-
Humanity and Inclusion: Kuondoa mada za milipuko Ukanda wa Gaza kutachukua miaka 30
Oct 24, 2025 04:15Afisa wa taasisi ya Humanity and Inclusion amesema kazi ya kukusanya silaha ambazo hazijalipuka katika Ukanda wa Gaza inaweza kuchukua kipindi cha miaka 20 hadi 30, akilitaja eneo hilo kama "uwanja wazi wa mabomu."
-
WFP: Kiwango cha chakula kinachoingizwa Gaza ni kidogo mno
Oct 24, 2025 00:49Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula (WFP) limetangaza kuwa, kiwango cha chakula kinachoingia Gaza bado kiko chini sana ya lengo la tani 2,000 kwa siku, likitoa wito kwa utawala wa Kizayuni wa Israel kufungua vituo zaidi vya mipakani.
-
Mashabiki wa Galatasaray wapamba majukwaa kwa bendera ya Palestina, wataka kukomeshwa mauaji ya kimbari Gaza
Oct 24, 2025 00:49Mashabiki wa Galatasaray wa Uturuki wakitangaza himaya na uungaji mkono wao kwa wananchi wa Palestina walipamba majukwaa ya uwanja wa Rams Park kwa bendera ya Palestina na kutoa wito wa kukomeshwa mauaji ya kimbari huko Gaza.
-
Ni mambo gani yameifanya Israel itengwe kisiasa na kijamii kiasi hiki?
Oct 23, 2025 23:02Israel inakabiliwa na mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa katika historia yake. Yair Lapid, kiongozi wa upinzani wa utawala wa Kizayuni, alikiri hivi karibuni katika kikao cha kamati moja ya Knesset kwamba Israel hivi sasa iko katika mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa katika historia yake.
-
Hamas: Miswada haramu ya unyakuzi wa Ukingo wa Magharibi inafichua sura mbaya ya ukoloni wa Israel
Oct 23, 2025 07:49Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imelaani pendekezo la awali la Bunge la Israel (Knesset) la kunyakua eneo la Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, na kusema kuwa hatua hiyo inaakisi sura mbaya ya ukoloni wa utawala wa Tel Aviv katika ardhi ya Palestina.
-
Kwa nini Marekani inashinikiza kupokonywa silaha makundi ya muqawama ya Iraq?
Oct 23, 2025 04:23Tommy Piggott, Naibu Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani alisema siku ya Jumanne kwamba Marco Rubio Waziri wa Mambo ya Nje, katika mazungumzo yake na Mohammad Shia Al-Sudani, Waziri Mkuu wa Iraq, ametoa wito wa kupokonywa silaha makundi ya muqawama ya nchi hiyo akidai kuwa ni tishio kwa maslahi ya Washington na Baghdad.
-
Ripota Maalumu wa UN atoa ripoti mpya kuhusu mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza
Oct 23, 2025 02:51Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ametoa ripoti yake mpya kuhusu mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni Israel katika Ukanda wa Gaza, na kutoa maelezo ya kina kuhusu ushiriki wa kimataifa katika ukatili wa Tel Aviv.
-
Lazzarini: Kujenga upya shule za Gaza ndio kipaumbele
Oct 22, 2025 23:10Philippe Lazzarini, Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), amesema kuwa, kurejesha haki ya elimu kwa watoto wa Gaza ni jambo la dharura na muhimu zaidi baada ya kusitishwa mapigano.
-
Malori ya misaada 986 tu kati ya 6,600 yameingia Gaza tangu kufikiwa makubaliano ya kusitisha vita
Oct 22, 2025 09:39Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Serikali ya Gaza imeripoti kuwa ni malori 986 pekee ya misaada yaliyoingia katika eneo hilo linalozingirwa tangu kusitishwa kwa mapigano kati ya Harakati ya Mapambano ya Palestina (Hamas) na utawala wa Israel tarehe 10 mwezi huu.
-
Utaratibu Mpya wa Kiuchumi wa Kikanda; Nafasi ya kimkakati ya Iran katika Ushirikiano na Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia
Oct 22, 2025 09:11Mkutano wa Nne wa Kistratijia wa "Iran na Eurasia; Biashara, Diplomasia na Utaratibu Mpya wa Kikanda," umefanyika leo katika Kituo cha Mikutano cha Shirika la Utangazaji la Sauti na Televisheni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Tehran.