-
Maulamaa wa Kiislamu: Kuwa na uhusiano wa kawaida na Israel ni kudharau jinai zake
Sep 01, 2020 02:32Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Kiislamu amesema kwamba, kitendo cha baadhi ya nchi za Kiarabu cha kuweka uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel ni kufumbia macho jinai za utawala huo katili dhidi ya wananchi wa Palestina.
-
Imarati yazidi kuikumbatia Israel, yaruhusu ndege za utawala huo
Aug 29, 2020 23:58Umoja wa Falme za Kiarabu umebatilisha sheria ya kuususia utawala haramu wa Israel na adhabu ya kukiuka sheria hiyo iliyokuwa imepiga marufuku kufanya miamala yoyote ya kibiashara na kifedha na utawala huo wa Kizayuni.
-
Iran: 'Mashariki ya Kati' mpya itaanzishwa kwa kutimuliwa Marekani katika eneo
Aug 28, 2020 12:35Msaidizi maalumu wa Spika wa Bunge la Iran katika masuala ya kimataifa amesema: 'Mashariki ya Kati' mpya itaundwa baada ya kuhakikisha Marekani imeshatimuliwa kikamilifu katika eneo hili la Asia Magharibi.
-
Israel na Umoja wa Falme za Kiarabu zakubaliana kujenga vituo vya kijasusi Yemen
Aug 28, 2020 06:52Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na utawala wa Kizayuni wa Israel zimesema kuwa zimekubaliana kushirikiana kuanzisha vituo vya ujasusi katika eneo la kistratejia la Socotra huko Yemen. Hiyo ni kufuatia mapatano yaliyofikiwa kati ya Abu Dhabi na Tel Aviv l ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya pande mbili.
-
Sudan yataka kuondolewa katika orodha ya ugaidi, yakataa kuanzisha uhusiano na Israel
Aug 26, 2020 06:08Serikali ya Sudan imetoa taarifa ikiiambia Marekani kwamba suala la kuondolewa jina la Sudan katika orodha ya magaidi halipasi kushurutishwa na kuanzisha uhusiano wa kidoplomasia na utawala haramu wa Israel.
-
Safari ya kieneo ya Mike Pompeo; juhudi za kuupa uhalali utawala wa Kizayuni wa Israel
Aug 25, 2020 12:19Katika kipindi cha uongozi wa Rais Donal Trump nchini Marekani, nchi hiyo imefanya mambo na kuchukua hatua ambazo hazijawahi kushuhudiwa huko nyuma kwa maslahi ya utawala haramu wa Israel.
-
Maulamaa wa Kisunni Iran walaani makubaliano ya Israel na UAE
Aug 24, 2020 12:01Wanazuoni wa Kisunni hapa nchini Iran wamekosoa vikali mapatano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya pande mbili hizo.
-
Kushadidi tofauti baina ya Uturuki na UAE na hatari ya kuharibika zaidi uhusiano wa nchi mbili
Aug 23, 2020 08:03Uhusiano wa Uturuki na Umoja wa Falme za Kiarabu unaelekea kuharibika zaidi baada ya Mkuu wa Mashtaka wa serikali ya Ankara kuiomba Polisi ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai INTERPOL imtie nguvuni Mohammed Dahlan, mshauri wa Mohammed bin Zayed, mrithi wa ufalme wa Imarati.
-
Wanaharakati wa Imarati wapinga hatua ya serikali ya nchi hiyo ya kufikia mapatano na utawala wa Kizayuni
Aug 21, 2020 00:08Wanaharakati wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) wameyataja mapatano yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na utawala wa Kizayuni ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya pande mbili kuwa ni kukiuka katiba na na kupuuza msimamo wa viongozi wa mwanzo wa Imarati katika kuinga mkono Palestina.
-
Bunge la Tunisia limelaani mapatano kati ya Imarati na utawala wa Kizayuni
Aug 18, 2020 06:57Bunge la Tunisia limelaani mapatano yaliyofikiwa ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na utawala ghasibu wa Israel.