-
Araqchi ayaonya madola ya Ulaya: Iran itajibu kwa nguvu ukiukaji wowote wa haki zake
Jun 06, 2025 23:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi amezionya nchi za Ulaya dhidi ya kuchukua hatua zozote ovu dhidi ya Iran kwenye Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) na kusisitiza kwamba, Tehran itajibu kwa nguvu ukiukaji wowote wa haki zake.
-
Abu Torabi Fard: Imam Khomeini ameugeuza Umma wa Kiislamu kuwa nguvu mpya duniani
Jun 06, 2025 03:19Khatibu wa Sala ya Idul Adh'ha iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema: Imam Khomeini (MA) alifanikiwa kuleta mageuzi makubwa nchini Iran na pia kuugeuza Umma wa Kiislamu kuwa nguvu mpya inayozidi kunawiri kwenye ulimwengu wa leo.
-
Baqaei: Kujaribu kuhalalisha jinai za kutisha za Israel ni janga kubwa zaidi duniani leo
Jun 06, 2025 03:18Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: Kujaribu kuhalalisha jinai za kutisha na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wasio na ulinzi wa Palestina, ni janga kubwa zaidi duniani leo, na kwamba waungaji mkono wa jinai hizo na wahalalishaji wa uhalifu wa kuchupa mipaka wa utawala wa Kizayuni ni washirika wa moja kwa moja wa jinai za Israel.
-
Iran yaishtaki IAEA kwa madai yake yasiyo na msingi
Jun 06, 2025 03:17Iran imetoa hati ya kisheria kupinga madai ya “ujasusi” ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA na kuyataja kuwa ni ya kichochezi na yasiyo na msingi. Tehran inaamini kuwa shirika hilo limevuka mipaka yake na linatoa matamshi dhidi ya Iran kwa kutegemea ushahidi bandia.
-
Pezeshkian: Iran ina nia ya kweli ya kuimarisha ushirikiano na nchi zote za Kiislamu
Jun 05, 2025 23:00Rais Masoud Pezeshkian amefanya mazungumzo ya simu na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia, na sambamba na kumpa mkono wa Idi kwa mnasaba wa sikukuu ya Idul Adh’ha amesisitizia udharura wa kuendelezwa uhusiano wa kidugu kati ya nchi hizi mbili za Kiislamu, kuzidisha ushirikiano wa kieneo na kuimarisha umoja na mshikamano wa mataifa yote ya Waislamu.
-
Imam Khomeini: Urithi wa uongozi wa kidini na kimapinduzi
Jun 05, 2025 06:55Katika mwaka wa 36 wa maadhimisho ya kuaga dunia Imam Ruhollah Khomeini (MA), mwanzilishi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979 nchini Iran, fikra zake zingali zinaendelea kuathiri sio tu mwelekeo wa kisiasa wa Jamhuri ya Kiislamu bali pia mijadala mipana zaidi kuhusu mahusiano kati ya Uislamu na siasa katika ulimwengu wa Kiislamu.
-
Ujumbe wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa Mahujaji wa Beitul Haram mjini Makka
Jun 05, 2025 05:38Katika ujumbe wake kwa Mahujaji wa Beitul Haram katika mji mtakatifu wa Makka, Ayatullah Khamenei Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa: Serikali za Kiislamu zinapaswa kufunga njia zote za kuusaidia utawala wa Kizayuni, na kwamba wananchi nao wanapasa kuziwajibisha serikali zao katika kufikia lengo hilo.
-
Kiongozi Muadhamu katika ujumbe wa Hija: Mataifa ya Kiislamu lazima yakabiliane na jinai za Wazayuni
Jun 05, 2025 03:49Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe muhimu kwa mnasaba wa msimu wa Hija ya mwaka huu; ambapo ameitaja Hija kuwa ibada ya kuhajiri kutoka katika maisha ya kimaada na kwenda katika maisha ya tauhidi na kumpwekesha Allah.
-
Pezeshkian: Umoja wa mataifa ya Kiislamu ni wajibu wa kidini na kistratajia
Jun 05, 2025 03:24Rais Masoud Pezeshkian wa Iran, amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu inatazama umoja na mshikamano miongoni mwa mataifa ya Kiislamu kuwa ni wajibu wa kidini na wa kimkakati.
-
Trump na matakwa ya kupindukia kwa Iran: Je, Washington inataka kufikia makubaliano au kutwisha matakwa?
Jun 05, 2025 00:45Rais Donald Trump wa Marekani amekariri matakwa ya kupindukia mipaka ya Washington kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa Iran kwa ajili ya kufikiwa mapatano ya pande mbili.