-
Wapalestina wanakoseshwa kufunga na kufungua Saumu kwa wakati kwenye jela za Israel
Feb 24, 2026 04:06Tume moja ya Palestina inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye jela za utawala wa kizayuni wa Israel imezishutumu mamlaka za jela hizo kwa kuwafanya Wapalestina hao washindwe kufunga Saumu zao "kwa wakati sahihi" katika mfungo huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Mkutano wa dharura wa mawaziri wa mambo ya nje wa OIC kujadili unyakuzi wa Israel wa ardhi za Palestina
Feb 23, 2026 07:09Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) itafanya mkutano wa dharura katika ngazi ya mawaziri wa mambo ya nje Alhamisi ijayo kujadili maamuzi ya hivi karibuni ya Israel yanayozidisha ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na unyakuzi wa ardhi za Palestina katika Ukingo wa Magharibi.
-
Ansarullah yalaani mauaji ya umati ya umwagaji damu ya Israel mashariki mwa Lebanon
Feb 23, 2026 03:39Harakati ya Ansarullah ya Yemen imelaani vikali "mauaji ya umati ya umwagaji damu" yaliyofanywa na utawala wa Israel katika eneo la Beqaa mashariki mwa Lebanon, na kuuwa takriban watu kumi na kujeruhi wengine wengi.
-
Kiongozi wa Ansarullah: Marekani ni mshirika wa adui Mzayuni katika jinai zake zote
Feb 23, 2026 03:38Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen, ameashiria kile kinachojulikana kama "Bodi ya Amani ya Trump" kwa ajili ya Gaza, na kusema: "Marekani ni mshirika wa adui Mzayuni katika jinai zake zote."
-
Matamshi ya Huckabee yalaaniwa vikali katika Ulimwengu wa Kiislamu, yaitwa ya 'kipuuzi' na 'kichochezi'
Feb 22, 2026 06:50Matamshi ya balozi wa Marekani katika utawala wa kizayuni wa Israel Mike Huckabee kwamba utawala huo ghasibu una haki ya kupanua eneo lake kwa kupora eneo kubwa la Mashariki ya Kati la nchi kadhaa za Kiarabu na Kiislamu za eneo hilo yamekosolewa na kulaaniwa vikali na nchi hizo, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu, OIC, Jumuiya ya Waarabu na makundi ya ukombozi wa Palestina.
-
Wazayuni washadidisha mashambulizi Ukingo wa Magharibi katika mwezi wa Ramadhani
Feb 22, 2026 06:48Sambamba na kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani, jeshi la utawala wa Kizayuni limeshadidisha mashambulizi yake katika maeneo mbalimbali ya Ukingo wa Magharibi huko Palestina.
-
Ansarullah: Kujizatiti upya kijeshi maadui katika eneo ni ishara kwamba Muqawama ungali hai
Feb 21, 2026 11:08Mjumbe mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Yemen ya Ansarullah ametoa taarifa akieleza kwamba kuzungumziwa duru mpya ya vita vinavyotaka kuanzishwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Muqawama ni sawa na adui kukiri kwamba alishindwa katika vita vilivyopita.
-
Licha ya vizuizi vikali vya Israel, Wapalestina laki moja wasali I'sha na Tarawehe Masjidul-Aqsa
Feb 21, 2026 11:07Licha ya vizuizi vikali vilivyowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vya kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa, makumi ya maelfu ya Wapalestina jana usiku walihudhuria katika msikiti huo mtukufu kusali Sala za I'sha na Tarawehe wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Mtazamo wa Moscow kuhusu maneva ya pamoja ya baharini kati ya Iran, Russia na China
Feb 21, 2026 09:11Moscow imetangaza kuwa mazoezi ya pamoja ya majini kati ya majeshi ya Iran, Russia na China yatafanyika katika Lango -Bahari la Hormuz.
-
Balozi wa Marekani: Ni sawa ikiwa Israel itanyakua ardhi kote Asia Magharibi
Feb 21, 2026 07:35Balozi wa Marekani katika utawala Israel amesema itakuwa “sawa tu” iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utapanua mipaka yake kote katika Asia Magharibi chini ya mpango wa “Israeli Kubwa.”