-
Kan'ani: Mahakama ya The Hague isisalimu amri mbele ya mashinikizo ya Marekani kuhusu Palestina
Jan 11, 2024 23:14Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema: Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) inapaswa kuchunguza kiadilifu shauri la Afrika Kusini na baadhi ya serikali nyingine dhidi ya utawala wa Kizayuni kuhusiana na jinai dhidi ya watu wa Gaza na isisalimu amri mbele ya mashinikizo ya kisiasa na yasiyo yza kisiasa ya Marekani.
-
Jeshi la Wanamaji la Iran lakamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama
Jan 11, 2024 12:06Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuikamata meli ya mafuta ya Marekani kwa amri ya mahakama katika Bahari ya Oman.
-
Profesa wa Iran; Mvumbuzi bora wa mwaka 2023
Jan 11, 2024 04:18Profesa Msaidizi katika Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Sharif cha Tehran, Iran ameshinda Tuzo Bora kwa jina la (Best Patent Award 2023) ya Kamati ya Kudumu ya Ushirikiano wa Kisayansi na Kiteknolojia ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (COMSTECH).
-
Iran yajiunga na kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel kuhusu mauaji ya kimbari ya Gaza
Jan 11, 2024 01:08Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuunga mkono uamuzi wa Afrika Kusini wa kuwasilisha kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Diplomasia ya Qur'ani ina nafasi kubwa ya kuleta mazungumzo baina ya dini tofauti
Jan 11, 2024 00:39Mshauri wa Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu wa Iran amesema kuwa, diplomasia ya Qur'ani ina nafasi kubwa katika kueneza utamaduni wa mazungumzo baina ya wafuasi wa dini tofauti kama ambavyo ina nafasi kubwa sana ya kuleta umoja na mshikamano kati ya Waislamu wenyewe kwa wenyewe.
-
Mkutano wa dharura wa mabunge ya nchi za Kiislamu wafanyika Tehran kujadili Gaza
Jan 10, 2024 08:56Spika wa Bunge la Iran Mohammad Baqer Qalibaf anasema utawala wa Kizyauni wa Israel uliasisiwa kwa mauaji ya kimbari na vita na hivyo kuendelea kuwepo kwake kunategemea kutekelezwa jinai hizo za kutisha.
-
Iran na Russia: Marekani inatafuta visingizio vya kupanua uwepo wake katika eneo
Jan 10, 2024 03:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian na mwenzake wa Russia Sergei Lavrov wamesema Marekani inajaribu kubuni visingizio ili kupanua uwepo wake katika eneo. Wanadiplomasia hao wakuu wa Tehran na Moscow wametoa indhari hiyo katika mazungumzo waliyofanya kwa njia ya simu jana Jumanne.
-
Kufichuliwa nafasi ya jasusi wa Uholanzi katika hujumu dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran
Jan 10, 2024 02:34Gazeti la Volkskrant la Uholanzi limefichua kuwa, raia mmoja wa nchi hiyo alikuwa na mchango mkubwa katika operesheni ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuhujumu kituo cha kurutubisha uranium cha Natanz nchini Iran.
-
Damu safi ya watu wa Gaza itaharakisha mkondo wa kuangamia Israel
Jan 10, 2024 01:48Kamanda mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu Iran anasema utawala haramu wa Israel unamwaga damu ya Wapalestina wasio na hatia ili kufidia "kushindwa kwake kwa fedheha" katika vita vya Gaza, akionya kwamba ukatili huo utaharakisha mkondo wa kuangamia utawala huo.
-
Damu safi ya watu wa Gaza itaharakisha mkondo wa kuangamia Israel
Jan 10, 2024 01:07Kamanda mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu Iran anasema utawala haramu wa Israel unamwaga damu ya Wapalestina wasio na hatia ili kufidia "kushindwa kwake kwa fedheha" katika vita vya Gaza, akionya kwamba ukatili huo utaharakisha mkondo wa kuangamia kwa utawala huo.