-
Ujerumani, mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu katika joho la mtetezi wa haki za binadamu
Nov 26, 2022 23:00Ujerumani, kama mwanachama wa Umoja wa Ulaya, pamoja na Marekani, imechukua mtazamo wa kiadui na kuingilia masuala ya ndani ya Iran wakati wa machafuko na ghasia za hivi karibuni.
-
Uungaji mkono wa Marekani kwa makundi yanayotaka kujitenga ya Iran
Nov 25, 2022 23:01Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imelaani operesheni za kijeshi Iran dhidi ya makundi ya kigaidi ya Wakurdi wanaotaka kujitenga yaliyoko kaskazini mwa Iraq na imeitaka Tehran kusitisha mashambulizi hayo.
-
Kombe la Dunia: Iran yaichapa Wales 2-0 na kuhuisha matumaini ya kusonga mbele
Nov 25, 2022 09:28Timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iimeichapa Wales mabao 2 kwa 0 katika fainali za mashindano ya soka ya Kombe la Dunia yanayoendelea nchini Qatar.
-
Raisi: Ustawi wa Iran unawaghadhabisha maadui
Nov 24, 2022 08:09Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema ustawi na maendeleo yanayoshuhudiwa hapa nchini yamewakasirisha mno maadui wa taifa hili.
-
Kuanza urutubishaji wa urani wa asilimia 60 katika kituo cha Fordo; radiamali ya Iran kwa hatua za uhasama za Magharibi
Nov 24, 2022 03:47Ikiwa ni katika kujibu azimio la hivi karibuni la Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran limetangaza uzalishaji wa urani iliyorutubishwa hadi kiwango cha asilimia 60 katika kituo cha Fordo.
-
Kukiri Grossi kuhusu kutokuwepo mpango wa kijeshi wa nyuklia nchini Iran
Nov 23, 2022 22:52Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA akijibu swali kuhusu uwezekano wa Iran kupata bomu la nyuklia amesema: "Katika kiwango cha sasa cha uzalishaji urani iliyorutubishwa, Iran imeweza kuzalisha kiwango cha kutosha cha kuiwezesha kutengeneza zaidi ya kifaa kimoja (cha mlipuko) iwapo itataka kufanya hivyo."
-
Al Mayadeen: Silaha nyingi zilizotumiwa kwenye machafuko Iran zimeingizwa kupitia Kurdistan ya Iraq
Nov 22, 2022 08:10Televisheni ya Al Mayadeen imeeleza katika ripoti maalumu kuwa, silaha nyingi zilizoingizwa kimagendo nchini Iran kwa ajili ya kutumiika katika vitendo vya kigaidi, kuzusha machafuko na kuvuruga amani zimepitishwa kwa kutumia mpaka wa eneo la Kurdistan ya Iraq.
-
Bunge la EU launga mkono ghasia nchini Iran, lavunja uhusiano na Tehran
Nov 22, 2022 04:42Katika hatua isiyo ya kidiplomasia na inayolenga kushajiisha zaidi fujo na ghasia hapa nchini Iran, Bunge la Umoja wa Ulaya limetangaza kukata uhusiano na Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi: Shari bila shaka itasambaratishwa
Nov 19, 2022 08:56Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema lengo kuu la wachochezi wa machafuko ya hivi karibuni ni kuliingiza taifa la Iran katika medani na kuongeza kuwa: "Mchafuko hayo bila shaka yatakomeshwa na taifa kuendelea kusonga mbele kwa nguvu zaidi na ari mpya katika uwanja wa maendeleo ya nchi."
-
Russia na China zapinga azimio la Bodi ya Magavana ya Wakala wa IAEA dhidi ya Iran
Nov 19, 2022 08:22Azimio jipya la Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) dhidi ya miradi ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani limepasishwa ambapo limetuma ujumbe ulio wazi kufuatia kupungua kwa kura za nchi zilizoliunga mkono licha ya mashinikizo mapya ya kisiasa ya Marekani na Troika ya Ulaya dhidi ya Iran.