-
Msishiriki katika uchokozi dhidi ya Iran, Gharibabadi azionya nchi za Ulaya
Jul 24, 2026 02:51Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amezionya nchi za Ulaya kwamba kutoa kambi au maeneo ya kijeshi kwa Marekani kutaziweka "katika safu ya wavamizi."
-
Iran iko tayari kuanzisha awamu mpya ya vita na kutumia mikakati mipya
Jul 24, 2026 02:42Msemaji wa jeshi la Iran jana Alhamisi alitahadharisha kuwa Tehran itatumia mikakati na mbinu mpya ili kuifanya Marekani ishindwe kuendeleza vita iwapo mashambulio ya nchi hiyo dhidi ya miundombinu ya kusini mwa Iran yataendelea.
-
Iran yaapa kulipiza kisasi iwapo Marekani itashambulia miundombinu
Jul 23, 2026 11:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi, ameweka bayana msimamo thabiti wa Iran kwamba shambulio lolote dhidi ya miundombinu ya Iran litajibiwa kwa hatua stahiki na za maamuzi dhidi ya wachokozi na wale wote wanaowasaidia.
-
Viongozi wa Iran na Iraq wasisitiza kuimarisha mahusiano ya kimkakati
Jul 23, 2026 11:49Viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iraq wamesisitiza juu ya mafungamano marefu ya kihistoria, kiutamaduni, kidini, na ya kijamii yaliyopo baina ya nchi hizo mbili, wakibainisha ulazima wa kuhifadhi na kuimarisha rasilimali hii yenye thamani kuu kama nguzo imara ya kutanua ushirikiano wa kimkakati.
-
Mashambulizi Makali ya Iran dhidi ya Vituo vya Marekani nchini Jordan
Jul 23, 2026 08:20Mashambulizi ya Iran dhidi ya vituo vya Marekani nchini Jordan yanachukuliwa kuwa miongoni mwa operesheni zilizofanikiwa zaidi katika mzozo wa kijeshi wa hivi karibuni kati ya Iran na Marekani.
-
Dkt. Pezeshkian: Hakuna sababu wala mpaka unaoweza kuvunja uhusiano wa Iran na Iraq
Jul 23, 2026 03:15Rais Masoud Pezeshkian wa Iran, amesema kuwa hakuna sababu yoyote wala mipaka ya kijiografia inayoweza kuvunja uhusiano wa kindugu na wa kihistoria uliopo kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iraq.
-
Mkuu wa Majeshi Iran aionya Marekani kuhusu hujuma ya kijeshi ya nchi kavu
Jul 23, 2026 03:07Mkuu wa Majeshi ya Iran, Meja Jenerali Amir Hatami, ametoa onyo kali kwamba uvamizi wowote wa nchi kavu wa jeshi la Marekani utakabiliwa na jibu la kijeshi la kuangamiza. Amesisitiza kuwa mamilioni ya Wairani wako tayari kuwakabili wavamizi kwa kila nyenzo waliyo nayo, huku Majeshi ya Ulinzi yakiwa katika utayari wa hali ya juu dhidi ya uchokozi wowote.
-
Ripoti: Tathmini ya CIA yakiri hujuma za Marekani dhidi ya Iran zimeshindwa
Jul 23, 2026 02:53Tathmini mpya ya kiintelijensia ya Marekani imetoa pigo kubwa kwa propaganda za kivita za utawala wa Donald Trump, kwa kuhitimisha kwamba kuendelezwa kwa uchokozi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hakutaweza kufanikisha malengo yoyote yaliyotangazwa na Ikulu ya White House.
-
Minab yazika vipande 62 vya miili ya watoto 32 waliouawa katika mashambulizi ya Marekani Februari 28 shuleni
Jul 22, 2026 11:54Zaidi ya vipande 62 vya miili ya wanafunzi 32 waliouawa katika shambulio la anga la Marekani katika Shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh huko Minab kusini mwa Iran vimetambuliwa kupitia vipimo vya vinasaba (DNA) na kuzikwa, karibu miezi mitano baada ya mashambulizi yaliyoua wanafunzi na walimu wao wasiopungua 168.
-
Rais Pezeshkian: Katu hatutalegeza kamba kuhusu haki za taifa la Iran
Jul 22, 2026 09:52Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kuwa mazungumzo yaliyofanyika kati ya Iran na Marekani yalianzishwa kwa kuzingatia misingi ya heshima, maslahi ya taifa, busara na hadhi ya Iran.