-
Abiy Ahmed: Hatuzungumzi na yeyote kuhusu manufaa yetu ya kitaifa ya bwawa la al Nahdha
Jul 12, 2021 22:06Waziri Mkuu wa Ethiopia amesema baada ya kupata ushindi chama chake katika uchaguzi wa Bunge kwamba, kabla ya bwawa la al Nahdha kuwa na manufaa ya uzalishaji wa nishati, lina manufaa makubwa zaidi kwa Ethiopia katika kutangaza nguvu na mshikamano wa wananchi wake.
-
Ushindi wa chama tawala katika uchaguzi wa Bunge nchini Ethiopia na changamoto za baadaye
Jul 12, 2021 03:00Hatimaye na baada ya kuahirishwa kwa miezi kadhaa, matokeo ya uchaguzi wa Bunge na serikali za mitaa yanaonesha kuwa, chama tawala nchini Ethiopia kimeibuka na ushindi kwa kupata viti 410 vya Bunge.
-
Ripoti: Eneo la Pembe ya Afrika liko katika ncha ya vita na machafuko
Jul 07, 2021 01:22Ripoti zinaonesha kuwa eneo la Pembe ya Afrika hususan nchi za Ukanda wa Mto Nile zinakabiliwa na hatari ya vita na machafuko makubwa baada ya Ethiopia kuanza awamu ya pili ya kujaza maji katika Bwawa la Renaissance.
-
Balozi wa Ethiopia alalamikia kugeuzwa Bwawa la al Nahdha kuwa kadhia ya kisiasa
Jul 05, 2021 01:40Balozi wa Ethiopia nchini Sudan amesema kuwa, inasikitisha kuona kwamba kumeingizwa siasa katika mradi wa Bwawa la al Nahdha wakati ambapo tangu mwanzo huo ulikuwa ni mradi wa maendeleo tu.
-
Ombi la Misri na Sudan kwa Baraza la Usalama; mgogoro wa Bwawa la An Nahda
Jun 28, 2021 05:56Huku awamu ya pili ya kujazwa maji katika Bwawa la An Nahda (Grand Renaissance Dam-GERD-) la Ethiopia katika Mto Nile ikikaribia, Misri na Sudan, nchi mbili ambazo zinapinga ujenzi wa bwawa hilo, zimetaka ujazwaji maji huo usitishwe kwa muda. Nchi hizo mbili zimetaka Ethiopia izipatie dhamana kuwa haki zao zitalindwa, jambo ambalo limeibua taharuki mpya baina ya nchi hizo tatu.
-
Sudan yakubali kwa masharti makubaliano ya muda ya Bwawa la Renaissance
Jun 28, 2021 04:57Waziri wa Mambo ya nje wa Sudan Mariam Al-Sadiq Al-Mahdi amesema kuwa nchi yake imepokea pendekezo kutoka kwa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo la makubaliano ya muda ya kujazwa maji Bwawa la Renaissance yanayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na Marekani.
-
Ethiopia yapinga hatua ya Sudan ya kutaka UN ijadili kadhia ya Bwawa la Renaissance
Jun 25, 2021 22:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje ya Ethiopia, Dina Mufti amepinga wito uliotolewa na Sudan wa kufanya kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili mgogoro wa Bwawa la Renaissance, akisema ujenzi wa bwawa hilo ni mradi wa maendeleo ambao si katika masuala yanayolihusu baraza hilo lililopewa dhamana ya kudumisha amani na usalama wa kimataifa.
-
Makumi wauawa katika shambulio la anga sokoni kaskazini mwa Ethiopia
Jun 23, 2021 23:11Makumi ya watu wameuawa katika shambulio la anga dhidi ya soko moja katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia.
-
Kura za uchaguzi wa Bunge Ethiopia zaendelea kuhesabiwa, mahudhurio ya wananchi yalikuwa makubwa
Jun 22, 2021 06:27Mchakato wa kuhesabu kura za uchaguzi wa Bunge na serikali za mitaa unaendelea nchini Ethiopia huku yombo vya usalama vikisema umefanyika kwa amani na usalama, ukitupilia mbali malalamiko machache ya hapa na pale.
-
Waethiopia wapiga kura katika uchaguzi muhimu wa Bunge
Jun 21, 2021 06:03Mamilioni ya wananchi wa Ethiopia mapema leo wameelekea kwenye masanduku ya kupigia kura kwa ajii ya kuchagua wawakilishi wao katika Bunge la nchi hiyo, uchaguzi ambao umesusiwa na baadhi ya vyama vya upinzani.