Feb 08, 2021 07:46
Wizara ya afya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, imetangaza kupatikana kwa mgonjwa mpya wa Ebola kwenye mji wa Butembo jimboni Kivu Kaskazini, eneo ambalo lilikuwa kitovu cha mlipuko wa 10 wa ugonjwa huo uliotangazwa kumalizika mwezi Juni mwaka jana.