Asia Magharibi
  • Kesi ya aina yake, mahakama Misri yamhukuru kiongozi mpya wa Syria

    Kesi ya aina yake, mahakama Misri yamhukuru kiongozi mpya wa Syria

    May 31, 2025 22:51

    Mahakama moja ya kiidara ya Misri, jana Jumamosi iliendesha kesi ya aina yake ambayo haijawahi kushuhudiwa dhidi ya Abu Muhammad al-Jolani, kiongozi wa utawala wa hivi sasa wa Syria akiwa hayupo mahakamani. Kesi hiyo inaweza kuwa hatua ya kwanza ya kuwawajibisha wahusika wa jinai za kivita nchini Syria.

  • Yemen yasema itageuza ndege za kivita za Israel kuwa chanzo cha dhihaka

    Yemen yasema itageuza ndege za kivita za Israel kuwa chanzo cha dhihaka

    May 31, 2025 03:46

    Serikali ya Yemen imetangaza kuwa inafanya juhudi za kuboresha mifumo yake ya ulinzi wa anga, huku ikikabiliana na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa Israel, na kuahidi kwamba karibuni ndege za kivita za Israel zitageuka kuwa chanzo cha dhihaka badala ya hofu.

  • Je, suala la watu wa Gaza ni kutambuliwa tu taifa la Palestina?

    Je, suala la watu wa Gaza ni kutambuliwa tu taifa la Palestina?

    May 31, 2025 01:55

    Huku mashambulizi ya kikatili ya mara kwa mara katika Ukanda wa Gaza yakiingia katika mwezi wake wa ishirini na picha za kutisha za watoto waliouawa kinyama zikionyeshwa kila siku, nchi nne za Ulaya zimetoa taarifa ya pamoja ya kutaka uanachama kamili wa Palestina utambuliwe rasmi katika Umoja wa Mataifa.

  • Je, uhusiano wa serikali ya Julani na utawala wa Kizayuni unaelekea wapi?

    Je, uhusiano wa serikali ya Julani na utawala wa Kizayuni unaelekea wapi?

    May 31, 2025 00:10

    Vyanzo vya habari vimetangaza kuwa ujumbe unaohusiana na serikali ya mpito ya Syria umefanya mazungumzo ya siri na viongozi wa utawala haramu wa Israel.

  • Maandamano ya kuwaunga mkono Wagaza yafanyika Iran, Yemen

    Maandamano ya kuwaunga mkono Wagaza yafanyika Iran, Yemen

    May 30, 2025 22:53

    Maelfu ya watu walimiminika barabarani na mitaani katika miji yote ya Iran baada ya Swala ya Ijumaa kushiriki maandamano ya kitaifa ya "Ijumaa ya Ghadhabu", wakitangaza uungaji mkono wao usioyumba kwa Wapalestina wa Gaza, na kulaani mauaji ya kimbari ya Israel katika eneo hilo lililozingirwa.

  • Israel yamjibu Macron: Kutambuliwa Palestina kutasalia kwenye karatasi tu

    Israel yamjibu Macron: Kutambuliwa Palestina kutasalia kwenye karatasi tu

    May 30, 2025 22:52

    Waziri wa Vita wa Israel, Israel Katz amemsuta na kumkejeli Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ambaye alisema mapema jana kwamba, kutambuliwa kwa taifa la Palestina, kwa masharti, ni "wajibu wa kimaadili."

  • Ben Gvir alitaka jeshi la Israel litumie 'nguvu kamili' Gaza

    Ben Gvir alitaka jeshi la Israel litumie 'nguvu kamili' Gaza

    May 30, 2025 22:52

    Waziri wa usalama wa ndani wa utawala wa Kizayuni wa Israel mwenye misimamo ya kufurutu ada, Itamar Ben Gvir ametoa wito wa kutumiwa "nguvu kamili" huko Gaza, baada ya madai ya uongo kwamba Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imepinga pendekezo jipya la Marekani kuhusu usitishaji vita.

  • Ireland yasisitiza Israel inatekeleza mauaji ya kimbari Gaza

    Ireland yasisitiza Israel inatekeleza mauaji ya kimbari Gaza

    May 30, 2025 04:04

    Katika mjadala mkali uliotikisa bunge la Ireland, naibu waziri mkuu Simon Harris, ametetea msimamo wa serikali kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unatekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Gaza.

  • Mkuu wa UNRWA: Waarabu wawape Wapalestina sehemu ndogo ya Matrilioni waliyompa Trump

    Mkuu wa UNRWA: Waarabu wawape Wapalestina sehemu ndogo ya Matrilioni waliyompa Trump

    May 30, 2025 04:03

    Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa Linalowahudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amezitaka nchi za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kutenga sehemu ndogo tu ya fedha zilizotajwa katika ‘makubaliano makubwa’ kati yao na Rais wa Marekani, Donald Trump, ili kusaidia wakimbizi wa Kipalestina wanaopambana kuendelea kuishi katika ardhi zao ambazo Israel imezikalia kwa mabavu  na pia wale wanaoishi katika nchi jirani.