-
Iran yamkemea balozi wa Marekani aliyeunga mkono mpango wa “Israel Kubwa”
Feb 22, 2026 08:52Iran imejiunga na nchi na mashirika kadhaa ya Kiislamu na Kiarabu katika kulaani vikali kauli za balozi wa Marekani katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu, aliyedokeza kuwa Israel ina haki ya kupanua uvamizi wake hadi sehemu kubwa ya Asia Magharibi.
-
Iran yajibu mapigo kwa kuyatambua majeshi ya wanamaji na wanaanga ya EU kama mashirika ya 'kigaidi'
Feb 22, 2026 03:21Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa kuhusu uchukuaji hatua za kujibu mapigo kukabiliana na uamuzi haramu wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, EU wa kuviwekea lebo ya ugaidi baadhi ya vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
China, Russia zasisitiza kutatuliwa kidiplomasia kadhia ya nyuklia ya Iran
Feb 21, 2026 22:46Wawakilishi wa Russia na China katika mashirika ya kimataifa yenye makao yake mjini Vienna Austria wamesisitiza suluhisho la kidiplomasia kwa suala la nyuklia la Iran.
-
Iran yaonya kuhusu wapenda vita wanaotaka “vita vya maafa”
Feb 21, 2026 04:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Marekani haijawahi kudai kusitishwa kabisa kwa urutubishaji wa urani katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yanayoendelea, huku akionya kuwa baadhi ya wenye misimamo mikali wanajaribu kuisukuma sera ya Marekani kuelekea katika “vita visivyo vya lazima na vya maafa.”
-
Russia yasisitizia uungaji mkono wake kwa haki za kisheria za Iran katika mazungumzo ya nyuklia
Feb 20, 2026 22:50Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetangaza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Sergey Lavrov amesema Moscow inaunga mkono kufikiwa suluhisho la kisiasa na kidiplomasia litakaloheshimu haki za kisheria za Iran katika mazungumzo ya nyuklia na Marekani.
-
"Vyombo vya diplomasia vya Iran vijadiliane kwa kuzingatia hekima, izza, na maslahi ya taifa"
Feb 20, 2026 08:03Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, "Vyombo vya kidiplomasia (vya Iran) lazima vichore ramani yake ya mazungumzo kwa njia sahihi, ya uwazi na ufasaha, kwa kuzingatia kanuni za heshima, uwazi na hekima, na kuchukua hatua za ujasiri na imara katika njia hii."
-
Iran yaonya: Hatutaanzisha vita, lakini tutajibu vikali uvamizi wowote
Feb 20, 2026 06:18Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kwamba, Jamhuri ya Kiislamu haitaanzisha vita, lakini itatoa jibu zito kwa kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya nchi hii.
-
Majeshi ya majini ya Iran, Afrika Kusini na Sri Lanka kushirikiana usalama baharini
Feb 20, 2026 03:45Kamanda wa Jeshi la Wanamaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza udharura wa ushirikiano kati ya vikosi vya majini vya Iran na vile vya Afrika Kusini na Sri Lanka ili kukabiliana na vitisho vya pamoja na kuhakikisha usalama endelevu katika maji ya kimataifa.
-
Mauzo ya nje ya kilimo ya Iran yaongezeka, asilimia 85 ya chakula ni uzalishaji wa ndani
Feb 20, 2026 03:44Waziri wa Jihadi ya Kilimo wa Iran ametangaza ongezeko kubwa la mauzo ya nje ya kilimo hapa nchini hadi dola bilioni nane na kutangaza kwamba asilimia 85 ya usalama wa chakula wa Iran inadhaminiwa na uzalishaji wa ndani.
-
Kiongozi Muadhamu ahudhuria hafla ya Qur'ani siku ya kwanza ya Ramadhani
Feb 19, 2026 23:58Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amehudhuria kikao cha kiroho cha Qur'ani katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, akijumuika na maqarii na wasomaji mashuhuri wa Iran na kimataifa wa Qur'ani Tukufu.