-
Baqaei: Marekani imefanya uhalifu wa kivita kwa kujaribu nguvu ya kombora lilitumika kwa mara ya kwanza kuua watu Lamerd, Iran
May 26, 2026 11:14Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: "Marekani ilitumia kwa mara ya kwanza kombora la PrMS katika shambulio lake kwenye eneo la makazi ya raia na uwanja wa michezo wa Lamerd katika Mkoa wa Fars kusini mwa Iran, kwa lengo la kujaribu nguvu za uharibifu za silaha hiyo."
-
Baqaei: Marekani inapasa kudhamini ushiriki wa timu ya taifa ya Iran katika mashindano ya Kombe la Dunia
May 26, 2026 02:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amezungumzia uvumi unaoendelea kuhusu kushiriki wa timu ya taifa ya kandanda ya Iran katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026, na kusisitiza kuwa Marekani inawajibika kuandaa mazingira yanayofaa kwa timu hiyo kushiriki katika mashindano bila vizuizi vyovyote.
-
Pezeshkian: Iran haitasalimu amri kwa matakwa 'ya kupitiliza' ya Marekani, inataka kurejeshea haki zake kikamilifu
May 25, 2026 12:28Rais Masoud Pezeshkian ametangaza kwamba Iran haitasalimu amri kwa mashinikizo ya Marekani na matwaka ya kuchupa mipaka ya utawala huo, akisema wapatanishi wa Iran watahakikisha haki za taifa zinarejeshwa kikamilifu kupitia mchakato wa kidiplomasia.
-
Kiongozi wa machafuko yaliyofadhiliwa na Marekani mwezi Januari auawa nchini Iran
May 25, 2026 10:18Mahakama ya Iran imetangaza kwamba mmoja wa viongozi wa makundi yenye silaha yaliyohusika na ghasia zilizofadhiliwa na madola ya kigeni mnamo Januari 2026 amenyongwa katika mji wa Nain.
-
Pezeshkian: Iran iko tayari kuihakikishia dunia kwamba haifuatilii silaha za nyuklia
May 25, 2026 09:19Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kuihakikishia jamii ya kimataifa kwamba haifuatilii silaha za nyuklia.
-
Rezaei: Iran itajiondoa katika mkataba wa kuzuia silaha za nyuklia iwapo itashambuliwa tena
May 25, 2026 09:18Iran imetoa onyo kali kwa Marekani, ikisema kuwa itajiondoa kwenye Mkataba wa Kuzuia Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), ikiwa Marekani itaanzisha tena mashambulizi dhidi ya yake.
-
Rais Pezeshkian: Iran inapigania haki zake halali katika mazungumzo na Marekani
May 24, 2026 12:50Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa Iran inataka kurejesha haki zake halali katika mazungumzo na Marekani. Hata hivyo, ameeleza kuwa uzoefu mchungu wa majadiliano ya huko nyuma na Washington unaifanya Tehran kusonga mbele kwa tahadhari kubwa.
-
Iran yaonya: Tuko tayari kutoa jibu “la maangamizi” dhidi ya uchokozi mpya
May 24, 2026 12:40Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yako katika kiwango cha juu kabisa cha utayari na yataitoa “adhabu yenye maangamizi na ya kuzimu” iwapo adui ataanzisha tena vita au shambulio lolote la kichokozi dhidi ya nchi.
-
Qalibaf: Iran haina imani na Marekani, haitasalimu amri kuhusu haki zake
May 24, 2026 03:30Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Iran haina imani yoyote na Marekani na kwamba haitarudi nyuma kamwe katika kutetea haki zake za kitaifa wakati wa mazungumzo na Marekani yanayolenga kuhitimisha vita katika eneo lote la Asia Magharibi.
-
Jeshi la Iran lasema meli 25 zimepita katika Lango la Hormuz
May 24, 2026 03:28Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetangaza kuwa meli 25, zikiwemo meli za mafuta, meli za mizigo (kontena), na meli zingine kibiashara, zimevuka Lango la Bahari la Hormuz katika kipindi cha saa 24 zilizopita hadi kufikia jana, baada ya kupata idhini na chini ya uratibu wa kiusalama wa jeshi hilo.