-
Helikopta ya Jeshi la Wanamaji la Iran yaitimua manowari ya US katika Bahari ya Oman
Jul 24, 2025 03:25Helikopta ya Jeshi la Wanamaji la Iran imeitimua manowari ya mashambulizi ya Marekani iitwayo USS Fitzgerald katika Bahari ya Oman, kwa kutoa ishara za onyo na hatimaye kuilazimisha ibadili mkondo wake kuelekea upande wa kusini wa eneo hilo.
-
Kwa nini Iran inachukulia juhudi za kuhuisha mfumo wa Snapback kuwa kinyume cha sheria?
Jul 23, 2025 23:09Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Anayeshughulikia Sheria na Masuala ya Kimataifa analichukulia jaribio lolote la Troika ya Ulaya la kuamilisha utaratibu wa Snapback kuwa ni jambo lisilokubalika kisheria.
-
Iran yaalani ukatili mkubwa wa sera ya njaa na mauaji ya Israel dhidi ya wakazi wa Gaza
Jul 23, 2025 07:37Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani " ukatili mkubwa" unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, na kulaani sera ya njaa na mauaji ya utawala huo dhidi ya Wapalestina wanaotafuta misaada huko Gaza.
-
Rais: Ni 'njozi' kuutokomeza mpango wa nyuklia wa Iran; ikihitajika tutaipiga tena vikali Israel
Jul 23, 2025 03:51Rais Masoud Pezeshkian amepuuzilia mbali juhudi na uchochezi wa Marekani na washirika wake, hususan utawala wa kizayuni wa Israel, wa kushinikiza kutokomezwa mpango wa nishati ya nyuklia wa Iran.
-
Araghchi: Tutajiimarisha zaidi na zaidi kutokana na masomo ya Vita vya Siku 12
Jul 23, 2025 02:43Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa, "kwa mafunzo tuliyopata katika vita vya siku 12 na kwa kuondoa nukta za udhaifu tulizonazo, tutakuwa Jamhuri ya Kiislamu yenye nguvu zaidi na zaidi".
-
Rais Pezeshkian: Ziitwazo ‘haki za binadamu’ na ‘asasi za kimataifa’ si chochote ila ni uwongo tu
Jul 22, 2025 10:25Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, zinazoitwa haki za binadamu na asasi za kimataifa si chochote zaidi ya uwongo tu na akabainisha kwamba, katika dunia ya leo iliyostaarabika na mbele ya macho ya watu wote, wanawakatia maji na chakula watu wanyonge, wanawake na watoto na kufanya mauaji ya kimbari; kisha wanazungumzia haki za binadamu, huku wao wenyewe wakiwa wamekiuka vipimo vyote vya kimataifa na haki za binadamu na kufanya jinai dhidi ya ubinadamu kila mahali dunian
-
Iran, Uturuki: Ulimwengu wa Kiislamu uchukue hatua dhidi ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel Ghaza
Jul 22, 2025 07:36Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Uturuki wametoa wito kwa mataifa ya Kiislamu duniani kuchukua hatua kali za kusaidia kukomesha vita vya miezi 21 vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.
-
Iran yatilia shaka 'hadhi' ya Tuzo ya Nobel baada ya Trump 'kuteuliwa'
Jul 22, 2025 03:13Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baqaei ametilia shaka itibari na uhalisi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, akisema tuzo hiyo yenye heshima kubwa zaidi ya amani duniani, imegeuzwa na kuwa chombo cha kisiasa badala ya kuwa nembo ya amani kwa wote.
-
Mamluki wengine wawili wa Mossad watiwa nguvuni kaskazini mashariki mwa Iran
Jul 22, 2025 01:01Askari usalama wa Iran wamewatia nguvuni magaidi wawili wa Shirika la Ujasusi la Israel (MOSSAD) katika mkoa wa kaskazini mashariki wa Khorasan ya Kaskazini, unaopatikana kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Iran: Hatutaachana na haki yetu ya kurutubisha urani
Jul 22, 2025 00:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu haina nia ya kuachana na mpango wake wa nyuklia, ikiwemo kurutubisha madini ya urani, licha ya uvamizi wa kijeshi wa mwezi uliopita wa Marekani na mutifaki wake wa kieneo, Israel.