-
Kwa nini Marekani inafanya njama za kuidhibiti Venezuela?
Dec 02, 2025 03:45Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amesisitiza kuwa, nchi yake itaendelea kulinda rasilimali zake kwa nguvu zote mbele ya tamaa ya kuchupa mipaka ya Marekani.
-
Papa Leo: Kuundwa taifa la Palestina ndio suluhisho pekee la amani
Dec 02, 2025 03:25Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, ambaye alikuwa safarini huko Beirut nchini Lebanon, amesema kwamba kuundwa taifa la Palestina ndio chaguo pekee linaloweza kuhakikisha haki kwa Wapalestina na Waisraeli.
-
ICC: Vikwazo vya Marekani vimewaathiri majaji, hatutasalimu amri kwa shinikizo lolote
Dec 02, 2025 02:54Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), Jaji Tomoko Akane, amesema kwamba vikwazo vya Marekani vilivyowekwa dhidi ya maafisa wakuu na majaji wa mahakama hiyo vimeathiri moja kwa moja maisha binafsi ya majaji na maafisa walengwa.
-
Afisa wa jeshi la Uingereza: Tuliua makumi ya Waafghani, maafisa walificha uhalifu huo
Dec 01, 2025 23:54Afisa wa zamani wa jeshi la Uingereza amefichua mauaji yaliyofanywa na askari wa kikosi maalumu cha Uingereza nchini Afghanistan na jinsi makamanda wa kikosi hicho walivyonyamazia kimya na kuficha uhalifu huu.
-
Kwa nini umma unapaza sauti zaidi katika mitaa ya Paris kupinga migongano ya sera za Ulaya?
Dec 01, 2025 23:10Makumi ya maelfu ya watu huko Paris, mji mkuu wa Ufaransa, wametoa kauli mbiu "Muqawama; kutoka Paris hadi Palestina; wakiunga mkono Wapalestina.
-
Watu 1,000 wafariki dunia katika mafuriko Indonesia, Sri Lanka, Thailand, Malaysia
Dec 01, 2025 06:56Mafuriko mabaya yaliyozikumba nchi za Indonesia, Sri Lanka, Thailand na Malaysia yamepelekea zaidi ya watu 1,000 kupoteza maisha katika kipindi cha chini ya wiki moja. Kwa uchache watu 502 wameripotiwa kufariki dunia nchini Indonesia, 335 nchini Sri Lanka, 176 nchini Thailand na watatu nchini Malaysia.
-
SIPRI: Kushamiri kwa vita kumeyapatia faida ya kupindukia makampuni makuu ya uundaji silaha
Dec 01, 2025 03:01Takwimu mpya zilizotolewa kwenye ripoti ya Taasisi ya Utafiti wa Amani ya Kimataifa ya Stockholm (SIPRI) zinaoneysha kuwa, mapato yanayotokana na mauzo ya silaha na huduma za kijeshi ya makampuni 100 makubwa zaidi ya uundaji silaha duniani yalifikia rekodi ya dola bilioni 679 mwaka 2024.
-
Kampeni ya 'Komboa Mateka Wapalestina' walioko kwenye magereza ya Israel yazidi kupamba moto
Dec 01, 2025 02:15Maelfu ya waandamanaji jana Jumamosi walimiminika kwenye eneo la katikati mwa mji mkuu wa Uingereza, London katika maandamano ambayo ni sehemu ya kampeni ya "Komboa Mateka Wapalestina", wakitaka kuachiliwa huru Wapalestina zaidi ya 9,100 wanaoshikiliwa katika magereza ya kutisha ya utawala wa kizayuni wa Israel, wakiwemo zaidi ya wanawake na watoto 450.
-
ICC kupokea malalamiko dhidi ya viongozi wa FIFA na UEFA wanaohusika na uhalifu wa vita wa Israel
Nov 30, 2025 23:18Wachezaji wa kandanda wa Kipalestina, vilabu na mashirika ya kimataifa wanapanga kuwasilisha malalamiko katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) dhidi ya wakuu wa mashirikisho ya kandanda duniani, FIFA na UEFA, kwa msingi kuwa wamehusika katika kusaidia uhalifu wa vita na mfumo wa ubaguzi wa rangi wa utawala haramu wa Israel.
-
Changamoto za Umoja wa Ulaya katika kuchangisha fedha kwa ajili ya Ukraine
Nov 30, 2025 23:16Umoja wa Ulaya umekumbwa na changamoto nzito katika kuzishawishi nchi wanachama zikubali kuchangia fedha za kuendelea kuiunga mkono Ukraine kwenye vita vyao na Russia.