-
Iran: Lazima kuwe na kikomo cha kutoadhibiwa Utawala wa Kizayuni
Oct 25, 2025 09:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kwamba hali ya kutoadhibiwa kwa utawala wa Kizayuni wa Israel, ambayo imepewa uhalali na wale wanaounga mkono utawala huo, inapaswa kukoma mara moja.
-
Iran: Baraza la Usalama halipaswi kukubali kudanganywa na kutumiwa vibaya
Oct 25, 2025 01:52Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema: Hati ya Umoja wa Mataifa imekumbana na mitihani mingi mizito kutokana na vitendo vya ukatili na kutumiwa vibaya kisiasa ya taasisi zake.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran: Trump ni mlea magaidi
Oct 24, 2025 06:41Imamu wa muda wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesisitiza kuwa Rais wa Marekani Donald Trump ni gaidi, na iwapo dunia inataka kumtambua gaidi halisi, basi mtu huyo si mwingine bali ni Trump mwenyewe.
-
Ali Larijani:Mashinikizo ya kiuchumi hayawezi kuvunja irada imara ya Iran
Oct 24, 2025 06:38Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Larijani, amesisitiza kuwa mashinikizo la kiuchumi kutoka mataifa ya Magharibi hayawezi kuathiri uthabiti wa taifa.
-
Iran yalaani muswada wa Knesset ya Israel wa kunyakuliwa Ukingo wa Magharibi
Oct 24, 2025 04:16Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali muswada uliopasishwa katika Bunge la Israel (Knesset) wa kunyang'anywa eneo la Ukingo wa Magharibi huko Palestina ukiutaja kuwa ni ukiukaji wa wazi wa hati na kanuni za Umoja wa Mataifa.
-
Iran yamuonya mkuu wa IAEA: Vitisho vilivyofeli havitaleta isipokuwa kusindwa kwingine
Oct 24, 2025 00:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amemuonya mkuu wa shirika la nyuklia la Umoja wa Mataifa, Rafael Grossi, dhidi ya kutoa "vitisho vilivyoshindwa" dhidi ya Tehran, akisema matamshi kama hayo hayataleta "isipokuwa kushindwa kwingine."
-
Mahdieh Esfandiari Muirani mtetezi wa Palestina aachiliwa huru
Oct 23, 2025 23:24Mahdieh Esfandiari, mwanaharakati wa Iran anayewaunga mkono watu wa Palestina, ameachiliwa kwa masharti kutoka katika jela ya Ufaransa baada ya kuzuiliwa kwa zaidi ya miezi saba.
-
Waziri wa Usalama wa Taifa: Iran haina imani kuhusu kulindwa maslahi ya taifa kupitia mazungumzo na Marekani
Oct 23, 2025 07:47Waziri wa Usalama wa Taifa wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu haina imani kabisa kuhusu kulindwa maslahi ya nchi hii kupitia kufanya mazungumzo na Marekani.
-
Iran: Mashirika 50 ya kijasusi yaliisaidia Israel katika Vita vya Siku 12 dhidi yetu
Oct 22, 2025 23:41Waziri wa Usalama wa Taifa wa Iran amesema: Katika vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel mwezi Juni mwaka huu dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, adui alipanga kuzusha uvunjifu mkubwa wa amani nchini Iran na alijaribu kutumia magaidi wake wote wakufurushiaji walioachiwa huru huko Syria na Afghanistan kwa ajili ya kuvuruga usalama wa Iran ya Kiislamu lakini alishindwa. Mashirika 50 ya kijasusi yaliisaidia Israel lakini pia yalishindwa.
-
Iran: Hatutarudi kwenye meza ya mazungumzo hadi Marekani iachane na sera zake za kupenda makuu
Oct 22, 2025 23:11Sayyid Abbas Araqchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, sharti la kurejea Iran katika meza ya mazungumzo ni Wamarekani kuacha siasa zao za kijuba na za kupenda makuu.