-
Je, Ulaya imetumia kadi yake ya mwisho dhidi ya Iran?
Aug 30, 2025 08:50Jarida la Foreign Policy limeashiria katika makala yake kuhusu hatua ya Ufaransa, Ujerumani na Uingereza ya kuanzisha mchakato wa kuanzisha utaratibu wa kurejesha vikwazo vya Baraza la Usalama dhidi ya Iran (snapback) kutokana na mpango wake wa nyuklia.
-
US yawazuia viongozi wa PLO na PA kuhudhuria UNGA huku nchi zikijiandaa kuitambua Palestina
Aug 30, 2025 02:23Marekani imebatilisha rasmi viza za maafisa wa Palestina, na kuwazuia kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNGA) utakaofanyika mwezi ujao wa Septemba mjini New York, makao makuu ya umoja huo, hatua ambayo inakuja wakati nchi kadhaa za Magharibi zinajiandaa kuitambua nchi ya Palestina.
-
Sasa Uturuki yakata mahusiano yote ya kibiashara na Israel, yafunga anga, bandari kwa sababu ya Ghaza
Aug 30, 2025 02:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan ametangaza kuwa nchi hiyo inafunga anga na bandari zake kwa ndege na meli za utawala wa kizayuni wa Israel, na kukata kikamilifu mahusiano yote ya kiuchumi na kibiashara na utawala huo kutokana na vita vyake vya mauaji ya kimbari unavyoendeleza huko Ghaza, Palestina.
-
Kansela wa Ujerumani azitaka nchi za Ulaya zijiandae kwa vita vya muda mrefu vya Ukraine
Aug 30, 2025 02:22Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz amesema nchi za Ulaya zinapaswa zijiweke tayari kwa vita vya muda mrefu nchini Ukraine kutokana na kile alichokiita kusitasita kwa Russia kushiriki katika mazungumzo.
-
Malaysia yataka utawala wa kizayuni wa Israel utimuliwe uanachama Umoja wa Mataifa
Aug 30, 2025 00:24Malaysia imetoa mwito wa kusimamishwa uanachama wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Umoja wa Mataifa kutokana na jinai zake katika Ukanda wa Gaza.
-
Kwa nini doria ya kwanza ya pamoja ya nyambizi za Russia na China ni muhimu?
Aug 29, 2025 23:01Doria ya pamoja ya nyambizi za Russia na China imefanyika kwa mara ya kwanza katika eneo la Asia-Pasifiki.
-
Kwa nini zaidi ya wanadiplomasia 200 wa Ulaya wanaukosoa Umoja wa Ulaya kwa kutochukua hatua kuhusu vita vya Gaza?
Aug 29, 2025 06:33Idadi kubwa ya wanadiplomasia wakuu wa zamani wa Ulaya wametaka Umoja wa Ulaya au nchi wanachama wachukue hatua za haraka kuhusiana na vita vya utawala wa Kizayuni huko Gaza na hatua zake zilizo kinyume cha sheria katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Guterres: Hali mbaya ya Ghaza hailingani na hali yoyote katika zama za hivi karibuni
Aug 29, 2025 04:06Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa indhari kali ya kuongezeka vifo vya raia huko Ghaza, akiielezea hali ya eneo hilo la Palestina lililowekewa mzingiro na Israel kuwa "haijafanana na yoyote katika zama za hivi karibuni."
-
Trump afufua tena simulizi za 'Riviera' ya Ghaza katika mkutano na Blair na Kushner
Aug 29, 2025 04:03Rais Donald Trump wa Marekani amefufua tena mpango wake wa kuwahamisha Wapalestina wote katika Ukanda wa Ghaza na kuligeuza eneo hilo la ardhi ya Palestina kuwa sehemu ya starehe na burudani alipokutana ikulu ya White House na mkwewe Jared Kushner na waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair ambao wote wawili wanahusishwa na uandaaji wa mpango huo unaotajwa kuwa ni wa kikoloni.
-
Russia: Tumepiga Ukraine kwa makombora ya hypersonic
Aug 28, 2025 22:53Russia imetangaza habari ya kutekeleza mashambulizi ya masafa marefu dhidi ya shabaha za jeshi la Ukraine, kwa kutumia aina mbalimbali za silaha, yakiwemo makombora ya hypersonic aina ya Kinzhal.