-
Hamas; kuuawa shahidi Barhoum; jinai nyingine katika rekodi nyeusi ya utawala wa Kizayuni
Mar 24, 2025 04:37Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa taarifa na kutoa mkono wa pole kufuatia kuuawa shahidi Esmail Barhoum mwakilishi wa Ofisi ya Kisiasa ya harakati hiyo.
-
Mchambuzi: Kurukia vita baada ya vita ni 'muhimu' kwa Netanyahu kubaki madarakani
Mar 23, 2025 23:01Elijah Magnier, mchambuzi mashuhuri wa masuala ya kijeshi amesema, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu anafanya juu chini ili aweze kusalia madarakani kwa angalau miaka miwili mingine; na hiyo ndiyo sababu ya "kurukia vita baada ya vita".
-
Hamas: Mauaji ya Wapalestina akiwemo Mbunge yataimarisha Muqawama
Mar 23, 2025 07:29Jeshi la Israel limefanya mashambulizi mapya ya kutisha ya anga katika Ukanda wa Gaza na kuua shahidi watu wasiopungua 40, akiwemo Salah al-Bardawil, Mbunge wa Palestina na Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas.
-
Israel yapigwa na makombora kutoka Yemen, ving'ora vyahanikiza
Mar 23, 2025 07:21Vikosi vya Ulinzi vya Yemen vimevurumisha makombora kuelekea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel, na kuwatia kiwewe na hofu Wazayuni; huku safari za ndege zikisimamishwa Tel Aviv.
-
Hamas: Muqawama ni chaguo la kimkakati la ukombozi wa Palestina
Mar 23, 2025 03:03Katika kumbukumbu ya mwaka wa 21 wa kuuawa shahidi Sheikh Ahmad Yassin, Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kwa kusema: "Tunashikamana na njia ya Sheikh Ahmad Yassin, tunalinda ardhi na matukufu yetu, na tuna imani thabiti kwamba Muqawama ni chaguo la kistratijia la kujikomboa na kupata uhuru wetu."
-
Hizbullah yapinga madai ya kuhusika na shambulio la maroketi
Mar 22, 2025 23:18Baada ya utawala wa Israel kudai kwamba maroketi 5 yalirushwa kuelekea katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu jana Jumamosi, Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imekanusha kuhusika kivyovyote na shambulio hilo.
-
'Kuripua Israel hospitali pekee ya matibabu ya saratani Ghaza ni ugaidi wa wazi wa kiserikali'
Mar 22, 2025 07:47Kitendo cha jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel cha kuiripua na kuibomoa kikamilifu hospitali pekee ya matibabu ya maradhi ya saratani katika Ukanda wa Ghaza kimelaaniwa vikali kimataifa na kuelezewa kuwa ni kilelezo cha wazi cha 'ugaidi wa kimfumo wa kiserikali' wa utawala huo haramu.
-
'Uwanja wa ndege wa Ben Gurion hautakuwa salama mpaka uchokozi dhidi ya Ghaza utakapokoma'
Mar 22, 2025 07:41Vikosi vya Ulinzi vya Yemen (YAF) vimetangaza kuwa Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion wa Israel sasa hauko salama kwa usafiri wa anga na utaendelea kuwa hivyo hadi uchokozi wa utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Ghaza utakapokomeshwa na vizuizi vya misaada lilivyoekewa eneo hilo la Palestina vitakapoondolewa.
-
Hamas yatoa wito kwa vyombo vya habari kupinga propaganda chafu za Israel
Mar 22, 2025 03:49Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa wito kwa Waarabu na Wapalestina kushiriki katika mapambano ya vyombo vya habari ili kukabiliana na propaganda na vita vya kisaikolojia vya Israel vyenye lengo la kuvunja irada na azma ya watu wa Palestina.
-
New York Times: Marekani haitaweza kuishinda Yemen
Mar 22, 2025 03:30New York Times limeandika kuwa Marekani haitaweza kutoa pigo kwa Yemen katika mashambulizi yake ya kichokozi dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.