-
Iran yalaani taarifa ya kichochezi ya nchi za Ghuba ya Uajemi na Marekani
Jun 27, 2026 02:53Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali taarifa ya pamoja ya Marekani na Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (P-GCC), ikiitaja kuwa ni “ya kuingilia mambo ya wengine, isiyo ya kuwajibika, na ya kichochezi,” huku ikizionya nchi za eneo hilo dhidi ya kuendelea kushirikiana kwa misimamo ya uadui na Washington.
-
Araqchi: Hatutasahau wala hatutasamehe mauaji ya Sayyidi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Jun 26, 2026 11:23Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika ujumbe wake kwamba: "Kuuliwa shahidi Sayyid na kinara wa mashahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu hakutasahaulika wala hakutasamehewa."
-
Iran: Waliohusika na mauaji ya wanafunzi wa shule ya Minab wachukuliwe hatua
Jun 26, 2026 04:21Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani "uhalifu mbaya" uliofanywa na Marekani katika shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh ya Minab nchini Iran wakati wa mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kislamu, na kutoa wito kwa wahusika wote, wapangaji na viongozi kuwajibishwa kikamilifu, akisisitiza kwamba: "Kumbukumbu ya watoto wa Minab inahitaji haki, uwajibikaji na utekelezaji, si kukaa kimya."
-
Rais Pezeshkian: Imam Hussein (a.s.) ametufundisha kusimama dhidi ya dhulma
Jun 25, 2026 10:07Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa, Imam Hussein (a.s.) ametufundisha kusimama dhidi ya dhulma, vishawishi vya madaraka, na tamaa ya maslahi binafsi.
-
Baghaei: NATO inapaswa kuwajibishwa kwa kushiriki katika vita dhidi ya Iran
Jun 25, 2026 09:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwamba, Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) na nchi wanachama wake, zikiwemo Italia na Romania, ambazo Katibu Mkuu wa NATO amekiri waziwazi nafasi yao katika kutekeleza mashambulizi haramu na ya kihalifu dhidi ya Iran, zinapaswa kuwajibishwa kwa aina yoyote ya ushirikiano katika uhalifu uliofanywa na Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Iran yapendekeza kuanzishwa Umoja wa Redio na Televisheni wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai
Jun 25, 2026 04:22Mwakilishi wa Mkuu wa Kitengo cha Matangazo ya Ng'ambo ya Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ametoa pendekezo la kuanzishwa Umoja wa Redio na Televisheni wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai kama utaratibu mpya wa kuimarisha diplomasia ya vyombo vya habari na muungano wa kitamaduni miongoni mwa nchi wanachama.
-
Mamilioni ya Wairani washiriki maombolezo kuelekea siku ya Ashura
Jun 24, 2026 11:04Mamilioni ya Waislamu katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maeneo mengine ya dunia leo mchana wameshiriki katika maombolezo ya kumbukumbu ya Ta'asua na jioni hii wanashiriki katika hafla za mkesha wa Ashura ambayo ni kukumbuka siku ya kuuliwa shahidi mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW), Imam Hussein bin Ali bin Abi Twalib (AS).
-
Qalibaf: Mkataba wa Islamabad ni tangazo la kufeli kwa Marekani
Jun 24, 2026 11:00Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Mkataba wa Maelewano (MoU) wa kumaliza vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa matokeo ya shinikizo au kulazimishwa, bali ni zao la ustahimilivu na nguvu ya taifa shupavu la Iran.
-
Pezeshkian: Iran haitazungumzia uwezo wake wa kjeshi, asema makombora yameiepusha Iran na hatima ya Gaza
Jun 24, 2026 10:59Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa Tehran haitawahi kamwe kufanya mazungumzo yoyote kuhusu uwezo wake wa ulinzi na kuzuia uchokozi (deterrence), akibainisha kuwa ghala la makombora la nchi hii ndilo limeiweka Iran salama dhidi ya kukumbwa na hatima ya Gaza.
-
Watafiti wa Iran wapiga hatua ya kwanza katika chanjo ya mRNA dhidi ya saratani ya matiti
Jun 24, 2026 10:57Watafiti kutoka taasisi tano za kisayansi na kitiba nchini Iran wamefanikiwa kubuni chanjo ya aina yake ya mRNA kwa kutumia njia za hali ya juu za kompyuta.