-
Hizbullah yaonesha nguvu zake, yaporomosha ndogo za maadui
May 31, 2025 22:51Licha ya Marekani kusimamia yenye vita kuusaidia utawala wa Kizayuni, na licha ya maadui hao kuwa na ndoto kwamba huenda Hizbullah ya Lebanon ikapoteza nguvu zake, lakini maadui hao wamejikuta wamo katikati ya vita tata mno ambavyo vinazidi kusambaratisha ndoto zao.
-
Kesi ya aina yake, mahakama Misri yamhukuru kiongozi mpya wa Syria
May 31, 2025 22:51Mahakama moja ya kiidara ya Misri, jana Jumamosi iliendesha kesi ya aina yake ambayo haijawahi kushuhudiwa dhidi ya Abu Muhammad al-Jolani, kiongozi wa utawala wa hivi sasa wa Syria akiwa hayupo mahakamani. Kesi hiyo inaweza kuwa hatua ya kwanza ya kuwawajibisha wahusika wa jinai za kivita nchini Syria.
-
Yemen yasema itageuza ndege za kivita za Israel kuwa chanzo cha dhihaka
May 31, 2025 03:46Serikali ya Yemen imetangaza kuwa inafanya juhudi za kuboresha mifumo yake ya ulinzi wa anga, huku ikikabiliana na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa Israel, na kuahidi kwamba karibuni ndege za kivita za Israel zitageuka kuwa chanzo cha dhihaka badala ya hofu.
-
Je, suala la watu wa Gaza ni kutambuliwa tu taifa la Palestina?
May 31, 2025 01:55Huku mashambulizi ya kikatili ya mara kwa mara katika Ukanda wa Gaza yakiingia katika mwezi wake wa ishirini na picha za kutisha za watoto waliouawa kinyama zikionyeshwa kila siku, nchi nne za Ulaya zimetoa taarifa ya pamoja ya kutaka uanachama kamili wa Palestina utambuliwe rasmi katika Umoja wa Mataifa.
-
Je, uhusiano wa serikali ya Julani na utawala wa Kizayuni unaelekea wapi?
May 31, 2025 00:10Vyanzo vya habari vimetangaza kuwa ujumbe unaohusiana na serikali ya mpito ya Syria umefanya mazungumzo ya siri na viongozi wa utawala haramu wa Israel.
-
Maandamano ya kuwaunga mkono Wagaza yafanyika Iran, Yemen
May 30, 2025 22:53Maelfu ya watu walimiminika barabarani na mitaani katika miji yote ya Iran baada ya Swala ya Ijumaa kushiriki maandamano ya kitaifa ya "Ijumaa ya Ghadhabu", wakitangaza uungaji mkono wao usioyumba kwa Wapalestina wa Gaza, na kulaani mauaji ya kimbari ya Israel katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Israel yamjibu Macron: Kutambuliwa Palestina kutasalia kwenye karatasi tu
May 30, 2025 22:52Waziri wa Vita wa Israel, Israel Katz amemsuta na kumkejeli Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ambaye alisema mapema jana kwamba, kutambuliwa kwa taifa la Palestina, kwa masharti, ni "wajibu wa kimaadili."
-
Ben Gvir alitaka jeshi la Israel litumie 'nguvu kamili' Gaza
May 30, 2025 22:52Waziri wa usalama wa ndani wa utawala wa Kizayuni wa Israel mwenye misimamo ya kufurutu ada, Itamar Ben Gvir ametoa wito wa kutumiwa "nguvu kamili" huko Gaza, baada ya madai ya uongo kwamba Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imepinga pendekezo jipya la Marekani kuhusu usitishaji vita.
-
Ireland yasisitiza Israel inatekeleza mauaji ya kimbari Gaza
May 30, 2025 04:04Katika mjadala mkali uliotikisa bunge la Ireland, naibu waziri mkuu Simon Harris, ametetea msimamo wa serikali kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unatekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Mkuu wa UNRWA: Waarabu wawape Wapalestina sehemu ndogo ya Matrilioni waliyompa Trump
May 30, 2025 04:03Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa Linalowahudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amezitaka nchi za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kutenga sehemu ndogo tu ya fedha zilizotajwa katika ‘makubaliano makubwa’ kati yao na Rais wa Marekani, Donald Trump, ili kusaidia wakimbizi wa Kipalestina wanaopambana kuendelea kuishi katika ardhi zao ambazo Israel imezikalia kwa mabavu na pia wale wanaoishi katika nchi jirani.