-
Israel yakiri rasmi kushindwa katika oparesheni ya Kimbunga cha al Aqsa
Feb 28, 2025 04:01Jeshi la utawala wa Kizayuni limekiri kuwa, katika mashambulizi ya Oktoba 7 mwaka 2023 lilishindwa kuwahami walowezi wa utawala huo wanaoishi katika maeneo jirani na Gaza; na kwamba lilifeli katika masaa ya awali mkabala wa mashambulizi ya Hamas.
-
UN: Israel inakanyaga haki za binadamu Gaza, Ukingo wa Magharibi
Feb 27, 2025 07:31Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema utawala wa Israel umekuwa ukipuuza usio na kifani haki za binadamu" katika Ukanda wa Gaza, na kuitaja hali ya kibinadamu katika eneo hilo lililozingirwa kuwa "janga."
-
Israel inakusudia nini kwa mashambulizi yake ya mara kwa mara dhidi ya Syria?
Feb 27, 2025 06:28Utawala wa Kizayuni wa Israel Jumatano Februari 26 ulishambulia mara kadhaa maeneo mbalimbali ya Syria na kuua na kujeruhi watu kadhaa.
-
UNRWA: Ukingo wa Magharibi ni 'uwanja wa vita', watu 50 wameuawa
Feb 27, 2025 04:39Wiki kadhaa za uvamizi wa kijeshi wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu zimegeuza jamii za Wapalestina kuwa “uwanja wa vita” na kuwaacha watu 40,000 bila makazi, mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yameonya jana Februari 26, 2025.
-
Makumi ya mateka wa Kipalestina waachiliwa huru, Hamas yakabidhi maiti
Feb 26, 2025 23:48Makumi ya mateka wa Kipalestina wanaoishi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na mji wa Quds wameachiliwa huru mapema leo Alkhamisi alfajiri ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya kubadilishana mateka kati ya Muqawama na Israel, na wamepokewa kwa shangwe kubwa Ramallah.
-
Kadi nyingine nyekundu yatolewa kwa Israel; mara hii ni nchini Malaysia
Feb 26, 2025 23:47Mashabiki wa soka wa Malaysia wamejiunga na kampeni ya 'Show Israel Red Card' yaani "Ionyeshe Israel Kadi Nyekundu" katika uuwanja wa soka ili kuonyesha uungaji mkono wao kwa Palestina.
-
HAMAS: Mwafaka umefikiwa kuhusu Wapalestina 620 ambao Israel ilichelewesha kuwaachia huru
Feb 26, 2025 09:28Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, ujumbe wake umehitimisha ziara yake katika mji mkuu wa Misri Cairo na umefikia makubaliano na wapatanishi ya kutatuliwa ucheleweshaji uliofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuwaachilia huru wafungwa Wapalestina ambao ilipasa waachiliwe siku ya Jumamosi iliyopita kama sehemu ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya pande hizo mbili.
-
Waislamu Uhispania wahuisha mila ya karne 5 zilizopita ya Andalusia ya kwenda Hija kwa farasi
Feb 26, 2025 08:13Marafiki watatu kutoka Uhispania wameamua kutumia usafiri wa farasi katika safari yao ya kuelekea Makka, Saudi Arabia kwa ajili ya kutekeleza ibada ya Hija yao kwa madhumuni ya kuhuisha mila na desturi ya tangu miaka 500 nyuma wa Waislamu wa Andalusia ya wakati huo.
-
Misri yakataa pendekezo la Wazayuni la kuitawala Gaza kwa miaka 8
Feb 26, 2025 03:10Cairo imekataa pendekezo la maafisa wa utawala za Kizayuni wa Isarel wanaotaka serikali ya Misri isimamia mamlaka ya Ukanda wa Gaza kwa miaka 8 hadi 15.
-
Mkutano wa Mazungumzo ya Syrian waitaka Israel kuondoa kwenye ardhi ya nchi hiyo
Feb 26, 2025 03:08Mkutano wa Kitaifa wa Mazungumzo ya Syria umeitaka Israel kuondoa katika ardhi ya nchi hiyo, na kusisitiza udharura wa kulindwa umoja wa ardhi ya Syria na kupinga kugawanywa nchi hiyo.