-
Kujiondoa rasmi Marekani katika Mapatano ya Tabianchi ya Paris
Nov 05, 2020 07:52Marekani ambayo imejiondoa katika mikataba kadhaa ya kimataifa wakati wa utawala wa Donald Trump, sasa imejiondoa rasmi katika Makubaliano ya Mabadiliko ya Tabianchi yaliyofikiwa mjini Paris, Ufaransa mwaka 2015. Mapatano hayo ni muhimu katika kulinda mazingira ili kuzuia ongezeko la joto duniani.
-
Kurefusha Marekani vikwazo dhidi ya Sudan; zawadi ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel
Nov 03, 2020 13:41Serikali ya Trump ikiwa na lengo la kuuridhisha utawala wa haramu wa Israel imechukua hatua tofauti ikiwemo ya kuandaa uwanja wa kutambuliwa rasmi utawala huo na mataifa ya Kiarabu na Kiislamu ambapo hatua yake ya karibuni kabisa na kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya Sudan na utawala huo ghasibu.
-
Mkuu wa zamani wa CIA: Nina wasiwasi wa Trump kujitangaza mshindi mapema
Nov 02, 2020 13:26Mkuu wa zamani wa shirika la ujasusi la Marekani CIA amesema, ana wasiwasi wa machafuko ya uchaguzi na rais wa nchi hiyo Donald Trump kujitangaza mshindi wa uchaguzi mapema.
-
Kushadidi migawanyiko ya kisiasa na kijamii Marekani
Nov 02, 2020 11:38Kampeni za uchaguzi wa rais wa Marekani zimefika ukingoni. Ikiwa imesalia masaa machache kabla ya uchaguzi mkuu, kumeshuhudiwa majibizano makali baina ya wagombea urais na wafuasi wao na hata katika baadhi ya maeneo kumeripotiwa kuongezeka mapigano ya mitaani baina ya wafuasi wa kambi mbili hasimu za kisiasa.
-
'Trump ni gaidi nambari moja duniani'
Nov 01, 2020 02:48Mshauri wa sera za kigeni wa Spika wa Bunge la Iran ameashiria mauaji ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ambaye aliuawa kigaidi kufuatia amri ya Rais Donald Trump wa Marekani na kusema, Trump ni gaidi nambari moja duniani.
-
Sanders: Donald Trump ana maradhi ya kusema uongo na fikra za kidikteta
Oct 31, 2020 11:04Seneta wa jimbo la Vermont na mwanasiasa mashuhuri wa Marekani, Bernie Sanders amemtaja Rais Donald Trump wa nchi hiyo kuwa ni kidhabi, na kusisitiza kuwa uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika tarehe 3 Novemba mwaka huu nchini humo ndio muhimu zaidi katika historia ya Marekani.
-
Kusitishwa uanachama wa Corbny ndani ya chama cha Leba kutokana na misimamo yake dhidi ya Uzayuni
Oct 31, 2020 10:01Jeremy Corbyn, kiongozi wa zamani wa chama cha Leba nchini Uingereza siku zote amekuwa akichukiwa na duru za Magharibi na Kizayuni kutokana na misimamo yake huru anayochukua hususan ya kupinga vitendo visivyo vya kibinadamu vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina kupitia matamshi na taarifa anazotoa.
-
Macron aendeleza vitendo vya kuuhujumu Uislamu; Trump aparamia mawimbi
Oct 31, 2020 02:38Kushtadi vitendo vya chuki na hujuma dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa vinavyokwenda sambamba na uungaji mkono wa Rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron kwa kisingizio kutetea uhuru wa kusema na kujieleza kumekabiliwa na radiamali mbalimbali na kuifanya nchi hiyo kubwa ya Ulaya ikabiiwe na wimbi kubwa la hasira.
-
Mwakilishi wa Marekani: Kuanzisha uhusiano na Israel hakutazuia kumegwa Ufukwe wa Magharibi
Oct 30, 2020 16:33Mwakilishi wa rais wa Marekani wa masuala ya Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) amesema mpango wa kumegwa sehemu ya eneo la Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan na kuunganishwa na Israel ungali uko pale pale.
-
Kufichuliwa hatua za upendeleo za Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa Marekani kwa maslahi ya kampeni za uchaguzi za Trump
Oct 30, 2020 12:39Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa Marekani John Ratcliffe amezungumzia tuhuma za Iran kuingilia uchaguzi wa mwaka huu wa Marekani ambazo sasa imebainika kuwa zimetolewa ili kuimarisha kampeni za uchaguzi za Donald Trump.