-
Pezeshkian: Hatutaacha mpango wetu wa amani wa nyuklia chini ya shinikizo lolote
May 18, 2025 08:40Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Tehran kamwe haitaachana na mpango wake wa amani wa nyuklia.
-
Umuhimu wa Mkutano wa Kimataifa wa Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran
May 18, 2025 07:24Mkutano wa Kimataifa wa Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran unafanyika kwa kuwashirikisha takriban wageni 200 kutoka nchi 53 duniani. Mkutano huo umefunguliwa rasmi mapema leo katika hafla iliyohudhuriwa na Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Waziri wa Mambo ya Nje, Abbas Araqchi.
-
Zaidi ya Wairani 30,000 wamewasili Saudi Arabia kwa ajili ya Hija
May 18, 2025 05:49Zaidi ya Wairani 30,000 wamewasili nchini Saudi Arabia kwa ajili ya ibada ya Hija ya kila mwaka, huku idadi hiyo ikitazamiwa kuongezeka katika siku zijazo.
-
Waziri Mkuu wa Pakistan apongeza jitihada za Iran kupunguza mvutano na India
May 18, 2025 05:47Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, amesifu juhudi za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kusaidia kupunguza mvutano kati ya Islamabad na New Delhi kufuatia shambulizi la kigaidi lililotokea mwezi uliopita katika eneo la Kashmir linalosimamiwa na India. Ametilia mkazo umuhimu wa kutafuta suluhu kupitia majadiliano na mikakati ya kisiasa.
-
Iran yatangaza ongezeko la watumiaji wa intaneti ya kasi ya simu za mkononi
May 18, 2025 05:45Iran imeripoti ongezeko zaidi la idadi ya watumiaji wa intaneti ya kasi ya simu za mkononi (mobile broadband) huku ikifanya juhudi za kuboresha huduma zinazotolewa na mtandao wake wa intaneti wa kasi.
-
Iran yaizamisha China kwenye mashindano ya Asia, yaingia Kombe la Dunia la Futsal kwa Wanawake 2025
May 18, 2025 01:02Timu ya taifa ya wanawake ya futsal ya Iran imemaliza katika nafasi ya tatu kwenye mashindano ya Kombe la Asia kwa Wanawake la Futsal la AFC 2025 nchini China, na hivyo kufuzu kwa mara ya kwanza kushiriki Kombe la Dunia la Wanawake la Futsal la FIFA.
-
Faida za makubaliano ya Iran na Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia
May 17, 2025 08:30Ali Ahmadnia, Mkuu wa Masuala ya Habari wa Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza kuwa takriban asilimia 87 ya bidhaa zinazouzwa kati ya Iran na nchi tano wanachama wa Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia (EAEU) zitauzwa kati ya nchi hizo bila kutozwa ushuru.
-
Kiongozi Muadhamu: Matamshi ya Trump ni fedheha kwa taifa la Marekani
May 17, 2025 07:53Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amekosoa matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani na kuyataja kuwa ni "fedheha" kwa taifa la Marekani.
-
Pezeshkian: Iran inafanya mazungumzo, lakini haigopi vitisho vyovyote
May 17, 2025 07:00Rais Masoud Pezeshkian amesisitiza kuwa, Iran haitasalimu amri na kuachana na haki zake licha ya vitisho, akieleza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitaachana na mafanikio yake ya heshima katika nyanja yoyote ile, iwe kisayansi au kijeshi.
-
Araqchi: Haki ya Iran ya kurutubisha urani kwa malengo ya amani si ya kufumbiwa macho
May 17, 2025 04:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwamba, hakuna sinario na kitu ambacho kitaifanya Iran iachane na haki yake ya kurutubisha madini ya urani kwa malengo ya amani.