-
Netanyahu aiomba US iishinikize Misri ipunguze kujiimarisha kijeshi kwenye Peninsula ya Sinai
Sep 21, 2025 09:10Waziri Mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu ameiomba serikali ya Marekani iishinikize Misri ipunguze hatua za kujizatiti kijeshi katika eneo la Peninsula ya Sinai. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa jana Jumamosi na tovuti ya habari ya nchini Marekani ya Axios.
-
Islamabad: Mkataba wa kiulinzi kati ya Pakistan na Saudia unafanana wa Muungano wa kijeshi wa NATO
Sep 21, 2025 09:09Pakistan imesema, makubaliano ya hivi karibuni ya kiulinzi ambayo hayajawahi kushuhudiwa iliyosaini na Saudi Arabia yanalingana na yale yaliyopo katika Muungano wa kijeshi wa Magharibi wa nchi wanachama wa NATO.
-
Ripoti: Qatar inataka Israel iombe radhi ili kuanza tena juhudi za usuluhishi
Sep 21, 2025 06:51Qatar imesema kuwa Israel inapasa kuomba radhi kutokana na mashambulizi iliyotekeleza dhidi ya Doha. Imesema Israel inapasa kuomba radhi kama sharti ili kuweza kuanza tena mazungumzo ya amani ya kuhitimisha vita na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala huo katika Ukanda wa Gaza.
-
Je, Israel inakabiliwa na "Hatima ya Afrika Kusini"?
Sep 21, 2025 06:03Tovuti ya Kiingereza ya BBC katikati ya Septemba 2025 katika makala ya kina yenye kichwa cha habari kilichosomeka "Je, Israel Inakabiliwa na 'Hatima ya Afrika Kusini'?" Ilizungumzia suala la kujikariri uzoefu wa Afrika Kusini kwa utawala ghasibu wa Israel.
-
HAMAS: Wazayuni msidhani mtawaona tena mateka wenu
Sep 21, 2025 03:25Wanamapambano wa Al-Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, wamewahakikisha Wazayuni kwamba hawatowaona tena mateka wao hivyo wanapaswa kuwaaga kutokana na kuvamiwa Ghaza.
-
Ansarullah: Silaha mpya zimeingia kwenye uwanja wa vita; Jahannam inamsubiri Waziri wa Vita wa Israel
Sep 20, 2025 11:33Mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Ansarullah ya Yemen huku akipuuzilia mbali vitisho vya waziri wa vita wa utawala wa Kizayuni ametangaza kuingia kwa silaha mpya katika medani ya vita kati ya nchi ya Kiarabu na utawala haramu wa Israel pamoja na washirika wake wa Magharibi.
-
Je, upo uwezekano wa kutokea vita kati ya Uturuki na utawala wa Kizayuni?
Sep 20, 2025 09:49Mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya Qatar yamezidisha mivutano kati ya Uturuki na Israel na kuibua uwezekano wa kutokea makabiliano ya moja kwa moja kati ya Ankara na Tel Aviv.
-
Baada ya kuangamizwa askari 6 wa kizayuni, HAMAS yaionya Israel: Ghaza itageuka 'kaburi' la askari wenu
Sep 19, 2025 11:08Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imeuonya utawala wa kizayuni wa Israel kwamba hatua yake ya kuzidi kujiingiza ndani ya Mji wa Ghaza kutaugeuza mji huo kuwa "kaburi," la wanajeshi wa kizayuni baada ya sita miongoni mwao kuangamizwa na wanamuqawama wa Palestina katika matukio tofauti wakati wa jeshi la Israel likiwa linaendeleza mashambulizi makali na ya kinyama yanayolenga kulikalia kwa mabavu eneo lote la Ghaza.
-
UNIFIL yaitaka Israel ikomeshe mashambulizi, iondoke kikamilifu katika ardhi ya Lebanon
Sep 19, 2025 11:04Vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa kusini mwa Lebanon, UNIFIL imesema, shambulio la anga lililofanywa na jeshi la Israel jana usiku kusini mwa Lebanon ni ukiukaji wa wazi wa azimio nambari 1701 la Baraza la Usalama na tishio la moja kwa moja kwa hali tete ya uthabiti katika eneo hilo.
-
Kiongozi wa Ansarullah akosoa misimamo dhaifu ya nchi za Kiislamu na Kiarabu kuhusu jinai za Israel
Sep 19, 2025 06:55Akikosoa misimamo dhaifu ya nchi za Kiarabu na Kiislamu katika kikao cha hivi karibuni cha Doha dhidi ya hujuma ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Qatar, kiongozi wa Ansarullah amesisitiza kuwa, vitisho vya Israel haviko kwenye medani ya Palestina pekee bali vinalenga jamii nzima ya Kiislamu.