-
Mexico yatupilia mbali tuhuma za Marekani dhidi ya Iran
Jan 18, 2020 23:27Wizara ya Mambo ya Nje ya Mexico imetupilia mbali madai ya hivi karibuni ya gazeti la Kimarekani la Wall Street Journal kuhusiana na upenyaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika eneo la Amerika ya Latini.
-
Njama za Marekani za kutaka kuficha hasara kubwa za shambulizi la makombora ya Iran huko Ainul Asad
Jan 18, 2020 09:13Katika jitihada zake za kutimiza ahadi ya kulipiza kisasi kikali dhidi ya Marekani kutokana na mauaji ya kigaidi yaliyofanywa na nchi hiyo dhidi ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani na wana jihadi wenzake, Alfajii ya Jumatano tarehe 8 Januari Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilishambulia kambi kubwa zaidi ya wanajeshi wa Marekani nchini Iraq ya Ainul Asad.
-
Hotuba za Kiongozi Muadhamu Katika Sala ya Ijumaa Tehran; ubainishaji wa nguvu na adhama ya Iran
Jan 18, 2020 04:23Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika hotuba zake za Sala ya Ijumaa wiki hii mjini Tehran, alisema: "Kushiriki kimuujiza taifa la Iran katika mazishi ya shahidi mtoharifu Qassem Soleimani na wenzake na pia jibu kali la IRGC lililotolewa kwa kushambulia kituo cha Ainul Assad cha Jeshi la Marekani (nchini Iraq) ni siku mbili ambazo zinaweza kutajwa kuwa Siku za Mwenyezi Mungu (Ayamullah). Siku hizi zimejaa somo na ibra na ni za kuainisha hatima."
-
Pendekezo la mazungumzo mapya ya nyuklia linaonesha udhaifu wa Ulaya
Jan 18, 2020 04:07Balozi wa Iran mjini Paris amesema pendekezo la kutaka kufanyika mazungumzo mapya kuhusu miradi ya nyuklia ya Iran linaonesha udhaifu wa Ulaya na ni dhihirisho wazi kuwa nchi hizo zina uepesi wa kuvunja mapatano.
-
Iran na India; juhudi kwa ajili ya kutumia sarafu ya taifa na kupanua ushirikiano wa kiuchumi
Jan 17, 2020 09:02Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekutana na kufanya mazungumzo mjini New Delhi na Narendra Modi, Waziri Mkuu wa India na kujadili suala la kupanua ushrikiano wa kiuchumi baina ya nchi mbili na kuchukua hatua za kuondoa baadhi ya matatizo yaliyopo katika njia hiyo.
-
India yasema ina hamu ya kuimarisha uhusiano wake na Iran
Jan 17, 2020 04:10Waziri Mkuu wa India amesema nchi yake ina hamu kubwa ya kuimarisha uhusiano wa pande mbili na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyuga tofauti.
-
Askari wa US waliojeruhiwa na makombora ya Iran wanatibiwa Ujerumani na Kuwait
Jan 17, 2020 03:54Licha ya utawala wa Washington hapo awali kudai kuwa hakuna askari wa Marekani aliyeuawa au kujeruhiwa katika majibu makali yaliyotolewa na Iran dhidi ya kambi mbili za kijeshi za nchi hiyo huko Iraq, lakini hivi sasa imefichuka kuwa, wanajeshi kadhaa wa US waliojeruhiwa walipekwa kwa usafiri wa ndege katika nchi za Ujerumani na Kuwait kwa ajili ya matibabu.
-
Meja Jenerali Baqeri: Marekani itapata jibu kali zaidi la Iran ikiendeleza mienendo yake hasi
Jan 17, 2020 00:00Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema iwapo Marekani itaendeleza chokochoko na mienendo yake hasi dhidi ya taifa hili, basi iwe tayari kupokea jibu kali zaidi la Iran ya Kiislamu.
-
Kufichuka siri ya Trump alivyoishinikiza Troika ya Ulaya itekeleze 'Utaratibu wa Kifyatuo' katika JCPOA
Jan 16, 2020 23:18Licha ya madai zinayotoa nchi za Ulaya kuhusu ulazima wa kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, Troika ya nchi hizo inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, siku ya Jumanne ya tarehe 14 Januari iliamua kutekeleza utaratibu wa kusuluhisha mzozano katika JCPOA, ambao kimsingi unatoa kitisho kwa Iran cha kuwekewa tena vikwazo vya nyuklia vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Kikao cha kumuenzi na kumkumbuka Jenerali Soleimani chafanyika Kodivaa
Jan 14, 2020 09:40Waislamu wa Ivory Coast wamefanya kikao cha kumuenzi na kumkumbuka Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na mashahidi wenzake waliouawa hivi karibuni na askari magaidi wa Marekani nchini Iraq.