Pars Today

Kiswahili
  • Nyumbani
  • Radio
  • Albanian shqip
  • Armenian Հայերեն
  • Assyrian ܐܬܘܪ̈ܝܐ
  • Azeri Azəri
  • Bangla বাংলা
  • Chinese 中文
  • Dari دری
  • English English
  • French français
  • German Deutsch
  • Hausa Hausa
  • Hebrew עברית
  • Hindi हिन्दी
  • Indonesian Bahasa Indonesia
  • Italian Italiano
  • Japanese 日本語
  • Kazakh қазақ тілі
  • Kiswahili Kiswahili
  • Pashto پښتو
  • Persian فارسی
  • Russian Русский
  • Spanish Español
  • Tajik Тоҷик
  • Taleshi Tolışə
  • Turkish Türkçe
  • Turkmen Türkmen
  • Uzbek узбек
  • Dunia
  • Asia Magharibi
  • Iran
  • Afrika
  • Dini
  • Parspedia
  • Disinfo

Ayatullah Khamenei

  • Iran yatangaza mashtaka rasmi dhidi ya Marekani na Israel kuhusu mauaji ya kigaidi ya Kiongozi Muadhamu na wanafunzi wa Minab

    Iran yatangaza mashtaka rasmi dhidi ya Marekani na Israel kuhusu mauaji ya kigaidi ya Kiongozi Muadhamu na wanafunzi wa Minab

    Aug 30, 2026 03:48

    Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa hati rasmi za mashtaka kufuatia vitendo vya kigaidi vilivyofanywa na muungano wa Marekani na Israel, ambavyo vilisababisha kuuawa kishahidi kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, pamoja na wanafamilia wake wanne, sambamba na wanafunzi na walimu katika shule moja mjini Minab.

  • Iran yaendelea kuboresha sekta yake ya ulinzi baada ya vita vya Marekani na Israel

    Iran yaendelea kuboresha sekta yake ya ulinzi baada ya vita vya Marekani na Israel

    Aug 22, 2026 02:55

    Wizara ya Ulinzi ya Iran imesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu inaendelea kuifanya sekta yake ya ulinzi kuwa ya kisasa, ikizingatia mahitaji yaliyojitokeza kutokana na vita vya hivi karibuni vilivyolazimishwa dhidi ya nchi hii na Marekani na Israel.

  • Marasimu ya Arubaini ya kumuenzi Kiongozi shahidi wa Iran na familia yake yafanyika Musalla wa Imam Khomeini, Tehran

    Marasimu ya Arubaini ya kumuenzi Kiongozi shahidi wa Iran na familia yake yafanyika Musalla wa Imam Khomeini, Tehran

    Aug 18, 2026 15:39

    Sambamba na kutimia siku arubaini tangu kufanyika mazishi ya kihistoria ya kiongozi wa Iran aliyeuliwa shahidi, shughuli ya kumbukumbu ya kumuenzi kiongozi huyo shahidi na familia yake imefanyika leo katika eneo la Swala (Mosalla) la Imam Khomeini (RA) mjini Tehran.

  • Ayatullah Mojtaba Khamenei asifu ushiriki ‘wa kihistoria’ wa waumini katika mazishi, aapa kulipiza kisasi kwa Kiongozi Shahidi

    Ayatullah Mojtaba Khamenei asifu ushiriki ‘wa kihistoria’ wa waumini katika mazishi, aapa kulipiza kisasi kwa Kiongozi Shahidi

    Jul 11, 2026 12:01

    Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ametoa shukrani zake za dhati kwa mahudhurio “ya kustaajabisha, yenye kuvunja nguvu za adui na ya kihistoria” katika mazishi ya Kiongozi Shahidi, akisisitiza kuwa malipo ya kisasi dhidi ya “watenda jinai wauaji waliodhalilika” ni jambo la yakini.

  • Kiongozi Shahidi Ayatullah Khamenei azikwa katika Haram ya Imam Ridha (a.s) mjini Mash'had

    Kiongozi Shahidi Ayatullah Khamenei azikwa katika Haram ya Imam Ridha (a.s) mjini Mash'had

    Jul 11, 2026 02:37

    Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran Ayatullah Sayyid Aali Khamenei amezikwa katika Haram ya Imam Ridha (a.s) mjini Mash'had kaskazini mashariki mwa Iran.

  • Rais Pezeshkian: Mazishi ya Kiongozi wa Iran ni kielelezo cha umoja wa kitaifa

    Rais Pezeshkian: Mazishi ya Kiongozi wa Iran ni kielelezo cha umoja wa kitaifa

    Jul 09, 2026 03:33

    Rais Masoud Pezeshkian amesema mahudhurio makubwa ya watu kutoka matabaka yote ya jamii katika mazishi makubwa yaliyofanyika kwa ajili ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ni kielelezo cha umoja wa kitaifa nchini Iran.

  • Mamilioni wamuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Khamenei katika miji ya Najaf na Karbala nchini Iraq

    Mamilioni wamuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Khamenei katika miji ya Najaf na Karbala nchini Iraq

    Jul 08, 2026 14:19

    Mamilioni ya waombolezaji leo Jumatano walikusanyika katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala nchini Iraq kwa ajili ya kuaga na kutoa heshima zao za mwisho kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei na familia yake waliouliwa shahidi katika mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

  • Pezeshkian: Kufa shahidi Ayatullah Khamenei kumetoa msukumo kwa Waislamu kudumisha umoja

    Pezeshkian: Kufa shahidi Ayatullah Khamenei kumetoa msukumo kwa Waislamu kudumisha umoja

    Jul 05, 2026 11:15

    Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kuwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu hayati Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na kuuawa kwake shahidi, vimewapa Waislamu kote duniani hamasa katika harakati zao za kudumisha umoja na mshikamano.

  • Makundi ya Ulaya yanayopinga ubeberu yawasili Iran kwa mazishi ya Kiongozi Shahidi

    Makundi ya Ulaya yanayopinga ubeberu yawasili Iran kwa mazishi ya Kiongozi Shahidi

    Jul 03, 2026 03:53

    Misafara ya wanaharakati wanaopinga ubeberu, wasomi, waandishi wa habari na wawakilishi wa vituo vya Kiislamu kutoka kote barani Ulaya inaendelea kuwasili Tehran kushiriki katika mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliyeuawa shahidi katika shambulizi la kushtukiza la Marekani na Israel.

  • Pezeshkian: Mahudhurio makubwa katika mazishi ya Kiongozi Shahidi ni ‘jibu madhubuti’ kwa ubeberu na ugaidi

    Pezeshkian: Mahudhurio makubwa katika mazishi ya Kiongozi Shahidi ni ‘jibu madhubuti’ kwa ubeberu na ugaidi

    Jul 03, 2026 03:51

    Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa umati mkubwa wa wananchi utakaojitokeza katika shughuli ya mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, utakuwa “jibu madhubuti” dhidi ya vitendo vya kigaidi, ukatili na mbinu za kibeberu. Amesema kuwa tukio hilo litakuwa dhihirisho la wazi la umoja wa taifa la Iran na dhamira yake isiyotetereka katika kulinda uhuru na heshima ya nchi.

Onesha Zaidi
Pars Today

© 2026 PARS TODAY. All Rights Reserved.

Habari
    Dunia
    Asia Magharibi
    Iran
    Afrika
    Dini
    Parspedia
    Disinfo
Pars Today
    SISI NI
    Wasiliana Nasi
    RSS