-
Rais Pezeshkian: Ushirikiano wa Iran na EAEU unafungua njia ya kuwa na 'kanda yenye nguvu'
Dec 22, 2025 03:23Rais Masoud Pezeshkian ameulezea ushirikiano wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Umoja wa Kiuchumi wa Ulaya na Asia EAEU kama mkakati wa muda mrefu wa kuimarisha mamlaka ya kitaifa ya kujitawala na kuanzisha kitovu cha nguvu ya kikanda.
-
Iran, Venezuela zalaani 'uharamia' wa Marekani Caribbean
Dec 21, 2025 11:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi na mwenzake wa Venezuela, Yvan Gil Pinto wamefanya mazungumzo kwa njia ya simu ambapo wamelaani uwepo wa jeshi la Marekani katika eneo la Caribbean, wakiishutumu Washington kwa kukiuka sheria za kimataifa, na kusisitiza dhamira yao ya kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika kupinga sera za upande mmoja.
-
Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi: Utawala wa Israel unaficha kushindwa kwa kutoa vitisho
Dec 21, 2025 03:08Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi, Naibu Mkuu wa Majeshi ya Iran, amesema "Israel" inajaribu kuficha kushindwa vikali katika Vita vya Siku Kumi na Mbili kupitia njia ya kutoa vitisho, propaganda za vyombo vya habari na ujanja wa kisiasa.
-
Iran yamnyonga ajenti wa Mossad aliyekuwa akiifanyia ujasusi Israel
Dec 20, 2025 13:02Idara ya Mahakama ya Iran imetangaza kuwa ajenti wa Shirika la Ujasusi la Israel (Mossad) aliyepatikana na hatia ya kuufanyia ujasusi utawala wa Israel, amenyongwa baada ya kukamilika kwa taratibu zote za kisheria.
-
Iran yasisitiza utayari wa mazungumzo kwa msingi wa kuheshimu haki za taifa
Dec 20, 2025 07:17Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amerejelea utayari wa Jamhuri ya Kiislamu kushiriki mazungumzo yanaliyojengwa juu ya heshima kwa haki za taifa, huku akipinga vikali mbinu zozote zinazotegemea shinikizo la upande mmoja.
-
Mabasi ya umeme yaliyoundwa Iran yaanza huduma mjini Tehran
Dec 20, 2025 07:05Kundi la kwanza la mabasi ya umeme yaliyotengenezwa nchini Iran limeanza kutoa huduma katika mji mkuu, Tehran, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha mfumo wa usafiri wa umma na kupunguza uchafuzi wa hewa unaosababishwa na mabasi ya dizeli ya kizamani.
-
Ushirikiano wa Tehran na Moscow; ushirika wa kimkakati katika njia ya mfumo mpya wa kimataifa
Dec 19, 2025 11:33Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitizia kuendelea kwa ushirikiano wa kimkakati na ushirikiano kati ya Tehran na Moscow.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Tuwaombee ushindi Mujahidina wa Ulimwengu wa Kiislamu
Dec 19, 2025 11:25Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa wa Tehran amesema kuwa, tuna wajibu wa kuwaombea dua Mujahidina wanaojitolea kila kitu chao kwa ajili ya kupigania haki na kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu.
-
Rais Pezeshkian atoa mwito wa umoja wa Waislamu duniani
Dec 18, 2025 10:27Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema Muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu, Imam Rouhullah Khomeini (MA) alikuwa mjumbe wa umoja na mshikamano miongoni mwa watu, akisisitiza kwamba mataifa ya Waislamu yanapaswa yaungane ili maadui wasiweze kuibua mifarakano miongoni mwao.
-
Iran yaalani vikwazo vya upande mmoja vya baharini vya Marekani dhidi ya Venezuela
Dec 18, 2025 07:41Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa na kulaani vitisho vya Marekani kwamba itaiwekea vikwazo vya baharini Venezuela na kuitaja hatua hiyo kuwa uharamia unaofadhiliwa na serikali.