-
Spika Qalibaf: Iran haitakubali makubaliano yoyote bila kuondolewa vikwazo
Jun 08, 2025 09:03Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa Iran iko tayari kujenga imani mkabala wa kuondolewa vikwazo huku ikidumisha urutubishaji wa madini ya urani, akieleza kuwa Iran haitakubali makubaliano yoyote pasi na kuondolewa vikwazo ilivyowekewa.
-
Pezeshkian: Iran kamwe haitokubali kuwa chini ya ubeberu
Jun 08, 2025 02:49Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran daima inakaribisha mazungumzo na maneno ya kimantiki, lakini kamwe haiko tayari kuwa chini ya ubeberu wa mtu yeyote yule.
-
Iran iko tayari kusaidia Kenya kujenga nyumba milioni moja
Jun 08, 2025 01:56Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa tayari kuisaidia Kenya kujenga nyumba milioni moja za bei nafuu nchini humo.
-
Araqchi aionya Troika ya Ulaya dhidi ya kuchua hatua yoyote ya uadui dhidi ya Iran katika Kikao cha Bodi ya Magavana ya IAEA
Jun 08, 2025 01:07Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa onyo la wazi kwa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza kufuatia hatua za hivi karibuni za nchi tatu hizo za Ulaya katika Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA.
-
Iran: Ripoti ya IAEA imethibitisha miradi ya nyuklia ya Tehran ni ya amani
Jun 08, 2025 00:18Iran imesema kuwa, ripoti ya hivi majuzi ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ambayo imeeleza kutokuwepo kwa ushahidi wowote wa kuaminika kwamba, miradi ya nyuklia ya Iran imeelekea katika mkondo wa kijeshi inathibitisha miradi ya nyuklia ya taifa hili inafanyika kwa malengo ya amani.
-
Kamati ya Bunge la Iran: Kurutubisha madini ya urani sio "suala la kujadiliwa"
Jun 08, 2025 00:18Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema: Urutubnishaji madini ya urani ni haki ya taifa hili na Tehran haiko tayari kuwekwa hilo katika ajenda ya mazungumzo.
-
Iran yatoa pigo kubwa la kihistoria kwa Israel
Jun 07, 2025 14:08Shirika la habari la IRIB limenukuu duru za kuaminikia katika eneo hili la Asia Magharibi zikisema kuwa, taasisi ya kiintelijensia ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa pigo kubwa kwa Israel. Imefanikiwa kuhamisha kutoka kwa utawala wa Kizayuni taarifa za siri za kijasusi, nyeti na za kiistratijia ikiwemo miradi na taasisi za atomiki za Israel.
-
Aragchi: Iran haitaki kumiliki silaha za nyuklia
Jun 07, 2025 09:35Seyed Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, amesisitiza kwa mara nyingine kuwa Iran haina nia yoyote ya kumiliki silaha za nyuklia, akieleza kwamba msimamo wa Iran umejengwa juu ya misingi ya kidini pamoja na fatwa ya wazi iliyotolewa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei.
-
Iran yalaani hatua ya kibaguzi ya Marekani ya kuwapiga marufuku Waislamu kuingia nchini humo
Jun 07, 2025 09:23Tehran imelaani vikali amri ya Rais wa Marekani, Donald Trump, ya kuwapiga marufuku wananchi wa Iran na raia kutoka mataifa mengine yenye Waislamu wengi kuingia Marekani, ikisema hatua hiyo inaonesha uadui wa kina wa Washington dhidi ya Wairani.
-
Iran, Imarati zasisitiza haja ya Waislamu kote duniani kuwa na umoja
Jun 07, 2025 03:30Rais Masoud Pezeshkian wa Iran na Kiongozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan wametoa wito wa umoja wa Waislamu.