Roman ya Iran kwa kutwaa taji la ubingwa wa dunia katika Mashindano ya Dunia ya Mieleka ya mwaka 2025 yaliyofanyika nchini Kroatia.
-
Iran na Pakistan zaja na mkakati wa pamoja wa ustawi wa kiuchumi
Sep 21, 2025 23:14Kamisheni ya 22 ya Pamoja ya Uchumi (JEC) kati ya Iran na Pakistan, iliyofanya kikao chake hapa mjini Tehran imetilia mkazo suala la kurejeshwa mkakati wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili jirani.
-
IRGC: Iran itatoa majibu madhubuti kwa chokochoko mpya za maadui
Sep 21, 2025 07:36Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limewaonya maadui wa Iran hususan Israel na Marekani kwamba, watakabiliwa na majibu makali na madhubuti ya Jamhuri ya Kiislamu iwapo watafanya makosa yoyote mapya au kufanya kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya nchi hii.
-
Kurudi kwenye meza ya mazungumzo; masharti ya Iran na wajibu wa pande za Magharibi na IAEA
Sep 21, 2025 03:42Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetoa notisi likisisitiza kuwa ushirikiano na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA utasitishwa hivi karibuni.
-
Pezeshkian: Iran kamwe haitasalimu amri mbele ya mashinikizo
Sep 21, 2025 03:22Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuhusu msimamo thabiti wa Iran, na kusema Jamhuri ya Kiislamu itashinda vikwazo vinavyochochewa na wale wote wenye nia mbaya na kamwe haitasalimu amri mbele ya uonevu na matakwa yao ya mabavu.
-
SNSC: Iran kusitisha ushirikiano na IAEA baada ya kuwekewa tena vikwazo
Sep 21, 2025 03:22Baraza Kuu la Usalama la Taifa la Iran (SNSC) limesema Tehran itasitisha ushirikiano wake na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupiga kura ya kutoiondolea kabisa Tehran vikwazo dhidi yake.
-
Iran yaonya kuwa itasitisha mkataba wa IAEA iwapo vikwazo vya UN vitarejeshwa
Sep 20, 2025 23:55Mwanadiplomasia mwandamizi wa Iran amesema kuwa makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA yaliyofikiwa mjini Cairo yatasitishwa ikiwa vikwazo vya Umoja wa Mataifa vitarejeshwa au utaratibu unaoitwa snapback.
-
Moscow: Kurejeshwa vikwazo dhidi ya Iran sio halali kisheria
Sep 20, 2025 07:55Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa alisema Ijumaa jioni kwamba, kurejeshwa kwa vikwazo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hakuna uhalali wowote wa kisheria na kwamba waliotia saini makubaliano ya nyuklia hawapaswi kuchukua hatua kama hiyo.