-
Baqaei akosoa utovu wa shukrani wa Kuwait na hatua yake ya kuwapokea maadui wa Iran
Jul 22, 2026 09:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei, ameikosoa serikali ya Kuwait kwa kile alichokiita kutokuwa na shukrani nchi hiyo na kuwakaribisha maadui wa Iran licha ya uhusiano wa ujirani uliopo kati ya nchi hizo.
-
Seneta wa Marekani afichua uongo wa Trump kuhusu vita dhidi ya Iran
Jul 22, 2026 06:20Seneta Mark Warner wa Marekani amekiri kwamba "hakuna tishio lolote linalokaribia" kutoka kwa Iran dhidi ya Marekani.
-
Araqchi: Mwenendo wa wanadiplomasia wa Ufaransa Tehran haukubaliki
Jul 22, 2026 03:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amelaani mwenendo wa wanadiplomasia wawili wa Ufaransa mjini Tehran na kuutaja kuwa "usiokubalika," huku akiitaka Paris kuzuia kujirudia vitendo vinavyokwenda kinyume na taratibu za kidiplomasia.
-
Je, ni malengo gani yanafuatiliwa na Marekani katika kushambulia miundombinu ya Iran?
Jul 19, 2026 13:45Kwa madai ya kushambuliwa meli kadhaa zinazopita kinyume cha sheria kusini mwa Lango-Bahari la Hormuz na kukiukwa Mkataba wa Islamabad, Rais Donald Trump wa Marekani aliamuru kuanzishwa tena mashambulizi ya kichokozi dhidi ya Iran kuanzia Julai 7, ambapo pia mzingiro wa majini dhidi ya Iran ulirejeshwa mnamo Julai 14.
-
Iran yaangamiza rada za jeshi la Marekani Magharibi mwa Asia, askari kadhaa wauawa
Jul 21, 2026 11:33Majeshi ya Iran yametekeleza operesheni za uharibifu mkubwa wa miundombinu kadhaa ya rada na mifumo ya mawasiliano ya kijeshi ya Marekani katika eneo hili sambamba na hujuma iliyofanya dhidi ya kambi tatu za Marekani nchini Kuwait, ikiwa ni hatua endelevu ya kulipiza kisasi dhidi ya ukiukaji unaofanywa na Marekani.
-
Iran yataka Baraza la Usalama la UN kulaani shambulizi la Marekani dhidi ya kituo cha nyuklia cha Darkhovin
Jul 21, 2026 11:31Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa wito kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani bila kusita shambulizi la kombora lililofanywa na Marekani dhidi ya Kituo cha Nishati ya Nyuklia cha Darkhovin, na kuthibitisha tena kuwa shambulizi lolote au tishio dhidi ya vituo vya nyuklia vya amani ni kinyume na sheria za kimataifa.
-
Shambulio la Iran dhidi ya Kituo cha Marekani huko Al-Tanf, Syria: Hatua Isiyo na Mfano Wake na Yenye Jumbe za Pande Kadhaa
Jul 21, 2026 06:35Kwa mara ya kwanza tangu kuanguka kwa serikali ya Bashar al-Assad miezi 19 iliyopita, vikosi vya jeshi la Iran vimeshambulia kwa njia ya anga eneo lililo ndani ya ardhi ya Syria.
-
Iran yathibitisha kupokea mapendekezo ya wapatanishi yanayolenga kupunguza mvutano
Jul 21, 2026 03:32Iran imethibitisha kupokea mapendekezo na maoni mbalimbali kutoka kwa wapatanishi kadhaa yanayolenga kupunguza mivutano na Marekani, huku Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Esmaeil Baqaei, akisema kuwa Tehran inaendelea na juhudi za kidiplomasia sambamba na hatua zinazochukuliwa na vikosi vya ulinzi vya Iran.
-
Baqaei: Marekani imeonyesha tena sera yake ya uharibifu kwa kushambulia miundombinu ya Iran
Jul 20, 2026 11:20Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amesema kuwa Marekani imeonyesha kwa mara nyingine tena sera yake ya uharibifu baada ya kufanya mashambulizi dhidi ya miundombinu ya Iran.
-
Kusimamishwa Ahadi za Mkataba wa Islamabad: Majibu ya Iran dhidi ya Ukiukaji wa Marekani
Jul 20, 2026 08:05Iran imesimamisha utekelezaji wa ahadi zake chini ya Mkataba wa Islamabad. Akifafanua suala hilo, Kazem Gharibabadi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, amesema kuwa baada ya Marekani kukiuka wajibu wake chini ya Mkataba wa Maelewano wa Islamabad, Tehran imesimamisha utekelezaji wa ahadi zake zote na kwamba sasa imejikita katika mipango ya kulinda nchi kwa uthabiti mkabala wa hujuma za adui.