Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Bandari na Ubaharia la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza habari ya kujengwa bandari kubwa zaidi ya kibiashara ya Iran katika Bahari ya Oman na katika eneo la Kuhe Mubarak katika wilaya ya Jask katika mkoa wa Hormozgan, kusini mwa nchi.
Msemaji wa Ikulu ya Russia (Kremlin), Dmitry Peskov ametoa radiamali kufuatia tuhuma zisizo na msingi za Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kusema kuwa, Moscow haizipi umuhimu tuhuma kwamba Tehran ilihusika na tukio la kushambuliwa meli katika Bahari ya Oman.
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Marekani hivi sasa imesakamwa na kipengee cha kisiasa cha kutoona haya na kukosa heshima ambacho kinaifanya isizingatie matokeo ya matamshi yake.
Marekani katika kipindi hiki cha utawala wa Rais Donald Trump imeanzisha jitihada za kuasisi muungano na kuimarisha uwepo wake katika eneo la Asia magharibi hususan katika Ghuba ya Uajemi kwa kisingizio cha eti kuwepo vitisho kutoka kwa Iran.
Viongozi mashuhuri wa kisiasa nchini Marekani na Uingereza wameionya vikali serikali ya Washington, dhidi ya kutumia tukio la kushambuliwa meli za mafuta katika Bahari ya Oman kama kisingizio cha kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Gazeti la Al-Quds Al-Arabi linalochapishwa London, Uingereza limeandika kuwa, baadhi ya pande katika eneo la Asia Magharibi hususan Saudi Arabia na utawala haramu wa Israel, zinahusika kushadidisha migogoro katika eneo.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Tehran imesikitishwa na matukio ya jana Jumapili yaliyotokea dhidi ya meli kadhaa za mafuta katika Bahari ya Oman katika eneo la Umoja wa Falme za Kiarabu na imetaka kuwekwa wazi na kwa kina uhakika wa matukio hayo.