-
Yemen yatangaza marufuku ya meli za Israel katika Bahari ya Sham
Jun 08, 2026 11:13Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza marufuku kamili ya usafiri wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu (Bahari ya Sham), vikisema kwamba harakati zote za adui katika eneo hilo sasa zitachukuliwa kuwa malengo halali ya kijeshi, baada ya kutekeleza shambulizi la kombora lenye usahihi dhidi ya maeneo nyeti ya Israel huko Tel Aviv.
-
Waandishi wa habari wa Gaza wasimulia unyanyasaji waliokumbana nao katika gereza la Israel
Jun 07, 2026 03:50Shirika la Waandishi wa Habari Wasio na Mipaka (RSF) limechapisha ushuhuda kutoka kwa waandishi wa habari watano wa Kipalestina huko Gaza, ambao walitekwa nyara na askari wa Israel baada ya Oktoba 7, 2023 ikiwa ni pamoja na visa vya unyanyasaji, kuhojiwa na ukiukwaji wa sheria unaohusiana moja kwa moja na shughuli zao za uandishi wa habari.
-
Israel na walowezi wa Kizayuni wazidisha mashambulizi katika Ukingo wa Magharibi
Jun 07, 2026 03:18Wanajeshi wa Israel na walowezi wa Kizayuni wamezidisha mashambulizi yao dhidi ya Wapalestina katika eneo la Ukingo wa Magharibi linalokaliwa kwa mabavu.
-
Utawala wa Bahrain unafuatilia malengo gani katika kuwatia mbaroni viongozi wa kidini?
Jun 05, 2026 14:06Ikiwa ni katika kuendeleza siasa zake za kuwakandamiza viongozi mashuhuri wa kidini Utawala wa Al Khalifa nchini Bahrain umewatia nguvuni viongozi wengine kadhaa wa kidini.
-
Hizbullah yashambulia vikosi vamizi vya Israel kusini mwa Lebanon
Jun 05, 2026 11:19Wapiganaji wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon wametekeleza wimbi la mashambulizi yaliyoratibiwa siku ya Alhamisi, wakilenga ngome kadhaa za kijeshi za Israel na kusababisha hasara kubwa kwa wanajeshi hao vamizi wa Kizayuni.
-
Foreign Policy: Chuki dhidi ya Wakristo imeongezeka huko Israel
Jun 04, 2026 03:12Uchunguzi uliofanywa na baadhi ya vyombo vya habari umebaini kuwa chuki na hujuma dhidi ya Wakristo vimeongezeka huko Israel.
-
Wanajeshi wa Israel wakiona cha mtemakuni Lebanon; ripoti ya Marekani: Hizbullah sasa ina uwezo zaidi kuliko awali
Jun 03, 2026 13:25Harakati ya muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imesema imetoa kipigo kikubwa kwa wanajeshi wa Israel katika mji wa al-Bayyada, kusini mwa Lebanon, huku jeshi la Israel likiendelea kushindwa na wanajeshi wake wakikabiliwa na mbinu za kisasa zaidi.
-
Je, Israel inafuatilia malengo gani katika kuzidisha vita nchini Lebanon?
Jun 03, 2026 12:13Utawala wa Kizayuni unaendelea kushambulia Lebanon ambapo katika siku za hivi karibuni ulikuwa umetishia kuushambulia mtaa wa Dhahiyah kusini mwa Beirut na kutaka watu wahame kutoka eneo hilo. Swali muhimu ni je, kwa nini utawala wa Kizayuni unataka kushadidisha mgogoro na vita nchini Lebanon?
-
Yemen yatishia kutoa jibu la pande zote kwa ongezeko lolote la mashambulizi ya Israel nchini Lebanon
Jun 03, 2026 04:10Harakati ya mapambano ya Ansarullah nchini Yemen imetangaza kuwa vikosi vya jeshi la Israel vilivyotumwa Lebanon vitaendelea kuwa katika hatari ya mashambulizi yatakayofanywa na harakati hiyo kuonyesha mshikamano na Lebanon na harakati yake ya mapambano ya Hizbullah hadi vitakapoondoka kabisa kwenye ardhi ya Lebanon.
-
Waliowengi Baraza la Usalama la UN walaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon
Jun 02, 2026 09:08Idadi kubwa ya wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wameonyesha kutokuridhishwa kwao na kuongezeka kwa mashambulizi ya kijeshi ya Israel dhidi ya Lebanon. Wakati hayo yakijiri, Marekani imepuuza kuukosoa utawala wa Israel, badala yake ikielekeza lawama zake zote kwa harakati ya Muqawama ya Hizbullah na nchi ya Iran.