-
Hamas yatoa wito wa kuchukuliwa hatua za kimataifa za kuvunja mzingiro wa Gaza, kukomeshwa mashambulizi ya Israel, kuhamishwa watu kwa mabavu
Feb 03, 2026 09:57Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ) imetoa wito kwa jamii ya kimataifa kushiriki katika maandamano ya hasira na shughuli za mashinikizo dhidi ya mashambulizi na mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na Israel dhidi ya watu wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Ripoti: Israel inashikilia miili 766 ya Wapalestina tangu Oktoba 2023
Feb 03, 2026 07:56Mamlaka za Israel zinashikilia miili ya Wapalestina 766 waliokwishatambuliwa, huku karibu nusu ya miili hiyo ikishikiliwa tangu Oktoba 2023, wakati Israel ilipoanzisha vita vya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza ulio chini ya mzingiro.
-
Utafiti: Idadi ya watu Gaza imepungua kwa 254,000 kutokana na vita
Feb 03, 2026 02:29Utafiti wa kuaminika uliochapishwa na gazeti la Uingereza la The Guardian umehitimisha kwamba idadi ya watu wa Ukanda wa Gaza imepungua kwa takriban watu 254,000, au 10.6%, ikilinganishwa na makadirio ya kabla ya kuanza kwa vita vya mauaji ya kimbari ya Israel, Oktoba 7, 2023.
-
Kundi la kwanza la Wapalestina wanaorejea kutoka Misri lapitia kivuko cha Rafah
Feb 02, 2026 13:54Kundi la kwanza la Wapalestina limeanza kurejea katika Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha mpaka cha Rafah kati ya eneo hilo la pwani na Misri, baada ya kivuko hicho kufunguliwa tena kwa ajili ya harakati za watu.
-
Mataifa ya Kiislamu na Kiarabu yailaani Israel kwa kukiuka usitishaji vita Gaza
Feb 02, 2026 07:11Mataifa kadhaa ya Kiislamu na Kiarabu yameulaani vikali utawala haramu wa Israel kwa kukiuka usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza
-
Hamas: Israel isitishe jinai ili mapatano ya usitishaji vita Gaza yafanikiwe
Feb 02, 2026 03:10Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas, katika Ukanda wa Gaza amesisitiza kuwa harakati za Palestina zimejitolea kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano na kwamba mafanikio ya mapatano hayo sasa yanategemea kulazimishwa utawala haramu wa Israel kuyazingatia na kujiepusha na jinai inazoendeleza dhidi ya Wapalestina.
-
Wanazuoni wa Yemen watangaza mshikamano na Iran
Feb 02, 2026 02:42Jumuiya ya Wanazuoni wa Yemen imetangaza mshikamano wake kamili na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kutaka ulimwengu wa Kiislamu kuchukua msimamo wa pamoja katika suala hilo.
-
Afisa wa Umoja wa Mataifa: Usitishaji mapigano Gaza si wa kweli
Feb 01, 2026 05:20Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) amelaani shambulio la jeshi la Israel katika kitongoji cha Sheikh Radwan kaskazini magharibi mwa Jiji la Gaza, ambalo limeua makumi ya Wapalestina akisema kwamba makubaliano ya kusitisha mapigano katika eneo hili si ya kweli.
-
Askari 10 na magaidi 109 wauawa katika mapigano kwenye jimbo la Balochistan, Pakistan
Feb 01, 2026 02:28Askari wasiopungua 10 na magaidi 109 wameuawa katika mapigano wakati vikosi vya usalama vya Pakistan vilipozima mashambulizi makubwa "yaliyoratibiwa" katika jimbo la kusini-magharibi mwa Balochistan. Hayo yalielezwa jana Jumamosi na afisa mmoja wa usalama wa Pakistan.
-
Israel yaua Wapalestina 31 wakiwemo watoto 6 katika ukiukaji mpya wa usitishaji vita Ghaza
Jan 31, 2026 14:44Wapalestina wasiopungua 31, wakiwemo kwa uchache watoto sita, wameuawa shahidi katika mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel tangu alfajiri ya leo hadi wakati huu katika Jiji la Ghaza na mji wa Khan Younis katika Ukanda wa Ghaza.