-
Ombi la Algeria kwa Jamii ya Kimataifa kuliunga mkono taifa la Palestina dhidi ya jinai za utawala wa Kizayuni
Oct 09, 2023 03:13Kupitia taarifa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Algeria imetaka uingiliaji kati wa haraka wa Jumii ya Kimataifa kupitia taasisi husika ili kuliunga mkono taifa la Palestina dhidi ya jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Amnesty: Hujuma za Israel dhidi ya Gaza yumkini ni jinai za kivita
Jun 15, 2023 03:05Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema huenda Israel ilifanya jinai za kivita katika mashambulizi ya anga ya utawala huo haramu wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza mwezi uliopita wa Mei.
-
Januari 19; Siku ya Ghaza na nembo ya muqawama wa Kiislamu
Jan 19, 2023 06:36Januari 19 imetajwa katika kalenda ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni "Siku ya Ghaza" kwa mnasaba wa kumbukumbu ya vita vya siku 22 katika Ukanda wa Ghaza huko Palestina.
-
Kwa mnasaba wa Siku ya Gaza, Waarabu watakiwa kuwa bega kwa bega na Muqawama kama ilivyo Iran
Jan 18, 2023 23:32Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, Iran inaunga mkono kishujaa kadhia na piganio tukufu la Palestina; na inavyotarajiwa, nchi za Kiarabu nazo pia zichukue msimamo kama huo wa Tehran.
-
Moto waua watu 21 Ukanda wa Gaza, Mamlaka ya Ndani yatangaza maombolezo ya umma
Nov 18, 2022 03:01Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ukanda wa Gaza imetangaza habari ya kufariki dunia watu wote waliokuwa katika jengo la ghorofa lililoteketea kwa moto katika kambi ya Jabalia kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, huku Jeshi la Ulinzi la Wananchi likieleza kuwa wafanyakazi wake wameopoa miili 21 ya waliofariki dunia kutokana na moto huo.
-
Wapalestina wa Gaza wataka kushtakiwa Wazayuni walioua watoto wao
Aug 17, 2022 07:47Wakazi wa Ukanda wa Gaza wamefanya maandamano wakitaka kufunguliwa mashitaka utawala wa Kizayuni wa Israel katika mahakama za kimataifa, kwa kuua watoto wa Kipalestina katika eneo hilo ambalo liko chini mzingiro.
-
Kukiri Mkuu wa Sera za Nje wa EU kwamba Magharibi imeonyesha undumakuwili katika kadhia za Ukraine na Gaza
Aug 14, 2022 21:52Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amekiri kuwa nchi za Magharibi zinatumia vipimo vya nyuso mbili na za undumilakuwili kuhusiana na masuala ya kimataifa.
-
Wamagharibi wakosolewa kwa undumakuwili juu ya vita Ukraine na Gaza
Aug 14, 2022 02:55Harakati inayopinga dhulma na ukandamizaji wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina imekosoa vikali undumakuwili wa nchi za Magharibi kuhusu vita nchini Ukraine kwa upande mmoja na katika Ukanda wa Gaza, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu kwa upande mwingine.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuhusu kuinuliwa hadhi ya Harakati ya Jihad Islami
Aug 13, 2022 04:06Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amejibu barua ya Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina na kusema, "mapambano (muqawama) ya kishujaa ya Jihad Islami yatapelekea kupanda hadhi ya harakati hiyo katika mapambano sambamba na kusambaratisha hadaa za utawala wa Kizayuni na kuufedhehesha utawala huo."
-
Abdollahian awapongeza wanamuqwama kwa kukabiliana na wanajeshi wa Kizayuni
Aug 09, 2022 20:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwa mara nyingine tena wanajihadi za harakati za muqawama wa Palestina wameweza kusimama kidete mkabala wa nguvu kubwa za kijeshi za utawala wa Kizayuni, na hatimaye wakawalazimisha maadui kusalimu amri na kuafiki kusitisha vita.