-
Pezeshkian: Iran itaendelea kuunga mkono Muqawama wa Palestina
Sep 03, 2024 23:34Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema kuwa, serikali yake iko tayari kutoa uungaji mkono usiotetereka kwa ajili ya mapambano ya mataifa yote yanayodhulumiwa duniani kote, hususan Muqawama wa Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel.
-
Iran yahimiza kuchukuliwa hatua za ‘haraka na madhubuti’ za kukomesha jinai za Israel Ghaza
Sep 03, 2024 03:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi anasema kuwa, jamii ya kimataifa lazima ichukue hatua za "haraka na madhubuti" za kukomesha jinai na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni huko Ghaza.
-
Jeshi la Iran lazindua Kifaru kipya cha teknolojia ya hali ya juu
Sep 03, 2024 01:12Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limezindua kifaru kilichoboreshwa kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu ili kuimarisha uwezo wake wa kivita na kukabiliana na maadui.
-
Iran: Dunia haitasahau nafasi ya UK katika kuundwa utawala wa Kizayuni
Sep 02, 2024 23:38Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, mataifa ya kieneo na dunia kwa ujumla hayatasahau mchango na nafasi ya Uingereza katika kuundwa utawala wa kibaguzi wa Israel katika kitovu cha ulimwengu wa Kiislamu.
-
Pezeshkian afafanua mipango ya serikali yake katika mazungumzo na wananchi
Sep 02, 2024 09:02Katika mazungumzo yake ya kwanza ya televisheni na wanachi, Rais Masoud Pezeshkian amefafanua mipango ya serikali yake katika nyanja za ndani na nje ya nchi, na kusema kuwa vipaumbele vya serikali ya 14 ni kuwaridhisha wananchi, kuzingatia masuala ya kiuchumi na kuimarisha uhusiano na nchi mbalimbali.
-
Iran yaghariki katika maombolezo ya Siku ya Kufariki Dunia Mtume Muhammad SAW
Sep 02, 2024 07:34Wananchi Waislamu wa Iran jana usiku na leo Jumatatu mchana wameshiriki katika maombolezo ya kukumbuka siku alipofariki dunia Bwana Mtume Muhammad SAW katika kona zote za nchi hususan Misikitini, katika Haram na maeneo mengine ya ibada.
-
Iran yaonya kuhusu njama za Israel za kuzusha mgogoro hatari Asia Magharibi
Sep 02, 2024 07:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran leo ameashiria jinai za utawala wa Kizayuni zinazoendelea kwenye Ukanda wa Ghaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kusema kuwa, utawala huo dhalimu unafanya njama za kugeuza hali tete iliyopo kwenye eneo hili hivi sasa kuwa mgogoro hatari.
-
Iran: Jamii ya kimataifa iwawajibishe ‘vinara wa mauaji ya kimbari’ wa Israel
Sep 02, 2024 04:26Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametoa wito wa kuwajibishwa "viongozi watenda jinai" wa utawala wa Israel kwa jinai zao dhidi ya raia wa Palestina katika Ukanda wa Gaza, huku vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo lililozingirwa vikiendelea bila kusitishwa.
-
Hali mbaya ya hewa, ukungu ndio chanzo kikuu cha ajali ya helikopta ya Rais Raisi, ripoti ya mwisho yasema
Sep 02, 2024 00:08Uchunguzi wa mwisho wa Jeshi la Iran kuhusu ajali ya helikopta iliyosababisha kifo cha Rais Ebrahim Raisi na wenzake kadhaa mwezi Mei mwaka huu unasema tukio hilo lilisababishwa na hali mbaya ya hewa iliyojumuisha ukungu mkubwa.
-
Araghchi asisitiza kuendelea sera za Iran za kuunga mkono muqawama
Sep 01, 2024 23:33Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza ulazima wa kuendelezwa sera za taifa hili za kuunga mkono Muqawama na mapambano dhidi ya utawala ghasibu wa Israel.