Huku Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikiendelea kukabiliana na janga la sasa la virusi vya corona, mlipuko mpya wa virusi vya Ebola umeripotiwa katika mkoa wa magharibi mwa nchi wa Equateur.
Maafisa wa afya katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wametangaza kuwa, maambukizi ya ugonjwa wa Ebola yamerejea tena nchini humo.
Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza habari ya kuthibitishwa kesi nyingine moja ya ugonjwa wa Ebola huko Jamhhuri ya Kidemokrasia ya Congo zikiwa zimesalia siku chache tu kabla ya kutangazwa rasmi kumalizika kabisa ugonjwa huo nchini humo.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa mgonjwa wa mwisho wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ameruhisiwa kurejea nyumbani baada ya kupatiwa matibabu katika kituo cha matibabu huko kaskazini mashariki mwa mji wa Beni.
Shirika la Afya Duniani WHO limesema dunia ni lazima iendelee kufadhili vita dhidi ya ugonjwa hatari wa Ebola kwani kuzembea katika hilo kutaleta madhara makubwa.
Maafisa wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamesema, maambukizi ya ugonjwa hatari wa ebola yameongezeka katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha kuwa, vita na mapigano huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yanakwamisha jitihada za kutokomeza ugonjwa hatari wa Ebola ambao umeua maelfu ya watu kufikia sasa.
Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mpaka (MSF) imetangaza kuwa maafisa wa afya wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameanza kutoa chanjo mpya ya kudhibiti ugonjwa wa Ebola iliyotengenezwa na kampuni ya Johnson & Johnson.
Shirika la Afya Dunia na maafisa wa serikali ya Congo DR wametoa mapendekezo ya kufanyika mabadiliko kuhusu jinsi ya kuwahudumia waathira wa ugonjwa wa Ebola.
Ugonjwa wa kutatanisha uliozuka katika jimbo la Katsina kaskazini mwa Nigeria umeua zaidi ya watu 60 katika jimbo hilo.