-
Jeshi la Iran laapa kuendelea na vita hadi Marekani na Israel ‘zitakapojutia’ uchokozi wao
Apr 03, 2026 06:39Msemaji mkuu wa Jeshi la Iran amesema Tehran itaendelea na vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel hadi kuifanya Marekani na utawala wa Israel "zijutie" kitendo chao cha uchokozi kinyume cha sheria.
-
IRGC yashambulia kampuni ya Kimarekani ya Oracle nchini Imarati
Apr 03, 2026 05:24Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu limetangaza katika taarifa yake kuwa: Limetoa kipigo kikali kwa Kampuni ya Kimarekani ya Oracle kufuatia mauaji ya kigaidi ya Mkuu wa Baraza la Kistratejia la Uhusiano wa Nje la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mkewe.
-
IRGC yatungua ndege ya pili ya kivita ya Marekani aina ya F-35 katika anga ya katikati mwa nchi
Apr 03, 2026 04:45Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limetungua ndege ya pili ya kisasa ya Marekani aina ya F-35 ikiwa katika anga katikati ya Iran kwa kutumia mfumo mpya wa ulinzi wa anga wa Kikosi cha Anga cha jeshi hilo.
-
Pezeshkian: Nchi za Ulaya zinawajibika kujibu uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
Apr 03, 2026 04:41Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amekosoa utendaji wa Umoja wa Ulaya mkabala wa ukiukwaji wa wazi wa sheria unaofanywa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, akisema: "Nchi chache za Ulaya zimechukua msimamo wa kuwajibika dhidi ya uchokozi huo, na nyingi zimekuwa na mtazamo wa kutojali na hata wa upendeleo."
-
Iran na Oman kuandaa itifaki ya Lango Bahari la Hormuz
Apr 03, 2026 03:38Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Iran na Oman zinashirikiana kuandaa itifaki ya pamoja ili kuhakikisha usafiri salama wa majini katika Lango Bahari la Hormuz katika kipindi cha baada ya vita.
-
Amir Hatami: Hakuna adui hata mmoja anayepaswa kubakia hai
Apr 02, 2026 07:17Kamanda wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameiagiza Makao Makuu ya Operesheni ya Jeshi kufuatilia nyendo na vitendo vya adui kwa jicho la kushuku na usahihi mkubwa, mara kwa mara, na kutekeleza mipango ya kukabiliana na mbinu za mashambulizi ya adui kwa wakati unaofaa.
-
Lango-Bahari la Hormuz liko chini ya udhibiti kamili wa IRGC
Apr 02, 2026 04:27Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limetangaza kuwa Lango-Bahari la Hormuz sasa liko chini ya udhibiti kamili wa vikosi vyake vya majini, huku likitoa maelezo ya mfululizo wa operesheni za makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya malengo ya Marekani na Israel katika maeneo mbalimbali ya kanda.
-
Rais Pezeshkian: Shambulio dhidi ya miundombinu ya Iran ni dalili ya udhaifu wa Marekani
Apr 02, 2026 04:22Rais wa Iran, amehoji katika ujumbe aliouelekeza kwa wananchi wa Marekani kwamba: Vita vinavyoendelea sasa vinanufaisha vipi maslahi halisi ya watu wa Marekani? Amesisitiza kuwa mashambulio dhidi ya miundombinu muhimu ya Iran, ikiwemo vituo vya nishati na viwanda, ni hatua inayolenga moja kwa moja kuvuruga maisha ya watu wa Iran.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aiambia Hizbullah: Iran itaendelea kuunga mkono Muqawama dhidi ya Marekani na Wazayuni
Apr 01, 2026 05:32Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Ali Khamenei amemwandikia barua Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem, akiahidi kuendeleza uungaji mkono wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa harakati hiyo ya Muqawama na mapambano katika kukabiliana na adui, Marekani na Uzayuni.
-
Brigedia Jenerali Fadavi: Ujinga wa Marekani umewaletea matatizo walimwengu
Apr 01, 2026 04:13Mshauri wa Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: “Walimwengu sasa wanakabiliwa na matatizo makubwa ya nishati kutokana na upumbavu wa shetani mkubwa, Marekani.”