-
Qalibaf: Majenerali wa Marekani hawataki kufa kwa ajili ya Israel
Apr 05, 2026 05:42Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu yaani Bunge la Iran, amekejeli hatua ya Waziri wa Vita wa Marekani, Pete Hegseth ya kuwatimua makamanda wenye uzoefu katika jeshi la nchi hiyo na kuandika: Hawataki tena kumtii mtangazaji wa televisheni anayehatarisha maisha ya Wamarekani kwa ajili ya njozi za Israel.
-
Iran yaangusha helikopta mbili za Black Hawk na ndege mbili za kijeshi za C‑130 za Marekani
Apr 05, 2026 05:36Msemaji wa Kamandi Kuu ya Khatam al‑Anbiya ya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa vyombo vya anga vya adui vilivyovamia mkoa wa Isfahan, vikijumuisha helikopta mbili aina ya Black Hawk na ndege mbili za usafirishaji wa kijeshi ya C‑130 zimetunguliwa na kuangamizwa na vikosi vya ulinzi.
-
Spika wa Bunge la Iran aonya kuhusu majibu mapana dhidi ya maslahi ya Marekani katika eneo
Apr 05, 2026 03:05Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Ghalibaf, amesisitiza kuwa “usalama endelevu” ndio kipaumbele kikuu cha Iran, akionya kwamba kuendelea kwa mvutano kutasababisha majibu mapana yatakayolenga maslahi ya Marekani katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Namna vita dhidi ya Iran vilivyobadilisha muundo wa soko la nishati duniani?
Apr 05, 2026 01:53Taasisi moja ya Marekani imekiri kwamba vita dhidi ya Iran vimebadilisha pakubwa muundo wa soko la nishati duniani.
-
Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran latoa wito wa kulaaniwa mashambulizi dhidi ya vituo vya amani vya nyuklia vya Iran
Apr 05, 2026 01:48Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran limetoa wito wa kulaaniwa mashambulizi dhidi ya vituo vyake vya amani vya nyuklia, likisema hilo ndilo tarajio la chini kabisa linalotazamiwa kutoka kwa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki.
-
Ndege kadhaa za kivita za Marekani zatunguliwa Iran, hadi sasa droni 160 za adui zimedunguliwa
Apr 04, 2026 07:28Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema vitengo vyake vya ulinzi wa anga vimeangamiza ndege kadhaa za kijeshi za Marekani katika “siku nyeusi” kwa majeshi ya nchi hiyo na utawala ghasibu wa Israel.
-
Iran: Hujuma dhidi ya madaraja ni uhalifu wa kivita
Apr 04, 2026 03:18Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali Marekani na utawala wa Israel kwa kutekeleza “uhalifu wa kivita wa kigaidi wa mtindo wa Daesh” wakati wa vita vyao vya kichokozi vinavyoendelea dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, akisema maadui hao wawili hawatapata nguvu kwa kuharibu madaraja makubwa nchini Iran.
-
Pezeshkian: Tutailinda Iran kwa azma thabiti na uwezo wetu wote
Apr 04, 2026 02:56Rais Mahmoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huku akiashiria kwamba Iran ilishambuliwa kijeshi na Marekani na utawala haramu wa Israel wakati ilipokuwa kwenye mazungumzo na Marekani, amesema: "Sisis tunasisitiza juu ya azma thabiti ya kujilinda."
-
Uchina: Tehran haitasalimu amri mbele ya mashinikizo
Apr 04, 2026 02:52Huku akielezea upinzani wa Beijing kuhusu kushambuliwa miundombinu ya Iran, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, amesema Tehran kamwe haitapigishwa magoti na mashinikizo yoyote ya kijeshi na kwamba hatua hizi zitachochea tu moto wa mivutano.
-
Marekani na Israel zalenga Chuo Kikuu cha Shahid Beheshti katika hujuma dhidi ya sayansi Iran
Apr 03, 2026 22:58Muungano wa kijinai wa Marekani na Israel unaendelea na mashambulizi yake dhidi ya miundombinu ya kitaaluma na ya kiraia nchini Iran, huku shambulizi la karibuni likiharibu vibaya kituo cha utafiti katika Chuo Kikuu cha Shahid Beheshti mjini Tehran.