-
Iran: Marekani haina ustahiki kuwatuhumu wengine; inachukiwa zaidi kwa kuiunga mkono Israel
Dec 25, 2023 23:29Iran imepuuzilia mbali shutuma "zisizo na thamani" za Marekani kwamba inazidisha mvutano katika bahari kuu, ikisema Washington, ambayo ni mshirika katika vita vya mauaji ya halaiki yanayofanywa na Israel kwenye Ukanda wa Gaza, "haina ustahiki" wa kutoa madai dhidi ya Tehran.
-
Radiamali ya Amir Abdollahian kwa madai ya Marekani kuhusu hatua ya Yemen dhidi ya meli za Israel
Dec 25, 2023 23:09Hossein Amir Abdollahian, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kusisitiza kuwa Iran haina askari wa niaba katika eneo la Asia Magharibi amesisitiza kuwa, Iran haihusiki na mashambulizi ya Yemen dhidi ya meli za Israel.
-
"Ubeberu wa US unaporomoka, muqawama ndiyo nguzo ya usalama katika eneo"
Dec 25, 2023 07:13Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Wamarekani wamekiri wenyewe kwamba, nidhamu ya dunia iliyojengeka katika misingi ya ubeberu ipo katika mkondo wa kuporomoka, na kwamba mabeberu hawawezi kuendelea kuwatwisha walimwengu misimamo na mitazamo yao.
-
Ebrahim Raisi: Wanaodai kuwa wafuasi wa Nabii Issa (as) hawapaswi kuiunga mkono Israel na mauaji yake dhidi ya watoto
Dec 25, 2023 00:57Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kuwa, wale wote wanaodai kwamba ni wafuasi wa Nabii Issa Masih (as) hawapaswi kuiunga mkono Israel na mauaji yake dhidi ya watoto huko katika Ukanda wa Gaza.
-
Mwakilishi wa Jihadul Islami: Iran ni muungaji mkono pekee wa wananchi wa Gaza na wanaodhulumiwa duniani
Dec 24, 2023 23:12Mwakilishi wa Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina nchini Iran amekosoa kimya cha nchi za Magharibi mkabala wa vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya wananchi wa Palestina katika Ukanda wa Gaza na kusema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni muungaji mkono pekee wa wanaodhulumiwa duniani.
-
Amir-Abdollahian: Kuna haja ya kuimarishwa harakati za kidiplomasia ili kukabiliana na jinai za Wazayuni
Dec 25, 2023 03:41Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya kuimarishwa juhudi za kidiplomasia kwa shabaha ya kukabiliana na jinai za Wazayuni katika Ukanda wa Gaza.
-
Jeshi la Wanamaji la Iran lapokea makombora mapya ya cruise
Dec 24, 2023 08:32Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limepokea mfumo wa kimkakati wa makombora ya cruis wa Talayieh na mfumo wa makombora wa Nasir na hali kadhalika helikopta za kwanza za vita vya kieletroniki na kijasusi.
-
Mazungumzo ya kwanza ya simu baina ya Marais wa Iran na Misri; hatua ya kukuza uhusiano
Dec 24, 2023 04:44Jana Jumamosi, Sayyid Ebrahim Raisi, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alizungumza kwa simu na Rais Abdel Fattah El Sisi wa Misri, ikiwa ni mara ya kwanza kwa marais wa nchi hizi mbili kuzungumza kwa simu na ikiwa ni katika sehemu ya juhudi za kufufua uhusiano wa pande mbili.
-
Rais Ebrahim Raisi: Marekani na Israel zishtakiwe kwa kufanya mauaji ya kimbari Gaza
Dec 23, 2023 23:09Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria chimbuko la matukio ya hivi karibuni huko Palestina na kusema kuwa, Marekani na utawala wa Kizayuni zinapaswa kushtakiwa kwa kufanya mauaji ya kimbari huko Gaza.
-
Marais wa Iran na Misri wahimiza kustawishwa uhusino wa nchi mbili katika nyuga zote
Dec 23, 2023 23:08Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumza kwa simu na rais mwenzake wa Misri na kutilia mkazo udharura wa kustawishwa uhusiano wa nchi hizi mbili katika nyuga tofauti.