-
Nchi 14 zikiwemo za EU zalaani mpango wa ujenzi haramu Ukingo wa Magharibi
Dec 25, 2025 06:40Kundi la nchi 14 zikiwemo za Ulaya limetoa taarifa ya pamoja ya kulaani vikali uamuzi wa Israel wa kuanzisha ujenzi mpya wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, na kuitaja hatua hiyo kuwa ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Hamas yasisitiza kuwa haitaweka chini silaha
Dec 25, 2025 02:39Harakati ya Kiislamu (Muqawama) ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas, imetangaza wazi kuwa haitakubali jaribio lolote la kuipokonya silaha, ikionya dhidi ya kuingiliwa mambo ya Palestina na mataifa ya kigeni. Hamas imesisitiza kuwa inahitaji dhamana zilizo wazi na madhubuti zaidi kwa awamu ya pili ya makubaliano ya kusitisha mapigano na utawala wa Israel.
-
Wazayuni wajigamba kwa kuishambulia kijeshi Qatar
Dec 24, 2025 11:26Waziri mmoja wa utawala wa Kizayuni wa ameishambulia Qatar kwa maneno makali na kutamba kuwa shambulio la miezi ya hivi karibuni lililofanywa na Israel nchini Qatar lilikuwa ni "hatua sahihi" iliyokuwa ya lazima kuchukuliwa.
-
Waziri wa Vita wa Israel afuta haraka matamshi yake kuhusu uvamizi
Dec 24, 2025 11:26Waziri wa Vita wa Israel amelazimika kufuta matamshi yake saa chache tu baada ya kudai kuwa kamwe utawala wa Kizayuni hautaondoa wanajeshi wake vamizi kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Mufti wa Al-Azhar: Kiwango cha dhulma ilichofikia kadhia ya Palestina hakimruhusu mtu kubaki njiapanda
Dec 24, 2025 02:39Taasisi kubwa zaidi ya Kiislamu nchini Misri ya Al-Azhar imesema, piganio la haki la Palestina limefikia kiwango cha dhulma na ukandamizwaji ambacho hakimruhusu mtu kubaki njiapanda na kudai kuwa haegemei upande wowote.
-
Mashinikizo ya Marekani kwa Pakistan kushiriki katika 'Kikosi cha Usalama cha Kimataifa' cha Gaza na kukataa Islamabad
Dec 24, 2025 02:38Licha ya mashinikizo ya Marekani kwa Pakistan ili kushiriki katika "Kikosi cha Usalama cha Kimataifa" cha Gaza, lakini Islamabad ilitangaza kwamba bado hakuna uamuzi uliochukuliwa nan chi hiyo wa kutuma wanajeshi katika Ukanda wa Gaza.
-
Abu Hatab wa Ghaza asimulia alivyoshiriki kuzika Wapalestina 18,000 waliouliwa kinyama na Israel
Dec 23, 2025 12:02Mzikamaiti Yousef Abu Hatab mkazi wa Ukanda wa Ghaza na mmoja wa mashuhuda wa moja ya majanga makubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Palestina, amesema ameshiriki kuzika karibu miili 18,000 ya Wapalestina waliouliwa shahidi wakati wa vita vya kinyama na vya mauaji ya kimbari yaliyofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel katika eneo hilo la Palestina.
-
HAMAS yaonya kuhusu mipango hatari ya Israel dhidi ya Baytul-Muqaddas
Dec 23, 2025 03:16Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeonya kuhusu mipango hatari ya Israel dhidi ya Baytul-Muqaddas na kuwafanya Wapalestina kuwa wakimbizi.
-
Uhaba wa dawa za matibabu Gaza umefikia viwango vya kutisha kufuatia mzingiro wa Israel
Dec 22, 2025 10:52Wizara ya Afya ya Gaza imetahadharisha kuhusu uhaba mkubwa na hatari zaidi wa dawa na vifaa vya matibabu. Imesema kuwa uhaba huo umelemaza uwezo wa eneo hilo wa kutoa huduma ya dharura ya matibabu na kuokoa maisha ya wagonjwa kufuatia kuendelea mzingiro wa Israel dhidi ya Gaza.
-
Arabi21: Utawala wa Kizayuni wa Israel unasambaza dawa za kulevya huko Gaza
Dec 22, 2025 10:20Chombo cha habari cha Arabi21 kimeripoti kuwa, ingawa jeshi la Israel limezuia kuingia bidhaa nyingi muhimu huko Gaza, ripoti zinaonyesha kuwa usafirishaji haramu wa dawa za kulevya katika eneo hilo unarahisishwa.