-
Caracas yamhutubu waziri wa Israel: Jina Venezuela ni kubwa, haliwezi kutamkwa na kinywa chako kichafu
Nov 25, 2025 23:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela ametumia lugha kali kujibu tuhuma za waziri wa mambo ya nje wa utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Caracas, kwa kumwita waziri huyo "mhalifu wa kivita" ambaye iwe sasa hivi au baadaye lazima akawajibishwe mbele ya vyombo vya haki na sheria vya kimataifa.
-
Katibu Mkuu wa UN atoa indhari kali: Dunia inabadilika kwa kiwango cha kutisha
Nov 25, 2025 23:31Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa onyo kali katika hotuba yake kwa Mkutano wa Saba wa Pamoja wa Umoja wa Afrika na Umoja wa Ulaya unaofanyika mjini Luanda Angola akisema, dunia inapitia mabadiliko ya kasi na ya kina, yanayochochewa na janga la tabianchi, kuongezeka kwa ukosefu wa usawa na misisimko ya nguvu za kimataifa.
-
Afghanistan: Shambulio la Pakistan limeua watoto tisa na mwanamke mmoja mkoani Khost
Nov 25, 2025 23:30Msemaji wa serikali ya muda ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban Zabihullah Mujahid, amesema watoto tisa na mwanamke mmoja wameuawa baada ya vikosi vya jeshi la Pakistan kushambulia nyumba moja katika jimbo la Khost kusini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Kwa nini Ulaya imechukua mkondo wa sera kali dhidi ya wakimbizi?
Nov 25, 2025 23:06Ujerumani inataka kuweka sheria kali zaidi dhidi ya wakimbizi na wahamiaji, na inapanga kufukuza nchini humo idadi kubwa ya wakimbizi.
-
Trump asaini dikri dhidi ya Ikhwanul Muslimeen
Nov 25, 2025 07:44Kwa kutia saini amri ya utendaji dhidi ya Ikhwanul Muslimeen au kwa jina jingine Muslim Brotherhood, Rais Donald Trump wa Marekani ameweka baadhi ya matawi ya kundi hilo la Kiislamu katika orodha ya "mashirika ya kigeni ya kigaidi".
-
Mahmood Mamdani: Israel ni dola la wavamizi, inafanya majaribio ya silaha zake juu ya vichwa vya watu wa Gaza
Nov 25, 2025 07:33Msomi na mwanafikra mashuhuri raia wa Uganda, Mahmood Mamdani, ambaye ni baba wa Muislamu wa kwanza kushinda nafasi ya umeya wa New York huko Marekani, Zohran Kwame Mamdani, ameishutumu Israel kuwa ni "nguvu ya uchokozi ambayo imepoteza hisia zote za maadili," na kwamba hakuna anayeamini kwamba kile inachofanya huko Gaza ni "kujilinda" kama inavyodai.
-
Afisa wa Umoja wa Mataifa: Hali bado ni mbaya huko Gaza
Nov 25, 2025 04:00Ramiz Alakbarov, Naibu Mratibu Maalumu wa Umoja wa Mataifa wa Mchakato wa Amani wa Mashariki ya Kati, ameonya kwamba hali katika Ukanda wa Gaza "inaendelea kuwa mbaya," na kusema kuwa familia nyingi haziwezi kumudu kununua kuku na nyama licha ya upatikanaji wa bidhaa za msingi za chakula na kuboreshwa kwa bei za bidhaa hizo.
-
Umoja wa Mataifa: Mwanamke mmoja huuliwa kila baada ya dakika 10
Nov 25, 2025 03:08Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa jana Jumatatu ilisema kwamba karibu wanawake 50,000 waliuawa na jamaa zao mwaka wa 2024, kwa kiwango cha mwanamke mmoja kila baada ya dakika 10, na kuelezea masikitiko yake kwamba hakuna maendeleo yoyote yaliyopatikana katika kupambana na mauaji ya wanawake.
-
Kura ya maoni: Wamarekani wengi wanapinga hatua za kijeshi dhidi ya Venezuela
Nov 24, 2025 23:14Kura ya maoni iliyofanywa na CBS News ikishirikiana na kampuni ya utafiti ya YouGov imeonyesha kuwa Wamarekani wengi wanapinga hatua zozote za kijeshi dhidi ya Venezuela.
-
Rais wa Korea Kusini: Mifumo ya kimataifa ya AI inapasa kuhakikisha mataifa yote yanapa teknolojia hiyo kwa usawa
Nov 24, 2025 23:10Rais wa Korea Kusini, Lee Jae Myung amesema kuwa mifumo ya kimataifa ya akili mnemba (AI) inapasa kuhakikisha kuwa mataiafa yote yanapata teknolojia hiyo kwa usawa.