-
Save the Children: Zaidi ya nusu ya waathiriwa wa tetemeko la ardhi mashariki mwa Afghanistan ni watoto
Sep 15, 2025 00:29Shirika la Kimataifa la Save the Children limetangaza kuwa, karibu watoto 1,200 wamepoteza maisha na maelfu ya wengine kuachwa bila makao katika tetemeko la ardhi la hivi majuzi mashariki mwa Afghanistan, ambalo limechukua zaidi la nusu ya jumla ya wahanga.
-
Rais wa zamani wa Ireland: Nikiwa raia wa Ulaya 'naona aibu' kwa namna EU inavyoamiliana na Israel
Sep 14, 2025 07:32Rais wa zamani wa Ireland Mary Robinson amesema, "anaona aibu" kwa mjibizo ambao Umoja wa Ulaya (EU) umeonyesha kwa vita vinavyoendelezwa na Israel huko Ghaza, na akaukosoa umoja huo kwa kushindwa kusimamisha makubaliano yake ya kibiashara na utawala huo wa kizayuni licha ya wito uliotolewa wa kuutaka ufanye hivyo.
-
Mafuriko yaliyoikumba Punjab ya Pakistan yaua watu wapatao 101, yaathiri watu milioni 4.6
Sep 14, 2025 07:31Watu wasiopungua 101 wameaga dunia katika mafuriko yaliyolikumba jimbo la Punjab la Pakistan. Hayo ni kwa mujibu wa afisa mmoja wa Mamlaka ya Kudhibiti Maafa ya Mkoa (PDMA).
-
Maseneta wa US: Israel inaangamiza kizazi Ghaza na Marekani ni mshirika, dunia lazima ikomeshe
Sep 14, 2025 07:18Maseneta wawili waandamizi wa Marekani wameishutumu Israel kwa kutekeleza kampeni ya maangamizi ya kizazi katika Ukanda wa Ghaza na kubainisha kwamba Marekani inashiriki katika jinai hiyo na kwamba dunia lazima ichukue hatua kukomesha jambo hilo.
-
Russia yasema wanajeshi 1,500 wa Ukraine wameuawa kwa siku moja katika maeneo ya vita
Sep 13, 2025 23:12Msemaji mmoja wa kijeshi Russia amesema kuwa wanajeshi wa Ukraine wapatao 1,465 wameuawa katika kipindi cha saa 24 zilizopita kufikia Jumamosi, katika maeneo yote ya operesheni maalum ya kijeshi.
-
Kwa nini Putin anataka kukomeshwa vigezo vya undumakuwili na vitisho dhidi ya tamaduni duniani?
Sep 13, 2025 23:11Putin ametaka kukomeshwa vigezo vya undumakuwili na vitisho dhidi ya tamaduni duniani.
-
Askari 12 wa Pakistan wauawa katika shambulio la kigaidi kaskazini magharibi mwa nchi
Sep 13, 2025 07:23Askari wasiopungua 12 wa Pakistan wameuawa katika makabiliano ya kufyatuliana risasi na magaidi kaskazini-magharibi mwa nchi hiyo.
-
Baada ya machafuko ya umwagaji damu, Nepal yateua Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke; UN yakaribisha
Sep 13, 2025 07:22Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayohudumu nchini Nepal yamekaribisha kuteuliwa Sushila Karki kuwa Waziri Mkuu wa mpito, wakati nchi hiyo ikikumbwa na mshtuko kufuatia ukandamizaji wa umwagaji damu dhidi ya maandamano yaliyoongozwa na vijana, ambayo yalisababisha vifo vya zaidi ya watu 50, uharibifu mkubwa wa mali na kujiuzulu kwa mtangulizi wake.
-
UNGA laidhinisha kwa wingi mkubwa sana wa kura "Azimio la New York" la kuundwa Dola la Palestina
Sep 12, 2025 23:41Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) limepitisha kwa wingi mkubwa sana wa kura "Azimio la New York" linalotoa mwongozo wa kuchukuliwa "hatua zinazoonekana, katika muda maalumu na zisizoweza kutenduliwa" kuelekea kwenye uundwaji wa Dola la Palestina.
-
Mbunge wa Uskochi ataka Israel izuiwe kushiriki michezo barani Ulaya kutokana na mauaji ya kimbari Gaza
Sep 12, 2025 22:58Mbunge mmoja kutoka Uskochi amewasilisha hoja rasmi akitaka mashirika ya michezo barani Ulaya kuiondoa Israel katika mashindano ya kimataifa kutokana na mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza.