-
Mapatano ya Aal Khalifa na utawala wa Kizayuni, chachu ya mapambano ya wananchi wa Bahrain
Sep 12, 2020 11:01Ikiwa umepita karibu mwezi mmoja tangu Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel zifikie mapatano ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia, Rais Doald Trump wa Marekani ametangaza kwamba Bahrain na utawala wa Kizayuni pia zimekubaliana kuanzisha uhusiano kama huo.
-
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na udhaifu katika kutetea maslahi ya Waarabu
Sep 10, 2020 10:56Kikao cha Jumatano ya jana cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Kiarabu (Arab League) kilichofanyika kwa njia ya video, kilimaliza kazi zake kwa kuunga mkono mapatano ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Imarati na Israel.
-
Mtifuano wa ana kwa ana kati ya Palestina na asasi za Waarabu kuhusu Makubaliano ya Abraham
Sep 09, 2020 13:36Kikao cha leo cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Arab League kimefanyika wakati msimamo ulioonyeshwa na jumuiya hiyo pamoja na Baraza Kuu la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi GCC, hususan katika siku za karibuni kuhusu mapatano yaliyofikiwa kati ya Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel umethibitisha kuwa, tajiriba ya uchukuaji maamuzi kitaasisi katika Ulimwengu wa Kiarabu imefeli;
-
Malalamiko ya Sudan kuhusu mashinikizo ya Marekani ya kuwa na uhusiano na Israel
Sep 06, 2020 11:42Serikali ya Trump muda wote imekuwa ikijionesha ni mtumishi asiye na doa wa malengo ya utawala wa Israel na imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kama kuzilazimisha nchi za Kiarabu na za Waislamu kutangaza uhusiano wa kawaida na utawala huo wa Kizayuni. Hata hivyo baadhi ya nchi kama Sudan zimeamua kupinga na pia kukabiliana na njama hizo.
-
Harakati ya PFLP yataka kutimuliwa Imarati katika Jumuiya ya Nchi za Kiarabu
Sep 06, 2020 02:26Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Wananchi kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina (PFLP) amesema kuwa, hatua ya Imarati ya kuanzisha uhusiano na utawala haramu wa Israel inakinzana na uamuzi wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu hivyo ametoa wito wa kutimuliwa nchi hiyo sambamba na kurejeshwa Syria katika jumuiya hiyo.
-
Imarati kufungua ubalozi wake Israel ndani ya miezi 5
Sep 05, 2020 11:23Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Falme za Kiarabu amesema nchi hiyo inatazamiwa kufungua ubalozi ndani ya utawala haramu wa Israel katika kipindi cha kati ya miezi mitatu hadi mitano.
-
Kikao cha kiistratijia cha Beirut, sauti moja ya Wapalestina
Sep 05, 2020 06:23Makundi ya Palestina yameitisha kikao cha pamoja mjini Beirut, Lebanon na kulaani njama mbalimbali zinazofanywa dhidi ya Palestina na wamesisitiza kuwa kitu kimoja na kuendelea na muqawama katika kukabiliana na njama za Kiarabu/Kimagharibi na Kizayuni.
-
Jordan yatoa msimamo kuhusu njama ya UAE na Israel ya kutaka kubadilisha hali ya msikiti wa Al Aqsa
Sep 02, 2020 15:09Wizara ya Mambo ya Nje ya Jordan imetangaza kuwa, Idara ya Waqfu ya nchi hiyo ndio pekee yenye mamlaka na ustahiki wa kusimamia masuala ya Msikiti mtukufu wa Al Aqsa na uendeshaji wake.
-
UN: Muungano wa Saudia ungali unaishambulia Yemen kwa mabomu yaliyopigwa marufuku
Sep 02, 2020 15:05Umoja wa Mataifa umeeleza katika ripoti kuwa, muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia unatumia mabomu yaliyopigwa marufuku ya vishada katika mashambulio yake dhidi ya mji wa al Hudaydah, magharibi mwa Yemen.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi: Imarati imeusaliti Ulimwengu wa Kiislamu na Palestina
Sep 01, 2020 13:10Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameitaja hatua ya serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ya kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni kuwa ni kuusaliti Ulimwengu wa Kiislamu, Ulimwengu wa Kiarabu na nchi za eneo na kadhia muhimu ya Palestina.