-
Hamas yasisitiza kutekelezwa usitishaji vita kamili
Mar 03, 2025 02:29Mahmoud al Mardawi mmoja wa viongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ameeleza kuwa abadan harakati hiyo haitakubali kuongezwa muda wa marhala ya kwanza ya makubaliano ya usitishaji vita.
-
Misri: Amani haitapatikana pasi na kuundwa nchi huru ya Palestina
Mar 02, 2025 22:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri amesema kuwa, hakutakuwa na usalama katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) bila ya kuasisiwa taifa la Palestina.
-
Mamlaka ya Ndani ya Palestina yataka walimwengu waishinikize Israel
Mar 02, 2025 22:53Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina imeonya juu ya matokeo mabaya ya kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza na kuitaka jamii ya kimataifa kuulazimisha utawala wa Kizayuni utekeleze majukumu yake ya kibinadamu.
-
Yemen yaitaka Riyadh ijifunze kutokana na hatma ya Zelensky
Mar 02, 2025 08:55Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amewaonya maafisa wa Saudi Arabia na kuwataka wapate somo na ibra kutokana na jinsi Marekani ilivyomfanyia Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, na kuwaonya dhidi ya kuitegemea kipofu Washington.
-
Misri yatayarisha mpango mbadala wa kukabiliana na wa Trump huko Gaza
Mar 02, 2025 03:58Vyanzo vya habari vya Misri vimeripoti kuwa Cairo imetupilia mbali mpango wa Rais wa Marekani, Donald Trump kuhusu eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina na sasa imetayari mpango mbadala.
-
HAMAS: Hadi sasa hakuna makubaliano yoyote kuhusu awamu ya pili ya mazungumzo ya Ghaza
Mar 01, 2025 23:00Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetangaza kuwa, mazungumzo baina yake na utawala wa Kizayauni wa Israel yamesimama na hakuna maendeleo yoyote ya maana kuhusu awamu ya pili ya mazungumzo ya kusimamisha vita huko Ghaza.
-
Ansarullah: Israel inatumia uungaji mkono wa US kukiuka makubaliano
Mar 01, 2025 03:43Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema Yemen inafuatilia kwa karibu utekelezwaji wa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza na kuongeza kuwa, inashuhudia namna "adui Mzayuni" anakwepa kutekeleza majukumu yake.
-
GCC yataka kuchukuliwa "hatua madhubuti" dhidi ya mashambulizi ya Israel nchini Syria
Mar 01, 2025 01:04Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC) limetoa mwito wa kuchukuliwa "hatua madhubuti" ili kukomesha mashambulizi ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Syria.
-
UN: Zaidi ya Wanafunzi 100,000 Wamerejea Shuleni Ukanda wa Gaza
Mar 01, 2025 00:19Umoja wa Mataifa umeripoti kuwa zaidi ya wanafunzi 100,000 wamejiandikisha mashuleni katika Ukanda wa Gaza baada ya mwaka mpya wa masomo kuanza Februari 23, na kuashiria kurudi mashuleni wanafunzi baada ya muda mrefu wa kusimamishwa masomo kutokana na mauaji ya kimbari ya utawala wa Kiziayuni wa Israel dhidi ya watu wa eneo hilo la Palestina.
-
Euro-Med Human Rights Monitor: Israel inatumia mateso kama silaha
Mar 01, 2025 00:19Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Mediterranean Human Rights Monitor limeeleza mshtuko wake mkubwa kutokana na hali mbaya ya kiafya na kisaikolojia ya mahabusi wa Kipalestina walioachiwa huru katika awamu ya saba ya utekelezaji wa makubaliano ya kubadilishana mateka kati ya Hamas na utawala haramu wa Israel.