-
Utawala wa Kizayuni umewatia nguvuni mamia ya wafanyakazi wa Kipalestina
May 01, 2024 23:06Vyanzo vya habari vya Palestina vimeripoti kuwa Wazayuni maghasibu wamewatia mbaroni zaidi ya wafanyakazi elfu tano wa Kipalestina katika mwaka huu wa 2024 huku hali za kiafya za raia hao wa Kipalestina zikitajwa kuwa mbaya.
-
Jitihada za China za kuleta maridhiano ya kitaifa Palestina
May 01, 2024 23:05Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China ametangaza kuwa kufuatia mkutano wa wawakilishi wa harakati za Palestina za Hamas na Fat'h mjini Beijing, pande mbili zimefikia makubaliano ya kujadili maridhiano ya kitaifa huko Palestina.
-
Congress ya Marekani inatumika kama ngao ya kumlinda Netanyahu
May 01, 2024 08:10Katika hali ambayo Baraza la Mawaziri la utawala wa Kizayuni lina wasiwasi mkubwa kuhusiana na uwezekano wa kutolewa waranti wa kukamatwa Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu na maafisa wengine wa utawala wa Kizayuni, tovuti ya habari ya Axios imeripoti kwamba wajumbe wa Congress wameionya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC na kuitaka isitoe vibali vya kutiwa nguvuni maafisa wa utawala wa Israel.
-
Miili 10,000 iliyozikwa chini ya vifusi vya Gaza, inaoza na kueneza magonjwa
May 01, 2024 00:33Shirika la Ulinzi wa kiraia la Gaza limeonya kuhusu maafa ya kiafya yanayokuja katika Ukanda uliozingirwa kutokana na kuoza maiti zilizo chini ya vifusi vya majengo yaliyoharibiwa na mashambulizi ya mabomu ya utawala katili wa Israel.
-
Kukaribia muda wa kutolewa hukumu ya mahakama mbili za kimataifa dhidi ya utawala wa Kizayuni
Apr 30, 2024 22:53Sambamba na kuongezeka uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ kutoa hukumu ya kukamatwa maafisa kadhaa wa utawala wa Kizayuni kwa tuhuma za kufanya jinai za kivita huko Gaza, gazeti la Times lilimeandika kuwa, kuna uwezekano pia kwamba Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC inajiandaa kutoa hati ya kukamatwa Netanyahu na maafisa wengine wa ngazi za juu wa Israel akiwemo Waziri wa Vita, Mkuu wa Majeshi na baadhi ya maafisa wa usalama wa utawala huo kwa kuhusika na vita hivyo.
-
Ujumbe wa Hamas umeondoka Cairo kwa ajili ya mashauriano zaidi
Apr 30, 2024 07:42Ujumbe wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) umeondoka Cairo, mji mkuu wa Misri ili kufanya mashauriano zaidi kuhusu pendekezo jipya lililotolewa kwa ajili ya kubadilishana mateka.
-
Vituo vya utafiti vya Ulaya vyaiunga mkono Palestina na kuiwekea vikwazo Israel
Apr 30, 2024 07:41Vituo vya utafiti barani Ulaya vimeuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni na kuunga mkono malengo ya Palestina. Viituo hivyo vya utafiti vya Ulaya pia vimelaani jinai za utawala huo unaotekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Gaza.
-
Balozi zote za Israel zawekwa kwenye hali ya tahadhari kuhofia waranti wa ICC wa jinai za vita vya Ghaza
Apr 29, 2024 23:17Wizara ya Mambo ya Nje ya utawala wa Kizayuni wa Israel imeziagiza balozi zake duniani kote kuwa tayari kwa madhara yanayoweza kutokea iwapo Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) itatoa waranti wa kukamatwa maafisa wa utawala huo kwa uhalifu wa kivita na ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
-
Wapalestina zaidi ya 8,500 wametiwa nguvuni Ukingo wa Magharibi tangu Oktoba 7 hadi sasa
Apr 29, 2024 23:16Jumuiya ya kushughulikia mateka wa Kipalestina imetangaza katika ripoti yake kwamba utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel umewatia nguvuni Wapalestina 8,505 katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan tangu tarehe 7 Oktoba 2023 mara baada ya kutekelezwa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
Kuharibiwa Gaza; Jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya kizazi cha sasa na kijacho
Apr 29, 2024 23:14Mwezi wa saba wa vita unamalizika tangu utawala wa Kizayuni uanzishe vita na mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza, huku mashambulizi ya kila siku ya utawala huo yakisababisha maafa na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya mji na afya katika ukanda huo.