-
Makundi ya ukombozi ya Palestina: Hatutaruhusu jeshi lolote la kimataifa au la Kiarabu kuingia Gaza
Mar 31, 2024 23:52Makundi ya ukombozi ya Wapalestina yametangaza kuwa jeshi lolote la kimataifa au la Kiarabu litakaloingia katika Ukanda wa Gaza halikubaliki na litatambuliwa kuwa ni jeshi vamizi.
-
Wapalestina zaidi ya 400 wameuawa shahidi katika hospitali ya al Shifa iliyozingirwa
Mar 31, 2024 08:03Vyombo vya habari kutoka Ukanda wa Gaza vimetangaza kuwa Wapalestina zaidi ya 400 wameuawa katika mashambulizi ya jeshi la Israel katika Hospitali ya al Shifa ambayo inaendelea kuzingirwa na utawala wa Kizayuni kwa siku ya 13 sasa.
-
Wapiganaji wa Muqawama Iraq washambulia kituo 'muhimu' cha kijeshi cha Israel
Mar 31, 2024 03:06Kundi la Wapiganaji wa Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) Iraq limetangaza kushambulia kituo "muhimu" cha kijeshi cha utawala wa Israel kilichoko kaskazini mwa maeneo yanayokaliwa kwa mabavu katika kuendelea kuwaunga mkono Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, ambao wanastahimili vita vya mauaji ya halaiki ya Israel.
-
Licha ya kuikosoa Israel hadharani, Biden ameidhinisha kwa siri silaha mpya za kuwaulia Wapalestina
Mar 30, 2024 22:48Rais Joe Biden wa Marekani hivi karibuni ameidhinisha kwa siri kupatiwa utawala wa Kizayuni wa Israel silaha mpya za kivita zenye gharama ya mabilioni ya dola zikiwemo aina za kisasa za mabomu na ndege za kivita.
-
61% ya Waisraeli hawaamini kama vita vya Ghaza vitamalizika kwa kusambaratishwa HAMAS
Mar 30, 2024 22:46Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa Palestina inayokaliwa kwa mabavu iliyopandikizwa jina bandia la Israel yanaonyesha kuwa asilimia 61 ya Wazayuni hawaamini kama vita vya Ghaza vitamalizika kwa "kusambaratishwa harakati ya Hamas".
-
Kwa mnasaba wa "Siku ya Ardhi", HAMAS yautolea wito Umma wa Kiislamu kuikomboa Palestina
Mar 30, 2024 22:45Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa taarifa maalumu kwa mnasaba wa "Siku ya Ardhi" ikisisitiza kuwa kuikomboa ardhi ya Palestina na matakatifu yake ni jukumu la Umma wote wa Kiislamu.
-
Saudia yaongoza katika kutupa chakula (israfu) duniani
Mar 30, 2024 07:58Saudi Arabia inaongoza kwa israfu au kutupa chakula duniani huku mamilioni ya watu wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula wakiwemo Wapalestina wa Gaza wanaokabiliwa na hujuma ya Israel.
-
Jeshi la Israel lakiri kuwaua na kuwazika Wapalestina wawili kwa tingatinga
Mar 30, 2024 02:34Televisheni ya CNN ya Marekani imenukuu taarifa ya jeshi la Israel likikiri kuwaua Wapalestina wawili na kufukia miili yao kwa kutumia tingatinga, baada ya televisheni ya Al Jazeera ya Qatar kurusha hewani kipande cha video kinachoonyesha undani wa mauaji hayo.
-
Hizbullah yajibu mapigo, yashambulia vitongoji vya walowezi wa Kizayuni
Mar 29, 2024 22:58Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imefanya mashambulizi kadhaa dhidi ya vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na kambi kadhaa za Israel kaskazini mwa maeneo yaliyokaliwa kwa mabavu na utawala huo ghasibu mwaka 1948, kama sehemu ya awamu nyingine ya operesheni za kulipiza kisasi dhidi ya utawala huo na kuwatetea watu wa Gaza.
-
HAMAS: Misimamo ya Israel imekwamisha mazungumzo ya Doha
Mar 29, 2024 08:29Mmoja wa viongozi waandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema mazungumzo ya kusimamisha vita katika Ukanda wa Gaza yamegonga mwamba huko Doha, mji mkuu wa Qatar kutokana na misimamo isiyoeleweka ya utawala haramu wa Israel.