-
Je, ni upi msimamo wa Umoja wa Ulaya kuhusu mpango wa Trump na usitishaji vita huko Gaza?
Oct 12, 2025 22:53Umoja wa Ulaya umeeleza kuwa usitishaji vita huko Gaza ni fursa ya kweli ya kuhitimisha vita vya uharibifu.
-
Mapigano makali yazuka kati ya majeshi ya Pakistan na Afghanistan kwenye mpaka wa nchi mbili
Oct 12, 2025 01:54Mapigano makali ya mpakani yamezuka kati ya majeshi ya Afghanistan na Pakistan huku vikosi vya nchi hizo mbili vikishambuliana kwa kutumia silaha nzito.
-
Amerika ya Kusini yagawanyika juu ya kiongozi wa upinzani Venezuela kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel
Oct 12, 2025 01:54Kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kiongozi wa upinzani nchini Venezuela María Corina Machado kumeibua hisia tofauti katika nchi za Amerika Kusini, huku baadhi ya viongozi wa nchi za eneo hilo wakipongeza hatua hiyo na wengine kulaani vikali kwa kuashiria matamshi na vitendo vya Machado vya kuchochea vurugu na machafuko au hata kuunga mkono kufanywa mashambulio na uvamizi wa kigeni dhidi ya nchi yake mwenyewe.
-
China: Marekani inakiuka mamlaka ya kujitawala ya mataifa mengine
Oct 11, 2025 22:51Fu cong, balozi na mwakilishi wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa amesema kuhusiana na uvamizi wa kijeshi wa Marekani dhidi ya Venezuela kwamba, hatua hiyo ya Washington inakiuka vikali mamlaka ya kujitawala ya mataifa mengine.
-
Kwa nini Trump amekosa Tuzo ya Amani ya Nobel?
Oct 11, 2025 07:37Baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kukosa Tuzo ya Amani ya Nobel, msemaji wa Ikulu ya White House ameikosoa Kamati inayoandaa Tuzo ya Nobel kwa kutomtunuku rais huyo tuzo hiyo, akiitaja hatua hiyo kuwa ni upendeleo wenye kufadhilisha siasa badala ya amani.
-
Wananchi wa Uruguay waandamana wakitaka kukatwa uhusiano na Israel
Oct 11, 2025 05:55Maelfu ya wananchi wa Uruguay waliingia mitaani na mabarabarani jana Ijumaa, kushiriki maandamano ya kuitaka serikali yao itambue mzozo wa kibinadamu unaoendelea Gaza kama mauaji ya halaiki, sanjari na kukata uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi na Israel.
-
China: Tutachukua hatua muhimu kujibu vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran
Oct 10, 2025 23:02Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesisitiza kuwa nchi yake itachukua hatua "muhimu" ili kulinda haki halali za makampuni na raia wa China katika kukabiliana na vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran.
-
Afghanistan; kutoka kwenye medani ya vita hadi kugeuzwa uwanja wa ushindani wa kijiopolitiki
Oct 10, 2025 22:55Miaka minne tangu ilipojiondoa Marekani, kwa mara nyingine tena Afghanistan imegeuzwa nukta kuu inayoangaziwa na madola yenye nguvu duniani.
-
Maria Machado ashinda tuzo ya amani ya Nobel; Trump aambulia patupu
Oct 10, 2025 07:54Mwanaharakati wa upinzani wa Venezuela María Corina Machado ameshinda Tuzo ya Amani ya Nobel 2025 kwa ujasiri wa kupigania demokrasia na uchaguzi huru licha ya vitisho. Kamati ya Nobel imemsifu kwa kuunganisha upinzani.
-
Bunge la Peru lamuondoa madarakani Rais Dina Boluarte
Oct 10, 2025 07:53Rais wa Peru mama Dina Boluarte ameondolewa madarakani kwa kura nyingi za wabunge, kufuatia hoja kadhaa zilizowasilishwa na makundi mbalimbali ya vyama vya siasa bungeni.