-
Palestina yatoa onyo kali kwa utawala wa Kizayuni kuhusu kitongoji cha al-Bastan
Nov 16, 2024 03:51Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imetahadharisha kuhuusu uharibifu huo kamili wa kitongoji cha al-Bastan cha Quds Tukufu inayokaliwa kwa mabavu na utawala pandikizi wa Israel na hasa baada ya Wapalestina 1,500 kulazimishwa kuyahama makaazi yao.
-
Kiongozi mmoja wa HAMAS auawa katika jela za Israel
Nov 15, 2024 23:25Mmmoja wa viongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS, Samih Aliwi, aliuawa shahidi jana Ijumaa, Novemba 15, 2024 ikiwa ni siku sita baada ya kuhamishwa kutoka gereza la Ramla na kupelekwa katika hospitali ya Assaf Harofeh. Taarifa nyingine zinasema aliuawa shahidi tangu siku sita nyuma lakini utawala wa Kizayuni ulikuwa unaficha kifo chake.
-
Haaretz: Zaidi ya Wazayuni 10,000 wameshakimbilia Canada mwaka huu kutokea Israel
Nov 15, 2024 23:24Idadi ya walowezi wa Kizayuni wanaokimbilia Canada imeongezeka kwa kasi kutokana na vipigo inavyopata Israel kutoka kwa wanamapambano wa Lebanon na Palestina.
-
Juhudi za Marekani za kuhalalisha jinai za Israel na kuendelea kuitumia silaha za mauaji ya umati
Nov 15, 2024 23:20Vedant Patel, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ametoa matamshi ambayo yanaonyesha kuwa Marekani haiko tayari kwa vyo vyote vile kumuwajibisha mshirika wake wa jinai za kivita, yaani utawala haramu wa Israel, na kuwa inatosheka tu kwa kutoa madai matupu yasiyo na maana kuhusiana na suala zima la haki za binadamu.
-
Njama mpya ya Israel ya unyakuzi wa ardhi ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan
Nov 15, 2024 05:52Bezalel Smotrich, Waziri wa Fedha wa utawala wa Kizayuni ametoa matamshi kuhusiana na ushindi wa Donald Trump katika uchaguzi wa rais wa Marekani na kusema kuwa, mwaka 2025 utakuwa mwaka wa utawala huo ghasibu kunyakua na kupanua udhibiti wake katika ardhi ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
UNRWA: Kizazi kizima cha Wapalestina kitanyimwa haki ya elimu Gaza
Nov 15, 2024 04:14Philippe Lazzarini, Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), ameonya kuwa, kizazi kizima cha Wapalestina huko Gaza "kitanyimwa haki ya elimu" ikiwa asasi hiyo katika Ukanda huo itafutwa chini ya sheria mpya ya Israel.
-
Borrell ataka Umoja wa Ulaya kusisitiza mazungumzo ya kisiasa na Israel
Nov 15, 2024 00:25Josep Borrell Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amependekeza kuwa, umoja huo unapaswa kusitisha mazungumzo yake ya kisiasa na Israel kutokana na utawala huo kuendelea kufanya mauaji na jinai huko Gaza na Lebanon.
-
Human Rights Watch: Vitendo vya Israel Gaza ni jinai dhidi ya binadamu
Nov 14, 2024 08:20Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limetangaza kuwa, amri ya kuhama ilioyotolewa na Israel katika eneo la kaskazini mwa Ukanda wa Gaza imefanywa kkwamadhumuni ya kuwatesa, kulazimishwa Wapalestina kuwa wakimbizi na kusambaa raia wa Palestina.
-
HAMAS: Andamaneni na zidini kuzizingira balozi za utawala wa Kizayuni na wanaouunga mkono
Nov 14, 2024 03:44Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa wito wa kuzidishwa harakati za umma katika ngazi ya kimataifa katika kulaani mwendelezo wa jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza na kuliunga mkono taifa la Muqawama la Palestina.
-
Sheikh Naim Qassem: Wapiganaji wa Hizbullah ni fakhari inayotetemesha mihimili ya Uzayuni
Nov 14, 2024 03:35Katibu Mkuu wa Hizbullah Sheikh Naim Qassem amewaandikia barua wapiganaji wa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu ya Lebanon, akiwapongeza kwa mapambano ya kujivunia wanayoyaendeleza katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel na waungaji mkono wake.